Friday, 28 September 2012
Waliotoswa CCM wafichua siri:FILIKUNJOMBE ADAI YEYE, MKONO, LUGOLA WALIPONZWA NA PINDA, NAPE ATAKA WASIORIDHIKA WAKATE RUFAA, WASOMI WAPONGEZA
SIKU moja baada ya Halmashauri Kuu ya CCM (Nec), kutangaza majina ya wagombea, baadhi ya vigogo walioachwa kwenye uteuzi huo wameeleza ya moyoni, huku Mbunge wa Ludewa, Deo Filikunjombe akisema anaamini ametoswa kwa sababu alitia saini ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.
Katika Bunge la 10 lililoketi Aprili mwaka huu, baadhi ya Wabunge wa CCM akiwamo Filikunjombe, Mbunge wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono na Mbunge wa Mwibara, Kangi Lugola, waliunga mkono hoja ya kutokuwa na imani na Pinda iliyokuwa imeanzishwa bungeni na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe wa Chadema.
Wabunge hao wa chama tawala, waliungana na wenzao wa upinzani kutaka kupiga kura za kutokuwa na imani na Pinda kutokana na kile kilichoelezwa kuwa ameshindwa kuisimamia Serikali kwa kuwawajibisha mawaziri wazembe.
Hata hivyo, mpango huo haukufanikiwa baada ya Spika wa Bunge Anne Makinda kueleza kuwa haukufuata taratibu zinazotakiwa.
Filikunjombe alipotakiwa jana kuzungumzia kuenguliwa kwake kwenye kinyang'anyiro cha uchaguzi wa ndani ya chama, alisema anaamini yeye na wenzake hao wa CCM, wametoswa kwa sababu ya kushiriki mpango wa kumng'oa Waziri Mkuu Pinda.
Hata hivyo, alisema amelazimika kukubali hali hiyo na kupokea matokeo, kwa kuwa hatua yake ya kusaini kitabu hicho ilitokana na nia njema kutaka Waziri Mkuu ajiuzulu ili mambo fulani muhimu katika jamii yafanyike.
Filikunjombe alibainisha kuwa alisaini kitabu hicho cha kutokuwa na imani na Pinda akiwa na akili timamu na alikuwa anajua kinachoweza kutokea kutokana na hatua yake hiyo.
Filikunjombe alibainisha kuwa alisaini kitabu hicho cha kutokuwa na imani na Pinda akiwa na akili timamu na alikuwa anajua kinachoweza kutokea kutokana na hatua yake hiyo.
"Nimesaini kitabu kile kwa nia njema, nikiwa na akili timamu na sijutii uamuzi wangu huo, ila siwezi kuwasemea Kigwangalla (Khamis mbunge wa Nzega) na Bashe (Hussein). Lakini sisi watatu (yeye, Lugola, Mkono) tumeenguliwa kwa sababu hiyo (ya kutokuwa na imani na Pinda)."
Aliendelea: "Nashangaa leo naonekana adui wa chama wakati nilikuwa nakinusuru na kusema kweli adui wa CCM ni Wabunge wa chama hicho ambao hawakusaini kitabu hicho cha kutokuwa na imani na Waziri Mkuu, " alisema Filikunjombe.
Mkono
Mbunge wa Musomo Vijijini, Nimrod Mkono alisema kutoswa kwake ni uamuzi wa watu aliowaita wenye chama.
"Walikata jina langu nikakata rufaa, likarudishwa Dodoma, lakini walipokutana wakaona sifai. Wakaamua kunifukuza sasa hapo mimi nifanye nini?" alihoji Mkono.
Mbunge wa Musomo Vijijini, Nimrod Mkono alisema kutoswa kwake ni uamuzi wa watu aliowaita wenye chama.
"Walikata jina langu nikakata rufaa, likarudishwa Dodoma, lakini walipokutana wakaona sifai. Wakaamua kunifukuza sasa hapo mimi nifanye nini?" alihoji Mkono.
Mkono alisema huu ni utaratibu wa chama chao cha CCM ambao umewapa baadhi ya watu haki ya kuwafukuza wengine bila kuwapa fursa ya kujitetea.
"Kama ilivyotokea kwangu wamekaa na kuona Mkono hafai, fukuza basi wakafanya hivyo na hiyo haijalishi kama nilisaini kutokuwa na imani na Waziri Mkuu au la. Suala la msingi ni kuwa Mkono amefukuzwa na atarudi kama ilivyokuwa kwa mwana mpotevu." alisema bila kufafanua.
Kigwangalla
Mbunge wa Nzega, Dk Hamis Kigwangalla alisema anaheshimu uamuzi wa vikao vilivyokaa na kufikia uamuzi uliochukuliwa na kwamba, ataendelea kuwa mwanachama na kukitumikia chama pamoja na wananchi kwa nguvu zote bila kinyongo.
“Nitaendelea kuheshimu vikao vya chama changu na kuwa mwanachama hai ingawa sijajua wametumia vigezo gani kuteua majina hayo,” alisema Dk Kigwangalla.
Mbunge wa Nzega, Dk Hamis Kigwangalla alisema anaheshimu uamuzi wa vikao vilivyokaa na kufikia uamuzi uliochukuliwa na kwamba, ataendelea kuwa mwanachama na kukitumikia chama pamoja na wananchi kwa nguvu zote bila kinyongo.
“Nitaendelea kuheshimu vikao vya chama changu na kuwa mwanachama hai ingawa sijajua wametumia vigezo gani kuteua majina hayo,” alisema Dk Kigwangalla.
WATU 11 WAUAWA WAKILA KIAPO NCHINI KENYA
Mkuu wa Polisi eneo la Pwani ya Kenya Bwana Aggry Adoli amethibitisha tukio hilo akisema kuwa wanakijiji waliwaona watu walioshukiwa kuwa wanachama wa MRC wakiingia msituni na kuwafuata na kisha kuwaua baadhi ya watu waliokuwa kwenye kundi hilo.
Duru zinasema kuwa watu hao walikuwa miongoni mwa watu walioshukiwa kuwa majambazi.
Walikamatwa na silaha za kijadi kama vile panga na visu. Polisi wanasema kuwa mmoja wao alikuwa mganga wa kienyeji
Eneo la Pwani mwa Kenya limekuwa na migogoro ya kila aina kuanzia kwa uhasama kati ya jamii hasimu zinazoishi pembezoni mwa mkoa huo.
Polisi wamekua wakilaumiwa kwa kukosa kudhibiti ulinzi mkoani humo hasa wakati huu wa heka heka za maandalIzi ya uchaguzi utakaofanyika mwezi Machi mwaka ujao.
Hata hivyo bwana Adoli anasema kuwa utovu wa usalama sio kosa la polisi bali ni kutokana na matatizo yanayokumba jamii za eneo hilo.
chanzo:bbc
Thursday, 27 September 2012
MAJAMBAZI WADAIWA KUDUNGA WATU SINDANO ZA SUMU!!!
Habari kutoka kata za Kilema Kusini, Kilema Kaskazini na Marangu zinadai kuwa mtandao wa majambazi hao wapatao 30, umekuwa ukilipiza kisasi kwa wananchi wanaojitokeza kutoa ushahidi polisi.
Wananchi hao wamependekeza kutumika kwa sheria ya kuwaweka kizuizini watuhumiwa, ili kuepuka uwezekano wa kuua watu.
Habari zilizozagaa katika Kijiji cha Makami Juu, zilidai kuwa usiku wa Septemba 11 mwaka huu, majambazi walimvamia mfanyabiashara, Respich Ngowi na kumuua kwa kumdunga sindano ya sumu.
“Waliiba kila kitu na wakamdunga sindano ya sumu, watu hawakuthubutu kutoka nje ya nyumba wakihofia kukatwa mapanga na kufuatiliwa na mtandao huo wa majambazi,”alidai mwananchi mmoja.
Wananchi hao walidai kuwa uchunguzi wa mwili wa marehemu uliofanywa na madaktari, ulithibitisha kuwa mfanyabiashara huyo alichomwa sindano mbili za sumu.
Mtandao huo ndio unaotuhumiwa kuilipua kwa petrol, nyumba ya Mwenyekiti wa Kijiji cha Kiraracha, Andrew Lekule na kuteketeza mkewe na mtoto wao mdogo wa umri wa miaka mitano.
Mkazi mwingine wa Kijiji cha Kitowo huko Kilema ,alidai kuwa mtandao huo ni kama umejitangazia “uhuru” kwa sababu unafanya uhalifu wakati wowote wanapojisikia kufanya hivyo.
“Ukiuza nguruwe wanakufuata usiku na hata ukiuza mti wako wanakuja na mapanga wanataka pesa za mauzo. Hali si nzuri hata kidogo karibu kata nzima ya Kilema Kaskazini,”alidai.
Hata hivyo mkazi wa Kijiji cha Ruwa alilidokeza gazeti hili kuwa pamoja na jitihada za polisi kukamata washukiwa lakini wananchi hawataki kutoa ushirikiano ikiwamo kuwatambua wahalifu.
“Tatizo hapa ni wananchi ambao hawana mwamko wa ulinzi shirikishi, yaani mtu anavamia nyumbani na anapiga yowe la kuomba msaada, lakini hakuna jirani anayetoka na kutoa msaada”alidai.
Mwananchi huyo ambaye naye hakupenda jina lake litajwe, alidai kuwa kama wananchi wangekuwa na umoja, wangeweza kusambaratisha mtandao huo.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kilimanjaro, Robert Boaz, alikiri kuwapo kwa matukio ya ujambazi, lakini alisema tatizo ni wananchi wanaokataa kuwatambua washukiwa wala kutoa ushahidi.
Kwa mujibu wa Kamanda Boaz, hivi karibuni alikwenda katika Kijiji cha Kitowo na kukabidhiwa majina ya washukiwa lakini alipowauliza waliompa majina kama wako tayari kutoa ushahidi, walikataa.
