Friday, 30 November 2012

Simu kukebehi wafu siyo uungwana


MZAHA mzaha umekuwa ukiongezeka miongoni mwa jamii kila linapotokea tatizo, liwe kama ni janga au hata furaha baadhi ya watu hutumia mzaha huo.
Baadhi ya watu hao wamekuwa wakikosa maadili na kupoteza mshikamano katika matukio mbalimbali mbayo yanahitaji kusaidiana na kuwafariji wahusika.
Kikubwa anbacho nitakizungumzia leo ni kuhusu matumizi mabaya mtandao hasa simu; kwa kweli ni aibu kwa taifa ambalo linaaminika kuwa la watu wenye umoja na mshikamano.
Matumizi hayo mabaya ya simu yamekuwa yakitumika katika kudhihaki matukio kama vile misiba ikiwemo ile ya watu maarufu nchini.
Ustaarabu wa Watanzania umekuwa ukishuka kutokana na kuyachukulia matukio hayo ya vifo kama mambo ya kufurahisha katika jamii.
Kifo cha Msanii Hussein Ramadhan Mkieti ‘Sharo Millionea’ chahusika: kuna baadhi ya watu ambao hawana utu wa kibinadamu; wamekuwa wakikichukulia kwa mzaha kwa kutumiana ujumbe ambao hauna maana yoyote sanasana kuwaongezea huzuni wafiwa.
Ukiangalia ujumbe unaotumwa na watumiaji simu hao hata haueleweki una lengo gani na ni kwa faida ya nani haswa.
Ujumbe wa kumkebehi mtu ambaye amekwishafariki kwa kweli unasikitisha sana; hivi ni vitendo ambavyo havistahili kuungwa mkono na kila mmoja ambaye anajua maana halisi ya kufiwa.
Kwa mfano ukiangalia ujumbe unaosema, “Sharo: Mnanizika wapi meeen? Majuto: Muheza Tanga; Sharo : Mmebugi meen nataka mnizike alipozikwa Michael Jackson meeen! Majuto: We unazikwa Lusanga kijijini. Sharo: Ooh mamaaaa!
“Kanumba: Kwani vipi mbona una mawazo na tayari umeishafika kwenye makazi ya milele! Sharo: Haya mawazo nawaza jee mazishi yatafanana kama na ya kwako yalivyokuwa meeen?
“Kanumba: Karibu sana Sharomilionea huku ndiko Airtel ulikokuwa unataka kuhamia, bado mzee wako Majuto!”
Huo ni mmoja wa ujumbe ambao umekuwa ukisambazwa na watu ambao unaweza kuwaita kuwa ni watu wenye mtindio wa ubongo na waliochanganyikiwa na maisha huku wakikosa kazi za kufanya.
Ujumbe kama huo uko wa aina nyingi na waandaaji wa ujumbe kama huo wamekuwa na kazi kubwa ya kuuandaa kwa malengo ya kufurahisha nafsi zao wakati wafiwa wakiteseka kwa uchungu wa kumpoteza ndugu yao.
Ukiachilia mbali hao wanaotuma ujumbe pia wapo wanaosambaza baadhi ya picha za msanii huyo ambazo kimaadili na utamaduni wa Kitanzania hazingepaswa kusambazwa kwenye mitandao ya kijamii.
Kwa kweli huu ni udhalilishaji pia haipendezi, sijui inatufundisha nini kama siyo kuudhalilisha mwili wa marehenu ambaye hastahili kufanyiwa hivyo.
Sitaki kuamini sana kama kweli kampuni za simu zina vitengo vinavyoaandaa ujumbe kama huo na kama kweli vitengo hivyo vipo na vinatumika kwa staili hiyo basi naamini ubunifu wao utakuwa umefikia kikomo na hawawezi kuendelea.
Itakuwa ni kampuni gani hizo zisizojali matatizo ya wateja wake, bali kujali fedha hata kama wengine wanaathirika na ujumbe kama huo?
Safu hii inawatahadharisha watu wanaoandaa ujumbe kama huo kutambua kuwa iko siku nao watakufa na nafsi zao zitasutwa mbele ya Mwenyezi Mungu.
Kikubwa Watanzania tujaribu kujiepusha na tabia ambazo haziwezi kutoa elimu ya aina yoyote katika jamii, ambayo ina mahitaji mengi katika kujiendeleza.
Mwisho wale wote waliotumiwa ujumbe wa aina yoyote na kuusambaza kwa wengine wanapaswa kutambua kuwa haukuisaidia familia ya marehemu bali wamechangia mitandao ya simu kwa ajili ya kuendeleza maslahi yao, na wao ni bure kabisa.
Hebu muulize anayekutumia ujumbe kama huo amelipwa shilingi ngapi na huo mtandao uliotumika kutuma ujumbe huo. Pia hii mitandao kama inajihusisha au haihusiki basi itoe tamko kuufahamisha umma kuwa inakuwaje vitu kama hivyo vinapitishwa kimzahamzaha katika mitandao yao huku wakiwa wanapepesa pesa macho tu?
chanzo: daima

