Tuesday, 21 May 2013

POLISI AMCHARANGA MAPANGA MWANAYE KISA MAPENZI



KATI ya stori za mwaka zinazosikitisha, hii ni mojawapo! Polisi mstaafu, mkazi wa Kitongoji cha Sango, Kata ya Nyasubi wilayani Kahama mkoani hapa, Samson Bwire (54), anashikiliwa na jeshi la polisi kwa kumcharanga mapanga binti yake, Devotha Gerald (4), kisa kikidaiwa ni wivu wa kimapenzi.
Tukio hilo lilitokea Mei 16, mwaka huu, majira ya jioni nyumbani kwa Bwire alipokuwa akigombana na mke wake, Happiness Elias (28).
Kwa mujibu wa mashuhuda, baba Devotha anadaiwa kufanya tukio hilo huku akiwa amelewa tilalila.
Habari zilidai kuwa, mwanaume huyo alikuwa kwenye ugomvi wa kimapenzi na mkewe ambapo katika purukushani akimtuhumu mama Devotha kumsaliti, mkewe huyo alifanikiwa kuchoropoka.
Ilidaiwa kuwa baada ya mama Devotha kuchoropoka ndipo baba huyo akamgeuzia kibao Devotha na kumalizia hasira zake kwa kuanza kumkatakata kwa panga bila huruma.
Kwa mujibu wa majirani, kelele zilisikika kutoka kwenye familia hiyo na kwamba walipokwenda walimkuta baba Devotha akichoma nguo za mkewe na alipowaona, aliingia ndani na kuanza kumkata mapanga mtoto huyo huku akiwa amefunga mlango.
Ilifafanuliwa kwamba baada ya kusikia kelele za mtoto, majirani walianza kuvunja mlango huku wakiomba msaada kutoka kwa polisi na baada ya polisi kufika walifanikiwa kumnusuru mtoto akiwa amejeruhiwa vibaya.
Kufuatia hali mbaya ya mtoto aliyekuwa amelowa damu kichwani, majirani walishindwa kuzuia hasira zao na ndipo walipoanza kumpiga Bwire ambaye ni askari polisi mstaafu wa cheo cha koplo.
Katika hali kama hiyo, ilibidi polisi wafanye kazi ya ziada kumnusuru baba Devotha na kumpakia kwenye gari kwenda kituoni.
Hata hivyo, wakati gari la polisi likiwa katika mwendo wa kasi eneo la Soko la Mkulima, baba Devotha aliruka kutoka kwenye gari na kuangukia lami, kitendo kilichomsababishia majeraha makubwa sehemu za usoni.
Mtoto Devotha na baba yake, wote walikimbizwa na kulazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Kahama kwa matibabu huku Bwire akiwa chini ya ulinzi mkali wa polisi ikiwa ni pamoja na kufungwa pingu.
chanzo:globalpublishers

Monday, 20 May 2013

Nine in ten parents want online porn automatically blocked by the Government



Parents overwhelmingly support calls for the Government to impose an automatic block on online pornography, headteachers have revealed.
The National Association of Headteachers (NAHT) found nine out of ten parents want a default setting on computers and smartphones which prevents the viewing of adult material.
The dramatic survey figures reveal 90 per cent of parents wanted the default block on porn sites. 
Two-fifths are so worried about the ease with which it can be found – often by mistake – that they want children as young as five to have guidance in classes
Half thought advice should be given to children once they reach the age of 13.
Only 7 per cent thought it was never appropriate to discuss the issue in class.
And just one in eight parents felt they were able to sufficiently educate their children about the dangers of what they can find online without the help of teachers and support from schools.