Alisema hivi karibuni waliwakamata watuhumiwa wanane lakini ilibidi watumie utaratibu wa kisheria unaojulikana kama “Binding Over” ambapo mahakama iliwaweka chini ya uangalizi wa miaka miwili.
Katika kipindi hicho, watuhumiwa hao hawatakiwi kufanya kosa lolote la jinai.
Kamanda Boaz alisema kutokana na mazingira ya wananchi kutokuwa na mwamko wa ulinzi shirikishi, Jeshi la Polisi limeanza mchakato wa kuzunguka katika vijiji vyote vya kata hizo, ili kutoa elimu hiyo.
Kuhusu mauaji ya mfanyabiashara Ngowi anayedaiwa kudungwa sindano ya sumu, alisema japo wananchi wamejenga hisia hizo lakini msema kweli ni taarifa ya daktari.
Kamanda Boaz alisema ofisi yake itafuatilia taarifa hiyo ili kujiridhisha kuhusu sababu za kifo hicho.Akizungumza na gazeti hili, Mbunge wa Vunjo, Agustino Mrema (TLP), amelitaka Jeshi la Polisi kujibu mapigo, vinginevyo wananchi watapata hisia kuwa limezidiwa nguvu na majambazi hao.
“Hali ya uhalifu inapanda Kilema na Marangu na polisi wasipojibu mapigo haraka, hali itakuwa mbaya sana na wananchi wako tayari kutoa ushirikiano kuusambaratisha mtandao huo,”alisema.
Chanzo: mwananchi
Tuesday, 25 September 2012
NYETI ZA MUME ZILIZOIBWA NA MKEWE, ZAREJESHWA!!!1
JUMA Ali, 48, mkazi wa Mtoni Wilaya ya Temeke, jijini Dar ambaye hivi karibuni alidai kwamba mkewe aitwaye Hadija Chande 40, amemuibia nyeti zake kimiujiza, katika habari iliyoandikwa na gazeti hili yaMUME: MKE WANGU KANIIBIA NYETI sasa furaha yake imerejea kufuatia mganga mmoja wa kienjeyji kumnyooshea mambo yake.
Akizungumza na Uwazi hivi karibuni, Juma alisema nyeti zake hizo zimerejeshwa na mganga huyo baada ya kutokuwa nazo kwa muda wa miezi miwili.
“Kwa kweli nimeteseka sana ila sasa namshukuru Mungu niko freshi, nyeti zangu zimerudi baada ya kwenda kwa mganga wa kienyeji huko Pwani kufuatia mke wangu kugoma kuzirejesha.
“Ilifika wakati nikahisi sistahili kuendelea kuishi kwa kuwa sikuwa mwanaume niliyekamilika lakini baada ya kushauriwa kwenda kwa wataalam, sasa mambo ni shwari,” alisema Ali.
Awali, mwanaume huyo alidai kuwa, Julai 28, mwaka huu mke wake alitoweka nyumbani na baadhi ya vitu vya ndani, aliporejea akitokea kazini hakumkuta na ndipo matatizo hayo ya kupotelewa na nyeti yalipoibuka.
Sakata hilo lilifika hadi kwenye Baraza Kuu la Waislam Tanzania, Wilaya ya Temeke ili kulitafutia ufumbuzi na Hadija alipotafutwa ili kulizungumzia hakuwa tayari kutoa ushirikiano.
chanzo:http://www.globalpublishers.info
Akizungumza na Uwazi hivi karibuni, Juma alisema nyeti zake hizo zimerejeshwa na mganga huyo baada ya kutokuwa nazo kwa muda wa miezi miwili.
“Kwa kweli nimeteseka sana ila sasa namshukuru Mungu niko freshi, nyeti zangu zimerudi baada ya kwenda kwa mganga wa kienyeji huko Pwani kufuatia mke wangu kugoma kuzirejesha.
“Ilifika wakati nikahisi sistahili kuendelea kuishi kwa kuwa sikuwa mwanaume niliyekamilika lakini baada ya kushauriwa kwenda kwa wataalam, sasa mambo ni shwari,” alisema Ali.
Awali, mwanaume huyo alidai kuwa, Julai 28, mwaka huu mke wake alitoweka nyumbani na baadhi ya vitu vya ndani, aliporejea akitokea kazini hakumkuta na ndipo matatizo hayo ya kupotelewa na nyeti yalipoibuka.
Sakata hilo lilifika hadi kwenye Baraza Kuu la Waislam Tanzania, Wilaya ya Temeke ili kulitafutia ufumbuzi na Hadija alipotafutwa ili kulizungumzia hakuwa tayari kutoa ushirikiano.
chanzo:http://www.globalpublishers.info
Husband and his parents jailed for life for murder of pregnant bride they held down and suffocated because they thought she was 'possessed'
One of the four smothered 21-year-old Nalia Mumtaz while the others held her down, apparently in an attempt to drive out the ‘jinn’ spirit from her body.
The killers included her husband, Mohammed Tauseef Mumtaz – who later claimed she suffocated herself – his parents, Zia Ul-Haq and Salma Aslam, both 51, and his brother in law Hammad Hassan.
The murder of the isolated young woman was said to have been instigated by Mumtaz’s parents.
The four were convicted in July following a three-month trial after a jury ruled they had deliberately smothered her. Mr Justice Keith handed them mandatory life terms yesterday.
He said that, while the murder conviction left no room for doubt about what had happened at the family home in Handsworth Wood, Birmingham, the prosecution had been unable to ‘say for sure’ what the motives behind the killing had been.
The court heard Mumtaz, who suffers from a genetic condition which has left him deformed, married his bride in an arranged ceremony in her homeland of Pakistan.
This was 14 months before she died while six months pregnant with their first child.
Birmingham Crown Court heard that a day before her death in the early hours of a July 2009 morning, Mrs Mumtaz, who spoke no English, had sounded ‘stressed’ when she called her parents to tell them her husband – and others in their neighbourhood – had been suggesting she may have become pregnant during a solo trip to Pakistan.
But the judge said a ‘less unlikely explanation for what happened’ was that the defendants believed Naila had been possessed by a jinn – a mischievous spirit mentioned in the Koran – ‘and that they deliberately smothered her in order to get rid of the jinn’.
The judge added: ‘That’s not an easy thing for those of us in the West to understand, but the evidence (from the trial) was that a belief in jinns is widespread in the community in which they lived.’ During the trial, prosecutor Christopher Hotten QC said family members had told police a person had been present at the house praying ‘to get the spirit out of her’.
Mumtaz claimed his wife had ‘suffocated herself by putting her hand in her mouth and she tried to strangle herself’ and that his parents and Hassan, 24, who all lived at the house, were trying to hold Mrs Mumtaz down to stop her from harming herself. Ambulance staff discovered Mrs Mumtaz unconscious in a bedroom with bruising to her arms and face. She died shortly after being taken to hospital at around 4.30am.Prosecutors said that while ‘complex cultural beliefs’ underpinned the defence case, the defendants had given untruthful accounts.
The court heard Mumtaz suffered from Klippel-Feil Syndrome, a rare genetic disorder which means the neck is shortened. However, it was alleged his bride had willingly entered into the arranged marriage, despite his deformity.
http://www.dailymail.co.uk/news/
http://www.dailymail.co.uk/news/
BEST PHOTO OF THE DAY!!
NEC CCM: Tetemeko
Vigogo kadhaa wakiwamo wabunge wameenguliwa katika mchakato wa uchaguzi ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Majina ya vigogo hao yaliondolewa na Kamati ya Maadili iliyoketi mjini hapa kwa siku tatu mfululizo chini ya Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo.
Rais Kikwete jana asubuhi alisema kazi ya kupitia majina ua wagombea ilikuwa ni ngumu na kwamba Kamati ya maadili ilifanya kazi nzuri na itafanya vikao vinavyofuata kwenda kwa kasi nzuri.
Akifungua kikao cha Kamati Kuu (CC), Rais Kikwete alisema kuwa Kamati ya Maadili imekuja na mapendekezo mengi tofauti na yale yaliyoliyopendekezwa na vikao vya mikoani.
Rais Kikwete alisema Kamati ya Maadili imefanya kazi ya kupitia jina moja hadi jingine ili kufahamu kwa nini waliochwa kupendekezwa wamefanyiwa hivyo.
“Tumefanya kazi ya kupitia jina moja hadi jingine kuona nani amependekezwa na wasiopendekezwa na kwa nini wameachwa na kuna maeneo tumekuja na mapendekezo tofauti na yaliyotolewa mikoani kwa sababu mbalimbali,” alisema.
Alisema wagombea 2,853 waligombea nafasi mbalimbali ndani ya chama na wengine 2,104 waliwania mafasi za uongozi kupitia jumuiya za chama hicho.
Taarifa kutoka ndani ya chama hicho ambazo imelifikia gazeti hili jana, zilisema kuwa waliodaiwa kuenguliwa na kikao hicho ambacho kilimalizika juzi saa 9:30 usiku, ni pamoja na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Khamis Mgeja, anayetetea nafasi yake.
Wengine ni Mbunge wa Viti Maalum, Munde Tambwe anayewania nafasi ya uenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Chama hicho (UWT) mkoani Tabora na Mbunge wa Kahama, James Lembeli.
Kada mwingine ambaye taarifa za uhakika zinaeleza ameenguliwa ni Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) mkoani Dodoma, Antony Mavunde, ambaye anagombea Makamu Mwenyekiti Taifa.
Habari zaidi za uhakika zinasema kuwa wengine ambao majina yao yameondolewa katia orodha ya wagombea ni wabunge Victor Mwambalaswa (Lupa) na Godfrey Zambi ( Mbozi Mashariki).
Zambi na Mwambalaswa walikuwa wanagombea nafasi ya Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mbeya.