‘Dada’ aiba mtoto


MSAIDIZI wa ndani, Doyi Yusuph (13), mwenyeji wa mkoa wa Kigoma, anasadikiwa kuiba mtoto wa kike, Yasinta Joel (5), katika nyumba aliyokuwa akifanya kazi wilayani Bukombe, Geita, na kisha kutoweka naye kusikojulikana.
Akizungumza na Tanzania Daima juzi, bibi wa mtoto huyo, Perepatua Alphonce, alisema dada huyo amefanya wizi huo huku akiacha sanduku lake la nguo, jambo ambalo liliwahadaa kwa kutogundua haraka kitendo hicho.
Perepetua maarufu kwa jina na Bibi Mgaya, alisema mjukuu wake huyo alikuwa akisoma chekechea kwa Mwalimu Kapesa na alikuwa akiishi na babu yake, Edward Mgasa.
Alisema dada huyo ambaye alikuwa na wiki moja tangu aanze kazi katika familia ya Mzee Mgasa, alimuiba mtoto huyo Novemba 23, mwaka huu, majira ya saa tatu asubuhi. Wakati akiondoka naye mtoto huyo alikuwa amevaa blauzi ya maua yenye mchanganyiko wa rangi nyekundu na zambarau na sketi ya Jeans rangi ya bluu.
“Niliishaachana na Mzee Mgasa ambaye alioa mke mwingine na walikuwa wakishirikiana kumlea mjukuu wetu. Siku ya tukio mzazi mwenzangu alikuwa kwenye machimbo madogo ya Ng’anzo kwenda kutafuta riziki,” alisema Perepetua.
Alisema amesharipoti suala hilo katika kituo cha polisi cha wilayani Bukombe na kufunguliwa jalada namba USH/IR/177/2012 na kuwaomba raia wema wanaomuona mtoto huyo kutoa taarifa katika kituo chochote cha polisi au kuwasiliana naye kwa simu namba  0755 910 377.
chanzo:daima

Video ya mgomo wa matatu(daladala) nchini kenya

Mmiliki gari lililomuua Sharo Milionea


MMILIKI wa gari ambalo lilikuwa likiendeshwa na msanii maarufu nchini, Hussein Ramadhan ‘Sharo Milionea’ na kupata nalo ajali iliyosababisha kifo chake huko Muheza, Tanga, Mohammed Ismaili maarufu kwa jina la Mudi Suma, ameibuka na kueleza uhusiano wake na marehemu, huku akisema amekubali hasara.

Akizungumza kwa simu kutoka Muheza jana Suma alisema hana mpango wa kudai fidia au kupeleka malalamiko yoyote kwa ndugu wa marehemu kwa kuwa; “Kilichotokea ni kazi ya Mungu.” “Siwezi kudai hata kidogo hivyo ni vitu vya kupita tu. Marehemu alikuwa ni zaidi ya ndugu yangu, gari ni kitu kidogo sana katika uhusiano tuliokuwa nao,” alisema Suma na kuongeza kwamba hata Marehemu Sharo Milionea naye alikuwa amemwachia mali zake kadhaa ikiwamo gari.