Mawaziri watatu kung’olewa


UPEPO mbaya ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) unazidi kuvuma, safari hii wabunge wake wakimtaka Rais Jakaya Kikwete kuwafukuza kazi mawaziri watatu.
Mawaziri wanaotakiwa kung’olewa ni Dk. Shukuru Kawambwa (Elimu na Mafunzo ya Ufundi), Dk. Mathayo David Mathayo (Mifugo na Maendeleo ya Uvuvi) na Dk. Fenella Mukangara (Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo).
Kama Rais Kikwete atakubali kuwaondoa madarakani mawaziri hao, hii itakuwa mara ya pili kwake kufanya hivyo. Mara ya kwanza ilikuwa Mei mwaka jana.
Mwaka jana Rais Kikwete aliamua kuwaengua madarakani baadhi ya mawaziri waliokuwa wakiandamwa kwa tuhuma mbalimbali, ikiwemo uwajibikaji mbovu.
Miongoni mwa walioenguliwa mwaka jana ni Dk. Haji Mponda aliyekuwa Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Mustafa Mkulo (Waziri wa Fedha), William Ngeleja (Nishati na Madini na Ezekiel Maige (Maliasili na Utalii).
Msimamo huo wa wabunge wameutoa jana katika kikao baina yao na Rais Kikwete kilichokuwa kikitathimini mwenendo wa chama na utendaji wa wabunge.
Chanzo chetu ndani ya kikao hicho kilieleza kuwa baada ya Rais Kikwete kutoa hotuba ya ufunguzi, baadhi ya wabunge walianza kuchangia, huku wengine wakishutumiana kwa kuvujisha siri za vikao nje kwa waandishi wa habari.
Wabunge hao walidai kuwa mawaziri hao watatu wamekuwa mzigo kwa Serikali ya CCM kutokana na utendaji wao kutokuwa wa kuridhisha.
Walisema matunda ya uwepo wa mawaziri hao kwenye wizara husika hayaonekeni, hivyo kumtaka Rais Kikwete awang’oe.
Waziri Kawambwa analaumiwa kwa kuzembea kwenye sekta ya elimu ambayo inazidi kushuka kiasi cha kuifanya serikali ifute matokeo ya kidato cha nne ya mwaka jana.

SIKILIZA SONGI JIPYA LA: shilole - paka la bar

Polisi wakamatwa na bangi gunia 18


SIKU chache baada ya Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam kuwakamata askari 16 wakituhumiwa kujihusisha na biashara ya magendo, askari wengine wawili wa jeshi hilo wamekamatwa mkoani Kilimanjaro wakiwa na shehena kubwa ya bangi wakiisafrisha kwenda nchini Kenya.
Askari hao walikamatwa Mei 19 mwaka huu saa nne usiku eneo la Kilemapofu, Wilaya ya Moshi Vijijini wakiwa na magunia 18 ya bangi ambayo walikuwa wameyapakia kwenye gari la Mkuu wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) mkoani Arusha aina ya Toyota Land Cruiser lenye namba PT 2025.
Akithibitisha kukamatwa kwa askari hao, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Robert Boaz alisema askari hao walikuwa wakipeleka bangi hiyo Wilaya ya Rombo kwa mfanyabiashra mmoja ambaye hakutaka kumtaja jina lake.
Kamanda Boaz aliwataja askari waliokamatwa na wanashikiliwa kwenye kituo kikuu cha polisi katika mji mdogo wa Himo kuwa ni F.1734 Koplo Edward (dereva) wa kikosi cha kutuliza ghasia (FFU) mkoani Arusha na G.2434 Konstebo George wa kituo cha polisi Ngarenanyuki Wilaya ya Arumeru.
Alibainisha kuwa kukamatwa kwa askari hao kunatokana na operesheni ya kukabiliana na dawa za kulevya inayofanywa na polisi katika mikoa ya Arusha na Kilimanjaro.
Alisema operesheni hiyo imefanyika kikamilifu katika Mkoa wa Arusha uliokuwa ukitumika kupitishia bidhaa hiyo, na sasa wahusika wameamua kuutumia Mkoa wa Kilimanjaro.
“Baada ya kuwahoji askari wale, walidai kuwa walikodishwa na mfanyabiashara huyo kuipeleka bangi hiyo wilayani Rombo tayari kwa kusafirishwa kwenda nchini Kenya ambako inaaminika kuna soko kubwa,” alisema.

Kibanda kuliteka Bunge leo


TUKIO la kutekwa na kuumizwa vibaya kwa Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri nchini (TEF), Absalom Kibanda linatarajia kuteka mjadala wa Bunge leo.
Jambo hilo linatarajiwa wakati wa kujadili hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kwa mwaka 2013/2014 itakayowasilishwa bungeni leo.
Kibanda ambaye pia ni Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya New Habari (2006), alivamiwa na watu wasiojulikana usiku wa Machi 6 mwaka huu, nyumbani kwake Mbezi Juu jijini Dar es Salaam.
Mhariri huyo akiwa getini kwake akisubiri kufunguliwa, akapigwa kwa nondo kichwani, kutobolewa jicho la kushoto, kukatwa kidole, kung’olewa kucha na meno mawili.

