Kaskazini mwa Mali nusu yake inaendeshwa na waasi wa Tuareg na wapiganaji wa Kiislam baada ya mapinduzi katika mji mkuu wa Mali.
Aguelhok katika eneo la Kidal alikuwa ni wa kwanza kukamatwa na waasi wa Tuareg .
Waislamu katika eneo la Aguelhok waliwapiga mawe mpaka kufa watu hao mbele ya watu 200 maafisa wamesema.
"Nilikuwepo. Wapiganaji hao wa Kiislamuwaliwachukua watu hao katikati ya Aguelhok. Watu hao waliwekwa kwenye mashimo mawili na wakapigwa mawe mpaka wakafa." Afisa wa serikali eneo hilo alisema.
"Mwanamke alizimia mara baada tu ya mapigo," alisema, akiongeza kuwa mwanaume alipiga kelele mara moja tu na baadaye akanyamaza.
chanzo:bbc
No comments:
Post a Comment