Hata hivyo, chanzo chetu kimesema kuwa kuna vigogo wengine ambao wamependekezwa waenguliwe na hivi sasa wanasubiri huruma ya vikao vya CC na Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC).
Kwa mujibu wa chanzo hicho, baadhi wabunge waliowania nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya chama, majina yao yamepitishwa.
Katika mkutano wake na waandishi wa habari, Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, alisema CC imekuwa ikitumia busara katika kupitisha majina ya wagombea wa nafasi mbalimbali kwa maslahi ya chama.
“Hata kanuni inasema kuwa anaweza kugombea kwa kibali maalum cha Kamati Kuu. Majina yanapofika tunasema huyu ni mbunge, tunaangalia je, inafaa tena kugombea nafasi nyingine inaporidhika basi inatoa kibali kwa mtu kuwania nafasi ya uongozi,” alisema.
Alisema CC imewahi kuruhusu na kukataa maombi ya watu mbalimbali kwa hivyo hilo halitakuwa jambo geni kama litatokea katika vikao vinavyoendelea.
Chanzo hicho kilisema kuwa Kamati ya Maadili iliamua kurahisisha kazi ya vikao hivyo kwa kuchambua jina moja baada ya jingine na kutoa mapendekezo yao kulingana na sifa walizonazo wanaomba kugombea nafasi hiyo.
Nape alipoulizwa na gazeti hili jana kuhusiana na taarifa za vigogo hao kuenguliwa, hakudhibitisha wala kukanusha taarifa hizo zaidi ya kusema kuwa hayo ni maneno ya barabarani.
Pia Nape aliwahi kukaririwa na vyombo vya habari akisema kuwa vikao hivyo siyo vya mwisho kutoa maamuzi na kuwa maamuzi hayo yanaweza kubadilishwa na vikao vingine.
Kikao cha mwisho kutoa maamuzi ni NEC ambacho kinatarajiwa kuanza leo.
CHEGENI, KAMANI WAWAGAWA VIJANA BUSEGA
Majina ya vigogo hao yaliondolewa na Kamati ya Maadili iliyoketi mjini hapa kwa siku tatu mfululizo chini ya Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo.
Rais Kikwete jana asubuhi alisema kazi ya kupitia majina ua wagombea ilikuwa ni ngumu na kwamba Kamati ya maadili ilifanya kazi nzuri na itafanya vikao vinavyofuata kwenda kwa kasi nzuri.
Akifungua kikao cha Kamati Kuu (CC), Rais Kikwete alisema kuwa Kamati ya Maadili imekuja na mapendekezo mengi tofauti na yale yaliyoliyopendekezwa na vikao vya mikoani.
Rais Kikwete alisema Kamati ya Maadili imefanya kazi ya kupitia jina moja hadi jingine ili kufahamu kwa nini waliochwa kupendekezwa wamefanyiwa hivyo.
“Tumefanya kazi ya kupitia jina moja hadi jingine kuona nani amependekezwa na wasiopendekezwa na kwa nini wameachwa na kuna maeneo tumekuja na mapendekezo tofauti na yaliyotolewa mikoani kwa sababu mbalimbali,” alisema.
Alisema wagombea 2,853 waligombea nafasi mbalimbali ndani ya chama na wengine 2,104 waliwania mafasi za uongozi kupitia jumuiya za chama hicho.
Taarifa kutoka ndani ya chama hicho ambazo imelifikia gazeti hili jana, zilisema kuwa waliodaiwa kuenguliwa na kikao hicho ambacho kilimalizika juzi saa 9:30 usiku, ni pamoja na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Khamis Mgeja, anayetetea nafasi yake.
Wengine ni Mbunge wa Viti Maalum, Munde Tambwe anayewania nafasi ya uenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Chama hicho (UWT) mkoani Tabora na Mbunge wa Kahama, James Lembeli.
Kada mwingine ambaye taarifa za uhakika zinaeleza ameenguliwa ni Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) mkoani Dodoma, Antony Mavunde, ambaye anagombea Makamu Mwenyekiti Taifa.
Habari zaidi za uhakika zinasema kuwa wengine ambao majina yao yameondolewa katia orodha ya wagombea ni wabunge Victor Mwambalaswa (Lupa) na Godfrey Zambi ( Mbozi Mashariki).
Zambi na Mwambalaswa walikuwa wanagombea nafasi ya Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mbeya.
Hata hivyo, chanzo chetu kimesema kuwa kuna vigogo wengine ambao wamependekezwa waenguliwe na hivi sasa wanasubiri huruma ya vikao vya CC na Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC).
Kwa mujibu wa chanzo hicho, baadhi wabunge waliowania nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya chama, majina yao yamepitishwa.
Katika mkutano wake na waandishi wa habari, Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, alisema CC imekuwa ikitumia busara katika kupitisha majina ya wagombea wa nafasi mbalimbali kwa maslahi ya chama.
“Hata kanuni inasema kuwa anaweza kugombea kwa kibali maalum cha Kamati Kuu. Majina yanapofika tunasema huyu ni mbunge, tunaangalia je, inafaa tena kugombea nafasi nyingine inaporidhika basi inatoa kibali kwa mtu kuwania nafasi ya uongozi,” alisema.
Alisema CC imewahi kuruhusu na kukataa maombi ya watu mbalimbali kwa hivyo hilo halitakuwa jambo geni kama litatokea katika vikao vinavyoendelea.
Chanzo hicho kilisema kuwa Kamati ya Maadili iliamua kurahisisha kazi ya vikao hivyo kwa kuchambua jina moja baada ya jingine na kutoa mapendekezo yao kulingana na sifa walizonazo wanaomba kugombea nafasi hiyo.
Nape alipoulizwa na gazeti hili jana kuhusiana na taarifa za vigogo hao kuenguliwa, hakudhibitisha wala kukanusha taarifa hizo zaidi ya kusema kuwa hayo ni maneno ya barabarani.
Pia Nape aliwahi kukaririwa na vyombo vya habari akisema kuwa vikao hivyo siyo vya mwisho kutoa maamuzi na kuwa maamuzi hayo yanaweza kubadilishwa na vikao vingine.
Kikao cha mwisho kutoa maamuzi ni NEC ambacho kinatarajiwa kuanza leo.
CHEGENI, KAMANI WAWAGAWA VIJANA BUSEGA
MAASKOFU KUWANYIMA WAUMINI SAKRAMENTO!!!
Maaskofu waliopitisha sheria hiyo wamesema kuwa yeyote atakayekosa kulipia kodi ya kanisa ambayo ni asilimia nane ya mapato yao watanyimwa sakramento na kisha kutotambuliwa kama wakatoliki.
Maaskofu hao wameshtushwa na idadi ya watu wanaoendelea kuasi ukatoliki.
Wanasema kuwa hatua kama hii ya kuasi dini itakuwa ni kwenda kinyume kabisa na maadili ya jamii.
Watu wote waliosajiliwa rasmi kama wakatoliki, waprotestandi au wayahudi, hulipa asilimia 8 hadi 9 ya mapato yao ya kila mwaka.
Kodi hiyo ilianza kutozwa karne ya 19 kama fidia ya kutaifishwa kwa mali ya kanisa nchini humo.
Idadi ya wakatoliki nchini Ujerumani ni asilimia 30, lakini idadi ya watu nchini Ujerumani wanaoasi kanisa hilo iliongezeka hadi watu 181,000 mnamo mwaka 2010, huku lawama zikitolewa kwa kashfa nyingi za ngono zilizokumba kanisa hilo wakati huo.
Maaskofu hao wamechukua hatua baada ya kushtushwa na ongezeko la waumini wa kanisa hilo wanaoasi dini, pamoja na profesa mmoja aliyestaafu Hartmut Zapp kutangaza mwaka 2007 kuwa kamwe hatalipa kodi hiyo ingawa atasalia kuwa muumini wa kikatoliki.
Iliarifiwa kuwa profesa huyo alitaka kuendelea kupokea sakramento na kuandelea kutambulika kama mkatoliki ingawa maaskofui walipinga hilo na sasa kesi kati ya profesa huyo na kanisa itafikishwa mahakamani siku ya Jumatano.
chanzo:bbc
Monday, 24 September 2012
UDAKU NA UDAKUZZZ:WASTARA,SAJUKI FULL VITUKO!!!
MASTAA wa filamu Bongo ambao ni wanandoa, Juma Kilowoko ‘Sajuki’ na Wastara Juma hivi karibuni waliwaacha watu hoi kufuatia vituko walivyokuwa wakivionesha, Ijumaa Wikienda liliwanasa kwenye shughuli.
Wawili hao walionesha vituko hivyo kwenye harusi ya mdogo wa Wastara aitwaye Latifa Juma iliyofanyika mwishoni mwa wiki, Tabata jijini Dar.
Katika sherehe hiyo, Wastara aliamua kuweka matatizo yao pembeni na kuanza kukata nyonga kwa staili iliyowaacha hoi maharusi pamoja na watu wengine waliokuwepo kwenye ‘mnuso’ huo.
Achilia mbali hilo, Sajuki naye alipoingia ukumbini hapo aliingia kwa staili ya kucheza kiduku huku mkononi akiwa ameshika kimfuko cha bisi ‘pop corn’.
Vituko havikuishia hapo kwani kuna wakati Wastara alipotakiwa kufika mbele kukata keki, Sajuki alimfuata kwa nyuma na kumshikia gauni lake refu kama mpambe wake na keki ilipokatwa alichukua kipande na kukila hata kabla ya maharusi.
Mpaka wawili hao wanaondoka ukumbini hapo, walikuwa wameacha gumzo kutokana na matukio yao ambayo yaliifanya sherehe hiyo ifane
chanzo:http://www.globalpublishers.info
Wawili hao walionesha vituko hivyo kwenye harusi ya mdogo wa Wastara aitwaye Latifa Juma iliyofanyika mwishoni mwa wiki, Tabata jijini Dar.