Mulongo: Arusha ipo nyuma matumizi ya vyoo

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo, amekerwa na tabia ya baadhi ya wananchi mkoani hapa kutokutumia vyoo na badala yake wanajisaidia holela na kuchafua mazingira.

Amesema mkoa huu ni miongoni mwa mikoa ambayo bado iko nyuma katika matumizi ya vyoo.

Amesema uchafuzi unaofanywa wa kujisaidia hovyo unaharatisha afya za watu kwa kuambukizwa maradhi ya milipuko.

Alisema hayo mwishoni mwa wiki katika hotuba yake iliyosomwa na Mkuu wa Wilaya ya Monduli, Jowika Kasunga, wakati wa ufunguzi wa semina elekezi ya viongozi wa mkoa kuhusu utekelezaji wa kampeni ya kitaifa ya usafi wa mazingira ya miaka minne ambayo inafanywa mashuleni na kwenye kaya.

Alisema lengo la kitaifa linaitaka mikoa iwe na matumizi ya vyoo katika mashule na kaya na kwamba mkoa huo unafanya uhamasishaji wa kutekeleza malengo hayo kutoka asilimia 12 hadi kufikia asilimia 53 ifikapo mwaka 2015.

Saturday, 18 May 2013

Huu ndio WARAKA wa Vinega “AntiVirus” kuhusu Ruge na Kusaga dhidi ya JayDee

Ni wazi na dhahiri kabisa kesi iliofunguliwa mahakamani dhidi ya Lady JayDee haina maana yoyote isipokuwa ni hofu ya mafisadi wa muziki nchini (Kusaga na Ruge) kwa kuwa waraka wa piliulikuwa utoke tar 15 may na mwingine tar 17 may mwaka huu wa 2013.
Hapa la kujiuliza ni juu ya interview ya Rugen a kinachoendelea sasa,eti suala limefika mahakamani,kweli Kusaga na Ruge mmeweza kuthibitisha nyie ni mafisadi na mnamuaibisha Rais Kikwete ambaye nina uhakika anajua kuwa nyie ndio kikwazo kikubwa na hata Bungeni alishawahi kuzungumza kuwa alitoa studio na pango kumbe tatizo sio hilo,tujiulize wote kuna nini wanachoficha hadi kumtafutia kesi raia mwema asie na hatia?
Tena anaejitafutia rizki ambayo wao wanapigana nayo kwa kumkandamiza?
Huku wakitumia mabavu wakilindwa na baadhi ya viongozi wa serikali na waandishi ambao majina yao mtayapata kupitia nyaraka zinazokuja (zipo 88) na huu ndio wa kwanza.
Nimesikitika sana na njia pekee ya kuufahamisha umma juu ya ufisadi huu wa Ruge Mutahaba na Joseph Kusaga ni kuyaanika yote ambayo jamii na Viongozi wa Serikali kama mlikuwa hamjui sasa ndio wakati muafaka wa kuwajua watu hawa ambao kila kukicha ni kuimarisha ufisadi wao na kujipendekeza kwa Viongozi sambamba na watoto wao (mtajua mpaka majina yao)

Naanza kupatwa na wasiwasi nikijiuliza, endapo Lady JD angekuwa amegombana na msanii mwenzake mkubwa kama Prof Jay, Ray C au Juma Nature wanasiasa wangeingilia kati? Ni wazi wasingesogea kwa kuwa hakuna maslahi zaidi ya kuingilia mgogoro huu ambao hawataki jamii ijue maovu yao.