“Siyo gari tu alilokuwa ameniachia. Kuna mikataba yake ya kazi, Bajaji yake na funguo za chumbani kwake. Nasubiri kukabidhi vitu hivyo baada ya kukaa na ndugu zake. Vitu viko kwenye mikono salama,” alisema.

Kuhusu gari lake lililopata ajali, Suma alisema lilikuwa na bima ndogo, lakini anapanga kwenda TRA atakaporejea Dar es Salaam kufuatilia baadhi ya mambo.
“Kabla ya kuondoka bima ile kubwa ilikuwa imekwisha kwa hiyo nikaamua kuikatia bima ndogo. Nitakapofika kesho (leo) Dar es Salaam, nategemea kwenda ofisi za bima kuzungumza nao,” alisema Suma.

Alipoulizwa kama kuna mtu mwingine atakayeathirika kutokana na gari hilo kuharibika katika ajali mbali na yeye, alijibu: “Hakuna tofauti na mimi mwenyewe na familia yangu.”

Kabla ya ajali
Suma alieleza kuwa kabla ya kuanza safiri yake, Sharo Milionea alifika nyumbani kwake mchana na kumweleza kuwa afya yake haikuwa nzuri.

“Kabla ya kuondoka aliniambia kuwa hajielewi elewi na kifua kilikuwa kinambana. Nikamshauri asiondoke peke yake, atafute mtu wa kuondoka naye ambaye atamsaidia kuendesha gari njiani,” alisema Suma na kuongeza:

“Tulianza kuwapigia simu jamaa zetu wanne wa kusafiri naye lakini kila tuliyemwambia hakuwa tayari. Ilikuwa ni changamoto mpaka ilipofika saa 10:45 hivi jioni, akaamua kuondoka peke yake. Wakati anatoa gari getini kwangu, nikamwambia, basi jaribu kuwa mwangalifu sana, maana alikuwa kweli anasumbuliwa na kifua. Tukakubaliana kwamba atakaporudi aende hospitali kucheki afya yake.”

Kuhusu uhusiano wake na marehemu, Suma alisema: “Mimi ni mfanyabiashara na yeye alikuwa msanii, lakini ilitokea tukawa marafiki sana mpaka ikafikia wakati nikaona kuwa ni ndugu yangu. Nilimwamini nikamtambua kama sehemu ya familia.”

Alisema marehemu alikuwa akitumia gari hilo kila alipolihitaji na safari ya kwenda nalo Tanga kwa wazazi wake ilikuwa ni ya tatu.“Siyo mara ya kwanza kuitumia gari lile, nilikuwa nimemwamini sana. Safari ya kwanza alichukua na kusafiri nalo mwenyewe, halafu safari ya pili ikafuata na hii ilikuwa safari ya tatu,” alisema Suma.

Eneo la ajali wakimbia makazi

Mtaa wa Tegeta ulifungwa kwa zaidi ya saa moja kufuatia vurugu.

Wananchi Geita washauri mafisadi kunyongwa hadi kufa


WANANCHI wa Wilaya ya Geita mkoani Geita wamesema ili kurudisha ari ya viongozi kutumikia umma, wale viongozi watakaokumbwa na kashfa za rushwa ama ufisadi wapewe adhabu kali ikiwa ni pamoja na kunyongwa hadi kufa.

Wakitoa maoni yao kwa ajili ya uundwaji wa Katiba Mpya, baadhi ya wakazi hao kwa nyakati tofauti walisema kwamba tatizo la rushwa na ufisadi limekuwa ni jambo la kawaida kiasi cha kuathiri maendeleo ya nchi na hivyo kuitaka Katiba Mpya kubainisha adhabu ya wala rushwa kuwa ni kunyongwa hadi kufa.

Akitoa maoni yake Elisha Ngeleja alieleza kwamba ili kukomesha rushwa nchini, ipo haja ya Katiba ijayo kubainisha kuwa adhabu ya wala rushwa wote watoaji na wapokeaji pale wanapopatikana na hatia, iwe ni kunyongwa.