Katika sherehe hiyo, Wastara aliamua kuweka matatizo yao pembeni na kuanza kukata nyonga kwa staili iliyowaacha hoi maharusi pamoja na watu wengine waliokuwepo kwenye ‘mnuso’ huo.
Achilia mbali hilo, Sajuki naye alipoingia ukumbini hapo aliingia kwa staili ya kucheza kiduku huku mkononi akiwa ameshika kimfuko cha bisi ‘pop corn’.
Vituko havikuishia hapo kwani kuna wakati Wastara alipotakiwa kufika mbele kukata keki, Sajuki alimfuata kwa nyuma na kumshikia gauni lake refu kama mpambe wake na keki ilipokatwa alichukua kipande na kukila hata kabla ya maharusi.
Mpaka wawili hao wanaondoka ukumbini hapo, walikuwa wameacha gumzo kutokana na matukio yao ambayo yaliifanya sherehe hiyo ifane
chanzo:http://www.globalpublishers.info
DIAMOND KUWASAKA WALIMBWENDE WATAKAOSHIRIKI VIDEO YAKE!!
Mama yake Diamond na dada yake walikuwepo.
MSANII mahiri wa muziki wa kizazi kipya, Naseeb Abdul 'Diamond Platinumz' jana mchana aliendesha zoezi la kusaka vijana watakaoshiriki katika video yake mpya ambayo bado hajaitaja jina.
Usaili huo wa kwanza wenye lengo la kupata vijana wakali 10 wa kiume na 10 wa kike watakaolamba shavu la kutokelezea katika video mpya ya Diamond ulifanyika katika Ukumbi wa Nyumbani Lounge jijini Dar es Salaam.
Kwa upande wa modo wa kiume, washiriki 18 walipita katika mchujo huo wa kwanza ambapo wataitwa katika fainali itakayotangazwa hivi karibuni. Kwa upande wa modo wa kike, washiriki 16 walifanikiwa kupenya katika awamu hiyo.
Usaili huo wa kwanza wenye lengo la kupata vijana wakali 10 wa kiume na 10 wa kike watakaolamba shavu la kutokelezea katika video mpya ya Diamond ulifanyika katika Ukumbi wa Nyumbani Lounge jijini Dar es Salaam.
Kwa upande wa modo wa kiume, washiriki 18 walipita katika mchujo huo wa kwanza ambapo wataitwa katika fainali itakayotangazwa hivi karibuni. Kwa upande wa modo wa kike, washiriki 16 walifanikiwa kupenya katika awamu hiyo.
WAGOMBEA CCM WAPUMULIA MASHINE!!!
Wagombea wa nafasi mbalimbali za Chama Cha Mapinduzi (CCM), ni kama wanapumulia mashine kutokana na idadi kubwa kujitokeza kuwania nafasi moja ikilinganishwa na nafasi halisi.
Kwa siku ya tatu mfululizo, Kamati ya Maadili ya CCM imeendelea kupitia majina ya wagombea mjini Dodoma huku ikieleza kuwa kazi hiyo imekuwa kubwa kutokana na wagombea kuwa wengi.
Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye ameonya kwamba wagombea wanaolumbana nje badala ya kwenye vikao halali vya ndani vya chama hicho , wakitishia patachimbika iwapo Halmashauri Kuu ya Taifa (Nec) ya chama hicho itawaengua, wanaonyesha jinsi walivyo na uwezo mdogo wa kuongoza.
Walioingia katika malumbano ya kisiasa ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta; Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Khamis Mgeja; Mbunge wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono na Mbunge wa Kahama, James Lembeli.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma jana, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, alisema kuwa:
“Unapotaka kuwa kiongozi wa taasisi kubwa moja ya sifa ni uwezo wako wa kuhimili presha, ukiona mtu anapiga kelele barabarani ujue uwezo wake wa kuhimili presha ni mdogo, presha imekuwa kubwa kiasi kwamba hawezi kuhimili inabidi aende kupumua barabarani.”alisema.
Aliongeza kuwa: “Busara itatumika kuamua nani arudi nani asirudi…siasa za leo ni za presha hasa inapofika wakati wa uchaguzi na inapofika siasa za jumuiya. Sasa kama unataka kuiongoza taasisi kubwa kama hiyo lazima uwe na kifua cha kuhimili presha.”
Kuhusu malumbano ya hivi karibuni kati ya Sitta ambaye pia ni Mbunge wa Urambo Mashariki, Nape alisema kuwa: “Hawa wote ni wajumbe wa vikao halali wanasema barabarani sijui labda wamelewa, hawa ni viongozi kama mtu ana agenda yake aje kwenye vikao.”
Nape aliongeza kuwa “Kwa hili nalo wasubiri vikao vitakapofanya maamuzi, wakiona wana maoni hai wanayofursa ya kuja kusema katika vikao, kwa sababu hatutafanyia kazi maoni barabarani."
Kuhusu mgogoro wa kada wa chama hicho, Hussein Bashe na Mbunge wa Nzega, Dk. Hamisi Kingwallah, alisema hilo linashughulikiwa na Kamati ya Maadili ya Chama hicho.
Alisema kama watabainika kuwa na makosa basi kikao hicho kitatoa adhabu ambayo si lazima itangazwe hadharani.
Akizungumzia kuhusiana na kuchelewa kuanza kwa vikao vya Kamati Kuu na Halmashauri Kuu, Nape alisema idadi kubwa ya waliojitokeza kugombea inaonyesha kukubalika kwa chama mbele ya wananchi.
“Vikao vya chini vinachokifanya ni kuweka alama tu kuanzia A hadi E ambayo inaonyesha kuwa haufai kabisa…Tafsiri kwamba vikao vya chini havikufanya kazi yake vizuri si kweli, vikao vya chini vilifanya kazi nzuri sana,”alisema Nape.
Alisema kuna watu ambao watakuwa wametoa malalamiko ni lazima vikao hivyo viangalie kwa kigezo cha mahitaji ya wakati huo yakoje.
Aidha imebainisha kuwa mchujo wa wagombea wa nafasi mbalimbali ndani ya CCM inaweza kuchukua muda mrefu kuliko ilivyotarajiwa kutokana na idadi kubwa ya wagombea waliojitokeza kuwania nafasi hizo.
Alisema Kamati ya Maadili ya chama hicho ilitakiwa kufanya kikao kimoja kwa ajili ya kupitia na kutoa mapendekezo ya wagombea lakini kutokana na wingi wao kamati hiyo imelazimika kuchukua siku tatu kufanya kazi hiyo.
“Hata hivyo kazi kubwa ni hii inayofanywa na Kamati ya Maadili, Kamati Kuu (CC) na Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) watakuwa na kazi ndogo kwa kuwa watakuwa wanayafanyia kazi mapendekezo yaliyotolewa na kamati hii ya maadili,” alisema Nnauye.
Alitaka idadi ya wagombea waliojitokeza kuwania nafasi hizo mbalimbali ndani ya chama hicho kuwa ni wenyeviti wa mikoa ambako kuna nafasi 31, lakini waliojitokeza kuwania nafasi hizo ni 187 na Katibu Siasa na Uenezi Mkoa nafasi 21 walioomba ni 170.
Wengine ni Makatibu wa Uchumi/Fedha mkoa nafasi 31 walioomba 148, wenyeviti wa wilaya nafasi 161 walioomba 965 na wajumbe wa NEC taifa nafasi 221 walioomba 1,380.
Katika nafasi za wenyeviti wa jumuiya za taifa, kwa upande wa Umoja wa Vijana CCM (UVCCM) nafasi ni moja walioomba 47 wote kutoka Zanzibar, Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) nafasi moja walioomba tisa na Jumuiya ya Wazazi nafasi moja walioomba ni 22.
Kwa upande wa makamu wenyeviti wa jumuiya ndani ya chama hicho, UVCCM nafasi ni moja walioomba ni 27 wote kutoka Tanzania Bara, UWT nafasi moja walioomba watatu na Wazazi nafasi moja walioomba ni 10.
Aidha katika nafasi za wenyeviti wa jumuiya wa mikoa zipo 93 walioomba ni 502 na kwa wajumbe wa Nec nafasi za jumuiya zipo nafasi 30 walioomba ni 279.
“Kazi ni kubwa kinachofanyika ni Kamati hii ya Maadili kupitia jina moja moja la kila mgombea,” alisema Nape.
Alipoulizwa kuwa haoni idadi kubwa ya wagombea iliyojitokeza inaweza kuleta makundi, Nape alijibu kuwa chama hicho kinauzoefu wa miaka 50 kuhusiana na watu wanaojitokeza kuwania nafasi mbalimbali za uongozi.
Kwa siku ya tatu mfululizo, Kamati ya Maadili ya CCM imeendelea kupitia majina ya wagombea mjini Dodoma huku ikieleza kuwa kazi hiyo imekuwa kubwa kutokana na wagombea kuwa wengi.
Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye ameonya kwamba wagombea wanaolumbana nje badala ya kwenye vikao halali vya ndani vya chama hicho , wakitishia patachimbika iwapo Halmashauri Kuu ya Taifa (Nec) ya chama hicho itawaengua, wanaonyesha jinsi walivyo na uwezo mdogo wa kuongoza.
Walioingia katika malumbano ya kisiasa ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta; Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Khamis Mgeja; Mbunge wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono na Mbunge wa Kahama, James Lembeli.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma jana, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, alisema kuwa:
“Unapotaka kuwa kiongozi wa taasisi kubwa moja ya sifa ni uwezo wako wa kuhimili presha, ukiona mtu anapiga kelele barabarani ujue uwezo wake wa kuhimili presha ni mdogo, presha imekuwa kubwa kiasi kwamba hawezi kuhimili inabidi aende kupumua barabarani.”alisema.