Napatwa mashaka jinsi wanasiasa wanavyolivalia njunga jambo binafsi
Kama hili na kulifanya ni la kiserikali basi tafuteni chanzo cha tatizo mjue ni sehemu gani sahihi ya kuanza kutatua kilichopo na sio kukimbilia kuunda vikao ambavyo naamini vimeshaitishwa vingi sana lakini hakuna kilichosaidia.
Wanasiasa badala ya kutafuta sababu zinazofanya wasanii wanalalamika mnakimbilia kutatua mgogoro wa Ruge na JD ili kusuluhisha mambo yasiendelee kuongelewa jamii ijue uovu wa mafisadi hawa.
Haitasaidia kwa sababu wanaojua maovu ya hawa mafisadi Rugen na Kusaga ni wasanii wengi wakubwa na watu wengine binafsi (kumbukeni waraka zipo 88)

Vijana mnaowategemea katika kampeni zenu na mnawaita Taifa la kesho, lakini mnakubali waendelee kukandamizwa na kunyanyasika huku wakizidi kuwaneemesha kina Ruge na Kusaga.
Tatizo mnalijua kaeni na wasanii wote wawaelezee matatizo yao, msikae na wasanii ambao wanaamrishwa na kina Ruge. Sikilizeni kilio cha wasanii wengine pia na itafutwe njia ya kupata maoni ya kila mmoja na kuachana na watu wengine ambao wanaendesha mtandao wa ufisadi chini ya kivuli cha Ruge (Said Fella na Babu Tale) ambao mtapata kujua kila kitu kuhusu ufisadi wao na kinachoendelea (kumbuka waraka zipo 88)

Ruge Mutahaba amekuwa ni tatizo na janga la Kitaifa katika tasnia ya muziki kwa ujumla, amekuwa akiwagawa wasanii kwa kutumia redio Clouds kwa vitisho vya kutopigiwa nyimbo, au kwa danganyio la kufanyiwa promotion mpaka kwenye magazeti endapo tu utakuwa chini ya bawa lake.
Wasanii wamekuwa hawalipwi vizuri ili waendelee kumtegemea fisadi huyu.
Kwani wasanii wote wangekuwa na kipato cha kuweza kusimama imara leo hii kauli kama ya Lady JD ingezungumzwa karibu na kila mwanabongoflava.

Fred Kavishe (fisadi mwingine) ambae anasimamia Kili music awards yuko bega kwa bega na Ruge kudanganya wananchi nani ni bora katika tuzo hizo ili kulinda maslahi yao binafsi.
Na wao huchagua wale wasanii ambao hawana sauti za kudai haki yao ili wawatumie kadri wanavyotaka.Tuzo za Kili ni uozo mtupu.Imefikia wakati basata itoe vibali kwa wadau wengine wa muziki (nako kuna ufisadi)wasio na interest binafsi na wasanii wao, kuendesha hizi shughuli ili kukuza muziki.Kutokuwepo na tuzo zingine kunasababisha ionekane kuwa basata nao wamo kwenye mgao wa mabepari hao wanaoua sanaa ya Tanzania

JINSI RUGE NA KUSAGA WANAVYOTAWALA
Njia anayoitumia Ruge na Kusaga iko wazi, wao wana redio na hapo hapo wana wasanii wao.Hivyo promotion inabidi wafanyie wasanii wao ambao ni waoga ili waweze kuwatumia bila wasanii hao kufanya fyoko fyoko.

Wasanii wengine ambao sio chini ya Clouds kwa kuwa hawana jinsi nyingine ya kupata hela inabidi wainyenyekee Clouds wakiamini ndio njia pekee ya kuwapatia vipato
Huku wakisubiri show moja ya fiesta ya kila mwaka.
Huko katika fiesta kuna wengine wanalipwa mpaka laki tatu na bado katika hiyo ili upangwe kwenye list ya kupanda jukwaani B12 nae lazima akate laki moja yake.
Hapo msanii anabakiwa na nini akirudi nyumbani?
Hivi laki tatu ni nini kwa maisha ya msanii?
Njia pekee ya kuwatawala ni kuwafanya waendelee kuwa maskini.
Leo hii mtangazaji wa redio ana sauti kuliko msanii.