“Hatua zinazochukuliwa sasa hazijasaidia tatizo linazidi kukua kila siku, rushwa inaongezeka, ili kukomesha katiba inapaswa kutamka bayana kwamba kila anayepatikana na hatia ya kula rushwa anyongwe hadi kufa,” alieleza.

Sylvester Mwanole yeye alipendekeza katiba ijayo inapaswa kubainisha wazi kuwa wanaohujumu mali za umma wafungwe kifungo cha maisha pale wanapopatikana kuwa na hatia.

Alisema tatizo la kuhujumu mali za umma linazidi kuongezeka kila uchao hii ni kutokana na kutokuwa na adhabu kali kwa wanaohujumu na hivyo kubainisha wafungwe kifungo cha maisha.

Naye Mary Mrungu akitoa maoni yake alipendekeza katika Katiba Mpya ufisadi ubainishwe kama kosa kubwa sawa na kosa la kuuwa na adhabu yake iwe kali kwani itasaidia kuwafaanya viongozi waliopewa dhama ya kuongoza nchi kuogopa.
chanzo:mwananchi

Thursday, 29 November 2012

VIDEO Sharo Milionea-Baada ya Mwili wake kuwasiri Nyumbani kwao Tanga-Muheza

ITV ilivyolipoti mazishi ya Sharo Milionea kijijini kwao Lusanga..

7 kunyongwa Misri kwa kutengeza filamu

Hasira dhidi ya filamu hiyo iliyokuwa inamkejeli Mtume Mohammed, ilisababisha maandamano dhidi ya Marekani kiasi cha kuteketezwa ubalozi wake nchini Libya.

Washukiwa hao saba walihukumiwa wakiwa hawapo mahakamani.
Hukumu hizo ziliidhinishwa na Mufti mkuu nchini Misri ambaye pia ni msomi wa dini ya kiisilamu.
Mwandishi wa BBC anasema kuwa ni nadra kwa Mufti kupinga hukumu kama hizi.
Filamu hiyo iliyokuwa ya hali ya chini mno, ilitengezwa mjini Carlifonia, Marekani na kutolewa kwenye internet mwezi Septemba.
Miongoni mwa wale walioshtakiwa ni mtengezaji wa filamu yenyewe Morris Sadek ambaye ni raia wa Misri.
Mahakama itatoa hukumu ya mwisho mwezi Januari kufuatia itikio la Mufti
chanzo:bbc

Mwanamke ajifunguwa makaburini na kumzika kichanga akiwa hai huko Songea.

Haya wasikilize MZEE SMALL NA BI CHAU

Udom yachunguza wanafunzi wanaojiuza

Serikali  ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (Udoso), imeanza kuchunguza tuhuma za baadhi ya wanafunzi kujihusisha na biashara ya ukahaba ili kuwachukulia hatua za kinidhamu.

Udoso ilichukua hatua hiyo baada baadhi ya vyombo vya habari nchini kuripoti taarifa kuwa baadhi ya wanafunzi wa chuo hicho wanajihusisha na biashara hiyo ya ngono.

Akizungumza na waandishi wa habari jana kwa niaba ya wanafunzi hao, Rais wa Udoso, Yunge Paul, alisema kuwa tayari kazi hiyo imeanza na watakaobainika watachukuliwa hatua za kinidhamu.

Alisema kuwa watu hao wanashusha heshima ya chuo hicho kikubwa na kama taasisi ambayo imebeba wasomi wengi na ni kioo cha jamii.

Aidha, alisema taarifa hiyo ya kashfa ya ngono iliyoripotiwa na vyombo vya habari imesononesha nchi nzima ukiwamo uongozi wa chuo.

“Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari kwa kweli imesononesha nchi nzima ikiwamo Udom yenyewe na wanafunzi na hivyo kuwajengea mashaka hata waajiri wao ambao wanatambua wapo hapo kwa ajili ya kusoma,” alisema.