Aliongeza kuwa: “Busara itatumika kuamua nani arudi nani asirudi…siasa za leo ni za presha hasa inapofika wakati wa uchaguzi na inapofika siasa za jumuiya. Sasa kama unataka kuiongoza taasisi kubwa kama hiyo lazima uwe na kifua cha kuhimili presha.”
Kuhusu malumbano ya hivi karibuni kati ya Sitta ambaye pia ni Mbunge wa Urambo Mashariki, Nape alisema kuwa: “Hawa wote ni wajumbe wa vikao halali wanasema barabarani sijui labda wamelewa, hawa ni viongozi kama mtu ana agenda yake aje kwenye vikao.”
Nape aliongeza kuwa “Kwa hili nalo wasubiri vikao vitakapofanya maamuzi, wakiona wana maoni hai wanayofursa ya kuja kusema katika vikao, kwa sababu hatutafanyia kazi maoni barabarani."
Kuhusu mgogoro wa kada wa chama hicho, Hussein Bashe na Mbunge wa Nzega, Dk. Hamisi Kingwallah, alisema hilo linashughulikiwa na Kamati ya Maadili ya Chama hicho.
Alisema kama watabainika kuwa na makosa basi kikao hicho kitatoa adhabu ambayo si lazima itangazwe hadharani.
Akizungumzia kuhusiana na kuchelewa kuanza kwa vikao vya Kamati Kuu na Halmashauri Kuu, Nape alisema idadi kubwa ya waliojitokeza kugombea inaonyesha kukubalika kwa chama mbele ya wananchi.
“Vikao vya chini vinachokifanya ni kuweka alama tu kuanzia A hadi E ambayo inaonyesha kuwa haufai kabisa…Tafsiri kwamba vikao vya chini havikufanya kazi yake vizuri si kweli, vikao vya chini vilifanya kazi nzuri sana,”alisema Nape.
Alisema kuna watu ambao watakuwa wametoa malalamiko ni lazima vikao hivyo viangalie kwa kigezo cha mahitaji ya wakati huo yakoje.
Aidha imebainisha kuwa mchujo wa wagombea wa nafasi mbalimbali ndani ya CCM inaweza kuchukua muda mrefu kuliko ilivyotarajiwa kutokana na idadi kubwa ya wagombea waliojitokeza kuwania nafasi hizo.
Alisema Kamati ya Maadili ya chama hicho ilitakiwa kufanya kikao kimoja kwa ajili ya kupitia na kutoa mapendekezo ya wagombea lakini kutokana na wingi wao kamati hiyo imelazimika kuchukua siku tatu kufanya kazi hiyo.
“Hata hivyo kazi kubwa ni hii inayofanywa na Kamati ya Maadili, Kamati Kuu (CC) na Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) watakuwa na kazi ndogo kwa kuwa watakuwa wanayafanyia kazi mapendekezo yaliyotolewa na kamati hii ya maadili,” alisema Nnauye.
Alitaka idadi ya wagombea waliojitokeza kuwania nafasi hizo mbalimbali ndani ya chama hicho kuwa ni wenyeviti wa mikoa ambako kuna nafasi 31, lakini waliojitokeza kuwania nafasi hizo ni 187 na Katibu Siasa na Uenezi Mkoa nafasi 21 walioomba ni 170.
Wengine ni Makatibu wa Uchumi/Fedha mkoa nafasi 31 walioomba 148, wenyeviti wa wilaya nafasi 161 walioomba 965 na wajumbe wa NEC taifa nafasi 221 walioomba 1,380.
Katika nafasi za wenyeviti wa jumuiya za taifa, kwa upande wa Umoja wa Vijana CCM (UVCCM) nafasi ni moja walioomba 47 wote kutoka Zanzibar, Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) nafasi moja walioomba tisa na Jumuiya ya Wazazi nafasi moja walioomba ni 22.
Kwa upande wa makamu wenyeviti wa jumuiya ndani ya chama hicho, UVCCM nafasi ni moja walioomba ni 27 wote kutoka Tanzania Bara, UWT nafasi moja walioomba watatu na Wazazi nafasi moja walioomba ni 10.
Aidha katika nafasi za wenyeviti wa jumuiya wa mikoa zipo 93 walioomba ni 502 na kwa wajumbe wa Nec nafasi za jumuiya zipo nafasi 30 walioomba ni 279.
“Kazi ni kubwa kinachofanyika ni Kamati hii ya Maadili kupitia jina moja moja la kila mgombea,” alisema Nape.
Alipoulizwa kuwa haoni idadi kubwa ya wagombea iliyojitokeza inaweza kuleta makundi, Nape alijibu kuwa chama hicho kinauzoefu wa miaka 50 kuhusiana na watu wanaojitokeza kuwania nafasi mbalimbali za uongozi.
HUU NDIO MTAZAMO WA GIRAFFE HOTEL DAR-ES-SALAAM
MKE WA CHENGE AHOJIWA TAKUKURU
MKE wa Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge (CCM), amehojiwa na Taasisi ya Kupambana na Kudhibiti Rushwa (TAKUKURU) kwa tuhuma za ufisadi.
Wakati mama huyo, Tina Chenge, akinaswa na kuhojiwa na TAKUKURU kwa rushwa, Chenge mwenyewe ambaye kwa muda mrefu amekuwa akitajwa ndani na nje ya chama chake kuhusika na kashfa ya ununuzi wa rada kutoka Kampuni ya BAE-System, alisafishwa na Rais Jakaya Kikwete kwamba hakuna rushwa katika ununuzi wa kifaa hicho.
Habari ambazo Tanzania Daima Jumapili imezipata, zilisema kuwa Tina alihojiwa juzi na TAKUKURU na kisha kuachiwa huru wakati uchunguzi dhidi yake ukiendelea.
Haikuweza kujulikana mara moja endapo amehojiwa kuhusiana na vitendo vya rushwa vinavyoendelea kwenye uchaguzi wa ujumbe wa Halmashauri Kuu (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), nafasi ambayo Chenge anawania au la.
Kukamatwa kwa mke wa kigogo huyo na hatimaye kuhojiwa na TAKUKURU, kulithibitishwa jana na Mkurugenzi wa taasisi hiyo nchini, Dk. Edward Hosea.
Akizungumza na gazeti hili jana, Dk. Hosea alikiri taasisi yake kumhoji mke wa Chenge, lakini hakuwa tayari kusema amehojiwa kwa tuhuma zipi.
“Ni kweli tumemhoji na huu ni mwendelezo wa kuwahoji watu mbalimbali wakiwemo mawaziri, wabunge wanaotuhumiwa kwa rushwa na hakuna atakayebaki bila kuhojiwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria,” alisema Dk. Hosea.
Alipoulizwa endapo mke wa Chenge amehojiwa kwa tuhuma za rushwa ndani ya uchaguzi wa CCM, Dk. Hosea alisema mahojiano hayo hayana uhusiano wowote na uchaguzi wa chama hicho tawala.
Hata hivyo, alisema kuhusu suala la rushwa ndani ya CCM, TAKUKURU imeshatoa maelekezo kwa watendaji wake mikoani na ripoti za taarifa hizo zinafanyiwa kazi.
Hivi karibuni, Rais Kikwete alivunja ukimya kwa kuuambia umma kwamba hakuna rushwa kwenye kashfa ya ununuzi wa rada.
Ingawa Rais Kikwete hakutaja jina, lakini kwa kauli hiyo ni dhahiri kwamba alimsafisha Chenge ambaye kwa muda mrefu amekuwa akitajwa kuhusika na kashfa ya ununuzi wa rada kutoka Kampuni ya BAE-System.
Chenge ambaye kwa sasa ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Fedha na Uchumi, anatajwa kuhusika kutoa ushauri wa kisheria wakati huo akiwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, ushauri ambao unatajwa kuzingatiwa katika hatua za uamuzi.
Mwingine anayehusishwa na kashfa hiyo ni aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu (BoT), Dk. Idriss Rashid.
Pamoja na hao, wanatajwa wafanyabiashara wenye asili ya India, lakini ambao wanaishi/walipata kuishi Tanzania, Tanil Somaiya, ambaye alikuwa akimiliki kampuni ya uwakala wa simu ya Shivacom na Sailesh (Shailesh) Vithlani kuwa watu wa kati wa biashara hiyo.
Akijibu swali kutoka kwa mmoja wa wahariri aliyetaka kujua hatua zilizochukuliwa kwa waliohusika na ununuzi wa rada wakati chenji yake imesharejeshwa, Rais Kikwete alisema Serikali ya Uingereza iliyokuwa ikichunguza kashfa hiyo imebaini kuwa hakukuwa na rushwa katika ununuzi bali kulikuwa na makosa ya uchapaji.
Dk. Hosea, alipata mara mbili kunukuliwa akisema Chenge hakuwa na kesi ya kujibu katika kashfa hiyo ya rada.
chanzo:daima
Wakati mama huyo, Tina Chenge, akinaswa na kuhojiwa na TAKUKURU kwa rushwa, Chenge mwenyewe ambaye kwa muda mrefu amekuwa akitajwa ndani na nje ya chama chake kuhusika na kashfa ya ununuzi wa rada kutoka Kampuni ya BAE-System, alisafishwa na Rais Jakaya Kikwete kwamba hakuna rushwa katika ununuzi wa kifaa hicho.
Habari ambazo Tanzania Daima Jumapili imezipata, zilisema kuwa Tina alihojiwa juzi na TAKUKURU na kisha kuachiwa huru wakati uchunguzi dhidi yake ukiendelea.
Haikuweza kujulikana mara moja endapo amehojiwa kuhusiana na vitendo vya rushwa vinavyoendelea kwenye uchaguzi wa ujumbe wa Halmashauri Kuu (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), nafasi ambayo Chenge anawania au la.