Kwanini redio zingine hazilaumiwi? Ni kwa sababu hazijihusishi moja kwa moja na wasanii.Hilo ni kosa kubwa sana linalofanywa na Clouds au pengine ndio mtazamo wao walioamua kuufuata kwa sababu wanaamini Serikali ipo mikononi mwao.
Maisha na ajira za watoto wa watu ambao wengi hawajasoma wanategemea vipaji, mnayakatili bila huruma

Mwisho tumuombee Lady JD Mahakama imruhusu azungumze yote, kila mtu anataka kusikia sio siri Clouds, Ruge na Kusaga ni nyonya damu.
Mahakama itambue kuwa wanaojua maovu ya Rugen a Kusaga sio Lady JayDee pekee ni wengi mno na kama njia ya kukimbilia mahakamani ndio wameichagua basi ongezeni mahakama kwa kuwa tupo wengi tutakuja kuyaongea kuhusu mafisadi hawa wa Clouds (siku hizi wanaitwa wafu)
Hela ina nguvu hata palipo na haki, JD hajatukana matusi na amekuwa makini katika kutoa kauli zake sasa anashitakiwa kwa kosa gani? Anashitakiwa kwa kudai haki yake. Anaconda wewe songa na sisi tunakuja kizimbani na sasa ndio TANZANIA itawajua Rugen a Kusaga ni kina nani na walianzia wapi,walikuwa wapi,wako wapi na nani wanaoshirikiana nao

chanzo:https://www.facebook.com/antivirusvinega?hc_location=timeline

Friday, 17 May 2013

Hivi ndivyo Waziri Magufuli alivyovunja mbavu Bungeni Dodoma

WAZIRI wa Ujenzi, Dk. John Pombe Magufuli ndiye waziri namba moja hadi sasa kwa kulivunja mbavu Bunge la Bajeti linaloendelea mjini Dodoma kutokana na vichekesho vyake wakati alipokuwa akijibu hoja za wabunge mbalimbali hivi karibuni.
Magufuli ambaye wengi humuita ‘Jembe’ kutokana na uchapa kazi wake, alikuwa akiwasilisha bajeti ya wizara yake na kuomba kuidhinishiwa Shilingi Trilioni 1.22 kwa mwaka wa fedha 2013/14.

Mheshimiwa huyo alimudu kuwafanya waheshimiwa wacheke sana huku ujumbe ukifika tofauti na mawaziri wengine waliopita ambao hotuba zao zinadaiwa kuwa zilijaa ushawishi wa usingizi.
“Tunajenga barabara kwa kiwango cha lami kutoka Dodoma kwenda Iringa, wale watani zangu wa Iringa hawatakuwa na haja ya kujinyonga kwenye miti, sasa watakuwa wakilala barabarani tu.”
Wabunge walivunjika mbavu kwa vicheko. Watani zake alimaanisha Wahehe ambao inadaiwa wanapokuwa na hasira wana tabia ya kujiua kwa kujinyonga (ni madai).
Kama vile haitoshi, waziri huyo akijibu swali la Mbunge wa Same Mashariki, Mheshimiwa Anne Kilango Malecela kuhusu barabara inayopita kwenye Kiwanda cha Tangawizi kupewa hadhi, pia alitumbukiza utani.
“Mheshimiwa Anne Kilango yale uliyosema tunayafanyia kazi, kuhusu barabara inayopita Kiwanda cha Tangawizi kupewa hadhi tumepokea, maana pia mheshimiwa rais alitupa maagizo.
“Nimeamini una akili sana ndiyo maana mtani wangu Malecela alitoka Dodoma na kwenda milimani Same huko, kwa nini hakuja usukumani?”
Aidha, waziri huyo akimjibu Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari ambaye alitoa ushauri kwa Wizara ya Ujenzi kupunguza idadi ya miradi na kukamilisha mmoja baada ya mwingine ili wizara iweze kufanikiwa huku akilalamikia kutojengewa barabara jimboni kwake, Magufuli aliwavunja mbavu tena wabunge:
“…ushauri wako ni mzuri ndiyo maana wizara yangu imeamua kuacha kujenga barabara jimboni kwako ili tukamilishe sehemu nyingine kwanza…”
Hata hivyo, wakati wabunge wakivunjika mbavu, Magufuli alisema Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) haina ubaguzi na itajenga barabara hiyo iliyoko jimboni kwa mbunge huyo.
Akimjibu Mbunge wa Viti Maalum (CCM –Bunda), Ester Bulaya ambaye alisema kwamba anamkubali waziri huyo kutokana na utendaji wake, Magufuli naye alisimama na kusema:
“Hata mimi namkubali Ester Bulaya...”

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...