Aliwaomba waandishi wa habari kushirikiana na taasisi hiyo katika kuhakikisha wale wote wanaojihusisha na biashara hiyo wanabainika.

Wiki iliyopita kituo kimoja na televisheni kilionyesha picha za baadhi ya wasichana wanaodaiwa kuwa ni wanafunzi wa chuo hicho wakifanya biashara hiyo katika moja ya mitaa ya mjini hapa.

Pia katika mahojiano hayo, baadhi ya wanafunzi walionyesha kusikitishwa na vitendo hivyo na kuongeza kuwa vinawadhalilisha.

Kwa upande wake, Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Profesa Idrissa Kikula, alikaririwa akisema ni vigumu kuwabaini wanafunzi wanaojihusisha na biashara.

Alisema watatumia Jeshi la Polisi kuwabaini wanafunzi hao ili wachukuliwe hatua.
chanzo:nipashe

Wednesday, 28 November 2012

PICHA ZA SAFARI YA MWISHO YA NDUGU YETU SHARO MILIONE!










                                       









picha na Milladyayo, moronew blog na bongonewztz

Ajali ilivyokatisha maisha ya Sharo Milionea







                           picha za ajali ya gari chanzo Millard Ayo              
“Sharo alianza kuchipua, ameanza kujitegemea yeye kama yeye, sababu katika maisha lazima uanze wewe, pili uiangalie jamii inahitaji nini kwako.
“Alijitahidi, amejipatia usafiri maskini ya Mungu, kapata pa kulala, katoka Dar kwenda Tanga kuwaona wazazi kwa gharama zake mauti yamemkuta. Jambo la msingi tumuachie Mungu na kuondoa mawazo mabaya kuhusu na kifo chake.”
Filamu alizoshiriki
Sharo Milionea aliibuka katika filamu mbalimbali akiigiza na King Majuto, ikiwemo ‘Mtoto wa Mama’ Back From New York, Kitale na Sharo ambayo ni tangazo ambalo limeingizwa kwenye milio ya simu.
Msanii huyo alipata umaarufu zaidi katika matangazo yake ya Airtel Money akiwa na King Majuto pamoja na lile la Azam Cola hasa staili yake ya kuongea ‘Kisharobalo’ akitumia maneno kama ‘Haaa! nimebugi meeeen! Ooooooh Mamaaa.
Akimzungumzia msanii huyo, Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel, Beatrice Mallya alisema tasnia ya sanaa imepoteza mtu muhimu kwani ndiyo alikuwa anaanza kuja juu.
“Tunasikitika kama Watanzania wengine, hasa washabiki wake, alikuwa mcheshi, mtu wa utani na masihara...sisi kama Airtel tutashiriki kikamilifu katika mazishi yake,” alisema Mallya ambaye hata hivyo alisita kusema kama watasitisha urushaji matangazo yake au la
“Hata kama angekuwa amefunga mkanda, kiukweli kwa jinsi gari hilo lilivyogonga mti mkubwa vile na kuuangusha, lazima angekatika kwani katupwa mbali sana,” alisema Bakari Hassan.
Kauli ya polisi
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tanga, Costantine Massawe alisema ajali hiyo ilitokea katika eneo la Songa Kibaoni, Wilaya ya Muheza na Sharomilionea (sasa marehemu) ndiye aliyekuwa akiendesha gari hilo.
Umati hospitalini
Katika Hospitali Teule wilayani Muheza, umati wa wananchi ulifurika baada ya kusikia aliyefariki katika ajali hiyo alikuwa msanii huyo.
Katika mji wa Muheza na vitongoji vyake wananchi walimiminika hospitalini hapo wakiongozwa na Mbunge wa Jimbo la Muheza, Herbert Mntangi na Mkuu wa Wilaya ya Muheza, Subira Mgalu kushuhudia hali hiyo.
Mntangi alilazimika kufanya kazi ya ziada ya kuwasihi wananchi waliokusanyika chumba cha maiti wakiwa na shauku ya kuingia ndani kuushuhudia mwili wa msanii huyo.
“Jamani naomba fanyeni subira, subirini wataalamu wafanye uchunguzi kwanza, lakini pia inabidi uandaliwe utaratibu maalumu wa namna ya kuushuhudia mwili.
“Hivi mnavyofanya vurugu siyo ustaarabu,” alisema Mntangi, na baada ya kauli yake ndipo wananchi wakaachia lango la chumba cha maiti.
Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali hiyo, Julius Mgema alisema polisi ndiyo walioufikisha mwili wa marehemu hospitalini hapo saa 3 usiku na wakaupeleka kwenye chumba cha kuhifadhia maiti kwa ajili ya taratibu nyingine.
Familia ilivyopokea taarifa