Kukamatwa kwa mke wa kigogo huyo na hatimaye kuhojiwa na TAKUKURU, kulithibitishwa jana na Mkurugenzi wa taasisi hiyo nchini, Dk. Edward Hosea.
Akizungumza na gazeti hili jana, Dk. Hosea alikiri taasisi yake kumhoji mke wa Chenge, lakini hakuwa tayari kusema amehojiwa kwa tuhuma zipi.
“Ni kweli tumemhoji na huu ni mwendelezo wa kuwahoji watu mbalimbali wakiwemo mawaziri, wabunge wanaotuhumiwa kwa rushwa na hakuna atakayebaki bila kuhojiwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria,” alisema Dk. Hosea.
Alipoulizwa endapo mke wa Chenge amehojiwa kwa tuhuma za rushwa ndani ya uchaguzi wa CCM, Dk. Hosea alisema mahojiano hayo hayana uhusiano wowote na uchaguzi wa chama hicho tawala.
Hata hivyo, alisema kuhusu suala la rushwa ndani ya CCM, TAKUKURU imeshatoa maelekezo kwa watendaji wake mikoani na ripoti za taarifa hizo zinafanyiwa kazi.
Hivi karibuni, Rais Kikwete alivunja ukimya kwa kuuambia umma kwamba hakuna rushwa kwenye kashfa ya ununuzi wa rada.
Ingawa Rais Kikwete hakutaja jina, lakini kwa kauli hiyo ni dhahiri kwamba alimsafisha Chenge ambaye kwa muda mrefu amekuwa akitajwa kuhusika na kashfa ya ununuzi wa rada kutoka Kampuni ya BAE-System.
Chenge ambaye kwa sasa ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Fedha na Uchumi, anatajwa kuhusika kutoa ushauri wa kisheria wakati huo akiwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, ushauri ambao unatajwa kuzingatiwa katika hatua za uamuzi.
Mwingine anayehusishwa na kashfa hiyo ni aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu (BoT), Dk. Idriss Rashid.
Pamoja na hao, wanatajwa wafanyabiashara wenye asili ya India, lakini ambao wanaishi/walipata kuishi Tanzania, Tanil Somaiya, ambaye alikuwa akimiliki kampuni ya uwakala wa simu ya Shivacom na Sailesh (Shailesh) Vithlani kuwa watu wa kati wa biashara hiyo.
Akijibu swali kutoka kwa mmoja wa wahariri aliyetaka kujua hatua zilizochukuliwa kwa waliohusika na ununuzi wa rada wakati chenji yake imesharejeshwa, Rais Kikwete alisema Serikali ya Uingereza iliyokuwa ikichunguza kashfa hiyo imebaini kuwa hakukuwa na rushwa katika ununuzi bali kulikuwa na makosa ya uchapaji.
Dk. Hosea, alipata mara mbili kunukuliwa akisema Chenge hakuwa na kesi ya kujibu katika kashfa hiyo ya rada.
TASWIRA YA KIVUKO CHA KIGAMBONI!!!
MASHAUZI CLASSIC WAPATA AJALI DAR!!
GARI la kundi la mipasho la Mashauzi Classic Modern Taarab, alfajiri ya juzi, lilipata ajali baada ya kuzimika ghafla katikati ya barabara na kurudi nyuma kwa kasi na kuingia kwenye mtaro kando ya barabara.
Tukio hilo lilitokea maeneo ya Mtoni Kijichi, wilayani Temeke, jijini Dar es Salaam, wakati gari hilo likiwarejesha nyumbani wasanii wa kundi hilo chini ya Mkurugenzi Mkuu, Isha Mashauzi ‘Jike la Simba’.
Meneja wa Mashauzi Classic, Suma Laga alisema jana kuwa, walikuwa wakitokea Tabata kwenye ukumbi wa Da’ West walipokuwa wakitumbuiza siku hiyo, wakielekea Mtoni Kijichi kumrudisha mpiga gitaa la besi, Amad Mominu.
“Wakati tunapandisha kilima cha kuiacha Mbagala Mission kuingia Kijichi, tukiwa tunakaribia kileleni, gari lilizimika ghafla na kuanza kurudi nyuma kwa kasi, wakati huo dereva akijitahidi kubana breki ambazo nazo zilikataa,” alisema Suma.
Suma alisema kuwa, baada ya jitihada za dereva kushindwa, gari hilo lilikwenda moja kwa moja na kugonga mtaro pembeni mwa barabara na wasanii kadhaa wameumia.
Aidha, alisema wasanii wanne wa kundi hilo, Zubeda Maliki, Asia Thabit (waimbaji), Ibrahim Kamongo (kinanda) na Goodluck Katambwa (mnenguaji), walijeruhiwa na kupelekwa hospitalini Mwananyamala ambako walitibiwa na kuruhusiwa.
chanzo:daima
Tukio hilo lilitokea maeneo ya Mtoni Kijichi, wilayani Temeke, jijini Dar es Salaam, wakati gari hilo likiwarejesha nyumbani wasanii wa kundi hilo chini ya Mkurugenzi Mkuu, Isha Mashauzi ‘Jike la Simba’.
Meneja wa Mashauzi Classic, Suma Laga alisema jana kuwa, walikuwa wakitokea Tabata kwenye ukumbi wa Da’ West walipokuwa wakitumbuiza siku hiyo, wakielekea Mtoni Kijichi kumrudisha mpiga gitaa la besi, Amad Mominu.
“Wakati tunapandisha kilima cha kuiacha Mbagala Mission kuingia Kijichi, tukiwa tunakaribia kileleni, gari lilizimika ghafla na kuanza kurudi nyuma kwa kasi, wakati huo dereva akijitahidi kubana breki ambazo nazo zilikataa,” alisema Suma.
Suma alisema kuwa, baada ya jitihada za dereva kushindwa, gari hilo lilikwenda moja kwa moja na kugonga mtaro pembeni mwa barabara na wasanii kadhaa wameumia.
Aidha, alisema wasanii wanne wa kundi hilo, Zubeda Maliki, Asia Thabit (waimbaji), Ibrahim Kamongo (kinanda) na Goodluck Katambwa (mnenguaji), walijeruhiwa na kupelekwa hospitalini Mwananyamala ambako walitibiwa na kuruhusiwa.
Friday, 21 September 2012
IJUMAA SEXIEST GIRL 2011/2012 JACK WOLPER AREJESHWA
HUKU mtifuano ukiwa mkali kati ya Wema Sepetu na Agnes Masogange, wadau wengi wameomba msanii Jacqueline Wolper arejeshwe kwenye shindano hilo ili mshindi apatikane kutokea tatu bora.
Baadhi ya wasomaji wanaofuatilia kwa karibu shindano hili walisema, mshindi kati ya Wema na Agnes anaweza kupatikana lakini itanoga zaidi Wolper akarudi ili apatikane mshindi namba moja, mbili na tatu.
Kufuatia ombi hilo, sisi hatuna hiyana na tumeamua kumrejesha msanii hyo ambaye naye anaonekana kukubalika kwa wengi, kwani hata kutolewa kwake awali kulikuwa kwa mbinde sana.
Kufuatia hatua hiyo, sasa wasomaji watatakiwa kumpigia kura mrembo anayestahili kuibuka mshindi kati ya washiriki hao watatu. Ili kupiga kura, andika jina la mrembo anayestahili kushinda kisha litume kwenda namba 0786799120.
chanzo:http://www.globalpublishers.info
Baadhi ya wasomaji wanaofuatilia kwa karibu shindano hili walisema, mshindi kati ya Wema na Agnes anaweza kupatikana lakini itanoga zaidi Wolper akarudi ili apatikane mshindi namba moja, mbili na tatu.
Kufuatia ombi hilo, sisi hatuna hiyana na tumeamua kumrejesha msanii hyo ambaye naye anaonekana kukubalika kwa wengi, kwani hata kutolewa kwake awali kulikuwa kwa mbinde sana.
Kufuatia hatua hiyo, sasa wasomaji watatakiwa kumpigia kura mrembo anayestahili kuibuka mshindi kati ya washiriki hao watatu. Ili kupiga kura, andika jina la mrembo anayestahili kushinda kisha litume kwenda namba 0786799120.
chanzo:http://www.globalpublishers.info
JK:SIJAMUUZIA BUSH KIGAMBONI!!!
Rais Jakaya Kikwete, jana alizindua rasmi ujenzi wa daraja la Kigamboni utakaogharimu Sh. bilioni 214.6 na kusema madai yaliyotolewa dhidi yake kwamba, amemuuzia kinyemela Rais mstaafu wa Marekani, George Bush, eneo la Kigamboni, ni uwongo uliopikwa.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Dk. Ramadhan Dau, daraja hilo litakalokuwa na urefu wa mita 680, litaunganisha maeneo ya Kurasini na Kigamboni na litakuwa na barabara sita; tatu zikiwa ni za kwenda na tatu kurudi na pia litakuwa na nafasi kwa ajili ya watembea kwa miguu.
Uzinduzi wa daraja hilo ulihudhuriwa na baadhi ya mawaziri, Balozi wa Misri nchini, Hosam Mohram, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Saidi Meck Sadiki, wakuu wa wilaya, mameya wa halmashauri za manispaa, jiji, wabunge na madiwani wa mkoa wa huo, makatibu wakuu na wataalam wa wizara, viongozi wa dini, vyama vya siasa na baadhi ya wakazi wa Jiji.
“Kuna uwongo mwingi uliwahi kusemwa kwamba, eti Kigamboni nimemuuzia George Bush. George Bush anatafuta nini huku? Wale ni matajiri wa mafuta. Sasa Kigamboni anakuja kufanya nini? Kuna watu wana viwanda vya kupika uwongo,” alisema Rais Kikwete.
Alisema kinyume cha madai hayo ya uwongo, mpango wa serikali ni kuifanya Kigamboni kuwa mji mpya na wa aina yake.
Kutokana na hilo, amewataka wakazi wa Kigamboni watakaohamishwa kupisha ujenzi wa mji huo juu ya stahiki zao, akisema wote watalipwa na kwamba hakuna atakayedhulumiwa, kwa kuwa serikali inajali haki za wananchi.
Rais Kikwete alisema Dar es Salaam ilivyo hivi sasa, hakuna kitu cha kuvutia kinachowafanya watu waende kuona au kukaa.
Badala yake, alisema hata watalii wamekuwa wakilitumia jiji hilo kama njia tu ya kupita kwenda katika miji mingine, kama vile Zanzibar, ili kuburudika na vivutio visiwani humo.
Kutokana na hali hiyo, alisema serikali imeanza kuzungumza na baadhi ya mashirika makubwa yenye vitu vya kuvutia, ambavyo alisema vitasaidia mji wa Kigamboni kukaa watu 450,000.
Alisema kwa sasa mji huo una wakazi wanaokadiriwa kuwa 45,000.
Alisema pamoja na mipango mizuri ya serikali ya kuliboresha Jiji la Dar es Salaam, kuna baadhi ya watu wasiopenda maendeleo ya nchi.
Rais Kikwete alisema watu hao inawauma sana kuona hatua iliyofikiwa na serikali kujenga daraja hilo na kuwataka waweke mbele maslahi ya nchi.
Aliungana na Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli, kuusifu uongozi wa NSSF chini ya Mkurugenzi Mkuu wake, Dk. Dau, kwa maamuzi mazuri ya kutumia asilimia 60 ya fedha zake (NSSF) kugharimia ujenzi wa daraja hilo.
Hata hivyo, Waziri Magufuli alisema pamoja na maamuzi na kazi nzuri iliyofanywa na NSSF, hajaona serikali ikimpa Dk. Dau nishani ya utumishi uliotukuka, badala yake ni wanajeshi tu ndiyo hupewa tuzo hiyo wanapofanya vizuri.
Waziri Magufuli alisema mara baada ya kukamilika, ni watembea kwa miguu na baiskeli tu ndiyo ambao hawatalipia matumizi ya daraja hilo, lakini magari yatalipa. Malipo hayo ni kwa ajili ya kugharimia uendeshaji wa daraja.
Hata hivyo, alisema watembea kwa miguu watatakiwa kupita na kwamba wale watakaogeuza daraja hilo kuwa sehemu ya kukaa kama inavyofanyika katika daraja la Manzese, watalipa.
Alisema fedha za kuwalipa fidia wamiliki ambao nyumba zao zitafuatwa na barabara za mradi wa ujenzi wa daraja hilo, zimekwishatengwa.
Hivyo, amewataka wakazi wa Kigamboni kutoanza kujenga kwani uthamini umekwishafanyika.
Alisema kila mtu atalipwa kulingana na thamani ya ardhi anayomiliki.
Hata hivyo, alisema watakaojenga sasa zinakopita barabara za mradi huo, wajiandae kuondoka bila kulipwa fidia.
Alisema mradi wa daraja hilo unatarajiwa kukamilika ama mwishoni mwa mwaka 2014 au mwanzoni mwa mwaka 2015.
Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka, alisema mradi huo unatarajia kutengeneza ajira 3,000 zitakazohusu vijana na wataalam wa ngazi mbalimbali.
Kutokana na hilo, aliwataka vijana kuchangamkia ajira hizo ikiwa ni pamoja na kuwa waaminifu wakati ujenzi wa daraja unaendelea.
Awali, Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Dk. Dau alisema wamekubaliana na serikali kwamba asilimia 60 zigharimiwe na NSSF kwa ujenzi wa daraja hilo na asilimia 40 zilizobaki zigharimiwe na serikali kulipa fidia watu watakaohamishwa kupisha mradi huo.
Alisema kwa mujibu wa mkataba kati yao na mkandarasi, ujenzi wa daraja hilo utakamilika ndani ya miaka mitatu, lakini akasema mkandarasi ameahidi kuwa atajitahidi kukamilisha ndani ya miaka miwili na nusu kuanzia sasa.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads), Patrick Mfugale, pamoja na mambo mengine, alisema daraja hilo litasaidia kumaliza tatizo la usafiri hasa kwa wakazi wa Kigamboni.
Alisema kwa sasa wakazi hao hulazimika kutumia kivuko na mitumbwi au njia ya mzunguko yenye urefu wa kilomita 52 kwenda na kurudi Kigamboni.
chanzo:Nipashe
Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Dk. Ramadhan Dau, daraja hilo litakalokuwa na urefu wa mita 680, litaunganisha maeneo ya Kurasini na Kigamboni na litakuwa na barabara sita; tatu zikiwa ni za kwenda na tatu kurudi na pia litakuwa na nafasi kwa ajili ya watembea kwa miguu.
Uzinduzi wa daraja hilo ulihudhuriwa na baadhi ya mawaziri, Balozi wa Misri nchini, Hosam Mohram, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Saidi Meck Sadiki, wakuu wa wilaya, mameya wa halmashauri za manispaa, jiji, wabunge na madiwani wa mkoa wa huo, makatibu wakuu na wataalam wa wizara, viongozi wa dini, vyama vya siasa na baadhi ya wakazi wa Jiji.
“Kuna uwongo mwingi uliwahi kusemwa kwamba, eti Kigamboni nimemuuzia George Bush. George Bush anatafuta nini huku? Wale ni matajiri wa mafuta. Sasa Kigamboni anakuja kufanya nini? Kuna watu wana viwanda vya kupika uwongo,” alisema Rais Kikwete.
Alisema kinyume cha madai hayo ya uwongo, mpango wa serikali ni kuifanya Kigamboni kuwa mji mpya na wa aina yake.
Kutokana na hilo, amewataka wakazi wa Kigamboni watakaohamishwa kupisha ujenzi wa mji huo juu ya stahiki zao, akisema wote watalipwa na kwamba hakuna atakayedhulumiwa, kwa kuwa serikali inajali haki za wananchi.
Rais Kikwete alisema Dar es Salaam ilivyo hivi sasa, hakuna kitu cha kuvutia kinachowafanya watu waende kuona au kukaa.
Badala yake, alisema hata watalii wamekuwa wakilitumia jiji hilo kama njia tu ya kupita kwenda katika miji mingine, kama vile Zanzibar, ili kuburudika na vivutio visiwani humo.
Kutokana na hali hiyo, alisema serikali imeanza kuzungumza na baadhi ya mashirika makubwa yenye vitu vya kuvutia, ambavyo alisema vitasaidia mji wa Kigamboni kukaa watu 450,000.
Alisema kwa sasa mji huo una wakazi wanaokadiriwa kuwa 45,000.
Alisema pamoja na mipango mizuri ya serikali ya kuliboresha Jiji la Dar es Salaam, kuna baadhi ya watu wasiopenda maendeleo ya nchi.
Rais Kikwete alisema watu hao inawauma sana kuona hatua iliyofikiwa na serikali kujenga daraja hilo na kuwataka waweke mbele maslahi ya nchi.
Aliungana na Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli, kuusifu uongozi wa NSSF chini ya Mkurugenzi Mkuu wake, Dk. Dau, kwa maamuzi mazuri ya kutumia asilimia 60 ya fedha zake (NSSF) kugharimia ujenzi wa daraja hilo.
Hata hivyo, Waziri Magufuli alisema pamoja na maamuzi na kazi nzuri iliyofanywa na NSSF, hajaona serikali ikimpa Dk. Dau nishani ya utumishi uliotukuka, badala yake ni wanajeshi tu ndiyo hupewa tuzo hiyo wanapofanya vizuri.
Waziri Magufuli alisema mara baada ya kukamilika, ni watembea kwa miguu na baiskeli tu ndiyo ambao hawatalipia matumizi ya daraja hilo, lakini magari yatalipa. Malipo hayo ni kwa ajili ya kugharimia uendeshaji wa daraja.
Hata hivyo, alisema watembea kwa miguu watatakiwa kupita na kwamba wale watakaogeuza daraja hilo kuwa sehemu ya kukaa kama inavyofanyika katika daraja la Manzese, watalipa.
Alisema fedha za kuwalipa fidia wamiliki ambao nyumba zao zitafuatwa na barabara za mradi wa ujenzi wa daraja hilo, zimekwishatengwa.
Hivyo, amewataka wakazi wa Kigamboni kutoanza kujenga kwani uthamini umekwishafanyika.
Alisema kila mtu atalipwa kulingana na thamani ya ardhi anayomiliki.
Hata hivyo, alisema watakaojenga sasa zinakopita barabara za mradi huo, wajiandae kuondoka bila kulipwa fidia.
Alisema mradi wa daraja hilo unatarajiwa kukamilika ama mwishoni mwa mwaka 2014 au mwanzoni mwa mwaka 2015.
Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka, alisema mradi huo unatarajia kutengeneza ajira 3,000 zitakazohusu vijana na wataalam wa ngazi mbalimbali.
Kutokana na hilo, aliwataka vijana kuchangamkia ajira hizo ikiwa ni pamoja na kuwa waaminifu wakati ujenzi wa daraja unaendelea.
Awali, Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Dk. Dau alisema wamekubaliana na serikali kwamba asilimia 60 zigharimiwe na NSSF kwa ujenzi wa daraja hilo na asilimia 40 zilizobaki zigharimiwe na serikali kulipa fidia watu watakaohamishwa kupisha mradi huo.
Alisema kwa mujibu wa mkataba kati yao na mkandarasi, ujenzi wa daraja hilo utakamilika ndani ya miaka mitatu, lakini akasema mkandarasi ameahidi kuwa atajitahidi kukamilisha ndani ya miaka miwili na nusu kuanzia sasa.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads), Patrick Mfugale, pamoja na mambo mengine, alisema daraja hilo litasaidia kumaliza tatizo la usafiri hasa kwa wakazi wa Kigamboni.
Alisema kwa sasa wakazi hao hulazimika kutumia kivuko na mitumbwi au njia ya mzunguko yenye urefu wa kilomita 52 kwenda na kurudi Kigamboni.
chanzo:Nipashe
SHAMBULIZI LA KUJITOA MHANGA SOMALIA!!!!
Shambulizi
watu wakiukimbia mji wa Kismayo
Shambulizi hilo limetokea karibu na mkahawa mmoja mjini Mogadishu. Walioshuhudia tukio hilo wamesema kuwa watu kadhaa wamejeruhiwa
watu wakiukimbia mji wa Kismayo
Shambulizi hilo limetokea karibu na mkahawa mmoja mjini Mogadishu. Walioshuhudia tukio hilo wamesema kuwa watu kadhaa wamejeruhiwa
Hadi sasa hakuna kundi lolote limeelezea kufanya shambulizi hilo.
Shambulizi la leo linatokea wakati majeshi ya Somalia yanakaribia kuuzingira mji wa Kismayo ambayo ni ngome kubwa na ya mwisho ya Al Shabaab.
Shirika la umoja wa mataifa la kuwahudumia wakimbizi UNHCR limeelezea kuongezeka kwa idadi ya watu wanaotoroka mji wa Kismayo ambao sasa wanafikia zaidi ya elfu moja kila siku.
'Mlipuko wa pili'
Mwandishi wa BBC mjini Mogadishu, Ibrahim Aden, ameelezea kuona zaidi ya miili sita katika mkahawa huo ambao uko mkabala na ukumbi wa michezo ya kuigiza baada ya shambulizi
Ameongeza kuwa eneo hilo ni maarufu kwa wafanyakazi wa umma pamoja na waandishi wa habari.Waandishi wawili wanasemekana kuwa miongini mwa wale waliouawa.
Baadhi ya waliojeruhiwa walipelekwa hospitalini wakiwa na majereha mabaya.
Taarifa ambazo hazijathibitishwa zinasema kuwa mlipuko wa pili vile vile ulitokea karibu na mkahawa wakati watu walipokusanyika kushuhudia kilichotokea.
chanzo:bbc
HAPPY BIRTHDAY MY FRIEND JOHN KIANDIKA!!!
It has been said that real friends
Are very hard to find.
The ones that stay when times are tough
A real friend - the lasting kind.
As I travel through this life,
I know one thing is true.
I will never find a better friend
Than I have found in YOU!
Happy Bday to a special friend!
Thursday, 20 September 2012
BABY MADAHA AACHA MATITI NJE JUKWAANI!!!
STAA ‘seksi’ wa filamu na muziki wa Bongo Fleva, Baby Joseph Madaha amejikuta akiumbuka mbele ya mashabiki wake baada ya matiti a.k.a nido zake kuchomoza na kuonekana hadharani akiwa jukwaani na kusababisha midume yenye ukame kumzengea.
Tukio hilo la aibu isiyo na kipimo lilishuhudiwa na mwanahabari wetu usiku wa kuamkia Septemba 17, mwaka huu kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro ambako kulikuwa na tamasha kubwa la Serengeti Fiesta 2012.
Baby Madaha alifanya kioja hicho baada ya kutakiwa kupanda jukwaani kuimba na Juma Kassim ‘Nature’ ambaye wameshirikiana katika moja ya nyimbo zake.
Bila hiyana, Baby alipanda stejini kwa mbwembwe na kujikuta akimwaga ‘lazi’ kwa kuonesha matiti au chakula ya mtoto hadharani na kusababisha umati uliokuwa umefurika uwanjani hapo kulipuka kwa shangwe huku mwanadada huyo akiendeleza libeneke la shoo kali.
Baada ya kushuka jukwaani ndipo bidada huyo alipovamiwa na wanaume wakware ambao wakambonyeza ‘Kizenji’ hadi alipookolewa na mabaunsa na kupelekwa nyuma ya jukwaa
chanzo:http://www.globalpublishers.info
UNYAMA WA POLISI: MIAKA MITATU FAMILIA ZAOMBOLEZA!!
Mzazi wa Shedrack Motika(Olais Motika)
Miaka mitatu sasa bado familia za vijana waliouawa kikatili na askari polisi mkoani Arusha zinaomboleza huku zikisubiri haki itendeke kwa waliohusika kukatisha maisha ya watoto wao kuchukuliwa hatua za kisheria.
Majonzi hayo yakiwa yamegubika familia hizo, kesi dhidi ya askari polisi wanaotuhumiwa kuwaua vijana hao haijapelekwa mahakamani miaka mitatu tangu tukio hilo litokee na hakuna dalili yoyote kwamba hatua zitachukuliwa.
Tukio la vifo vya Ewald Mtui na Shedrack Motika wanaodaiwa kukatishwa maisha yao na risasi za polisi katika mazingira ya utatanishi wakidaiwa kuwa ni majambazi waliokuwa wanataka kupora kwenye kituo cha mafuta eneo la Kijenge, linaendelea kutesa mioyo ya wapenda haki, ndugu na jamaa wa vijana hao.
Wakizungumza na NIPASHE kwa nyakati tofauti, wana familia hizo wamedai kuwa serikali imeshindwa hata kuwapeleka mahakamani askari wanaotuhumiwa kufanya mauaji hayo yaliyotikisa Jiji la Arusha na vitongoji vyake.
Mzazi wa marehemu, Motika, Olais Motika alisema kuwa wamelifuatilia suala hilo katika ofisi ya Mwanasheria wa Serikali Kanda ya Arusha, lakini hakuna majibu ya uhakika waliowahi kupewa.
Mzee Motika anasema kwamba wamekuwa wakiambiwa kuwa faili limepelekwa katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP).
“Hata huko kwa DPP tumefuatilia lakini tumekuwa tunazungushwa, tumechoka na tunaomba watetea haki za binadamu waingilie kati mauaji ya watoto wetu waliouawa bila hatia,” alisema Mzee Motika wakati akizungumza na NIPASHE.
Motika alieleza kuwa inaonekana kwa nyakati hizi kwa mtu wa kawaida kupata haki ni jambo gumu sana kutokana na timu iliyoundwa na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Isdore Shirima, kubaini na kuthibitisha kuwa vijana hao hawakuwa majambazi.
Alifafanua kuwa timu hiyo ilibaini pia kwamba halikuwepo hata tukio la ujambazi lililotokea katika kituo cha mafuta kinachomilikiwa na mfanyabiashara maarufu mwenye asilia ya Kiasia.
“Hatujamsahau kijana wetu, alikuwa sehemu ya maisha yetu, alikuwa na ndoto za maisha marefu, lakini yakakatizwa kinyama na polisi bila huruma,” alisema Mzee Motika na kuwa kibaya zaidi ni kuona jambo hilo likizimwa na wataalamu ambao yeye aliwaamini kuwa ni walinzi wa watu.
Miaka mitatu sasa bado familia za vijana waliouawa kikatili na askari polisi mkoani Arusha zinaomboleza huku zikisubiri haki itendeke kwa waliohusika kukatisha maisha ya watoto wao kuchukuliwa hatua za kisheria.
Majonzi hayo yakiwa yamegubika familia hizo, kesi dhidi ya askari polisi wanaotuhumiwa kuwaua vijana hao haijapelekwa mahakamani miaka mitatu tangu tukio hilo litokee na hakuna dalili yoyote kwamba hatua zitachukuliwa.
Tukio la vifo vya Ewald Mtui na Shedrack Motika wanaodaiwa kukatishwa maisha yao na risasi za polisi katika mazingira ya utatanishi wakidaiwa kuwa ni majambazi waliokuwa wanataka kupora kwenye kituo cha mafuta eneo la Kijenge, linaendelea kutesa mioyo ya wapenda haki, ndugu na jamaa wa vijana hao.
Wakizungumza na NIPASHE kwa nyakati tofauti, wana familia hizo wamedai kuwa serikali imeshindwa hata kuwapeleka mahakamani askari wanaotuhumiwa kufanya mauaji hayo yaliyotikisa Jiji la Arusha na vitongoji vyake.
Mzazi wa marehemu, Motika, Olais Motika alisema kuwa wamelifuatilia suala hilo katika ofisi ya Mwanasheria wa Serikali Kanda ya Arusha, lakini hakuna majibu ya uhakika waliowahi kupewa.
Mzee Motika anasema kwamba wamekuwa wakiambiwa kuwa faili limepelekwa katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP).
“Hata huko kwa DPP tumefuatilia lakini tumekuwa tunazungushwa, tumechoka na tunaomba watetea haki za binadamu waingilie kati mauaji ya watoto wetu waliouawa bila hatia,” alisema Mzee Motika wakati akizungumza na NIPASHE.
Motika alieleza kuwa inaonekana kwa nyakati hizi kwa mtu wa kawaida kupata haki ni jambo gumu sana kutokana na timu iliyoundwa na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Isdore Shirima, kubaini na kuthibitisha kuwa vijana hao hawakuwa majambazi.
Alifafanua kuwa timu hiyo ilibaini pia kwamba halikuwepo hata tukio la ujambazi lililotokea katika kituo cha mafuta kinachomilikiwa na mfanyabiashara maarufu mwenye asilia ya Kiasia.
“Hatujamsahau kijana wetu, alikuwa sehemu ya maisha yetu, alikuwa na ndoto za maisha marefu, lakini yakakatizwa kinyama na polisi bila huruma,” alisema Mzee Motika na kuwa kibaya zaidi ni kuona jambo hilo likizimwa na wataalamu ambao yeye aliwaamini kuwa ni walinzi wa watu.
Subscribe to:
Posts (Atom)
.jpg)

.jpg)






.jpg)









.jpg)



.jpg)
.jpg)




.jpg)