Msanii Hussein Ramadhani "Sharo Milionea" amefariki dunia, hivi ndivyo ITV ilivyotangaza

USIKOSE KUANGALIA VIDEO HIII YA MAISHA YA MASELA:El Salvador's MS-13 gang: Life on the inside

King Majuto amlilia Sharo Milionea

                                           Mzee majuto na sharobaro milionea

                                        Sharobaro milionea
KIFO cha msanii Hussein Ramadhan ‘Sharo Milionea’ kimemshutua msanii mwenzake King Majuto hadi akaanguka na kupata shinikizo la damu.

Majuto alipatwa na hali hiyo baada ya kupata taarifa za msiba huo na hadi anazungumza na gazeti hili, ingawa alikuwa na nafuu, mwili wake ulikuwa umevimba.

Akizungumza na Mwananchi Majuto alisema: “Kimeniuma sana kifo cha mwanangu Sharo.
“Nimeshirikiana naye kwa mambo mengi, nilifahamiana naye tangu mwaka 2009 tulikutana pale Vijana Production, na tangu nimefahamiana naye, kuna mambo mengi sana tumefanya,” alisema Majuto ambaye mara baada ya kupata taarifa ya kifo cha msanii huyo alipata na shinikizo la damu.

“Nilimuongoza kwenye mambo mengi na siku zote nilikuwa nikimsihi asikimbilie kuoa kama walivyo vijana wengine ambao wakipata hela kidogo wanachokimbilia ni kuoa.
“Nilikuwa ninamwambia jenga maisha yako kwanza, hakikisha unakuwa na nyumba, gari na miradi, ili hata ukioa mtoto asipate shida nashukuru alinisikiliza alianza kupata mafanikio kifo ndo kimemchukua.

“Sijui nisemeje kifo kina siri nzito, ningejua anakufa lini ningekata rufaa na hata kutoa rushwa lakini hiyo ni siri ya Mungu pekee...alikuwa ameanza kupata mafanikio masikini, sijui ni macho mabaya ya watu, sijui Mungu pekee ndio anajua kwa sababu alikopatia ajali wala hakukuwa na kona kali.

“Alikuwa meneja wangu, matangazo yote mnayoyaona yeye ndio alikuwa akiingia mikataba yote na fedha zote, hakuwa mdhulumishi, kazi zote tulizofanya pamoja na yeye ndio alikuwa akisimamia, akiniambia mzee tusifanye hii kazi nami sifanyi.

“Alikuwa ana msimamo wake, akisema Sh1milioni ni hiyo hiyo habadiliki tofauti na mimi na roho ya huruma, nikimtajia mtu bei akiniomba basi napunguza, sifanyi hivyo kwa njaa, hapana, ila ni ile imani niliyonayo sasa tofauti na Sharo.

“Sidhani kama pengo lake kwangu litazibika na sijui kazi zangu nitazifanyaje tena bila yeye, alikuwa ni kila kitu kwangu pamoja na kumzidi umri.”
Mwenyekiti Simba
Mwenyekiti wa Klabu ya Simba, Ismail Aden Rage alitoa pole kwa wadau wa filamu na kumuelezea marehemu Sharo Milionea kuwa hakuwa msanii wa kawaida kwani ni miongoni mwa kizazi kipya cha vijana wa Kitanzania walioamua kutafuta maisha kwa kutumia vipaji walivyopewa na Mungu.

Yeye alijitumbukiza zaidi katika uchekeshaji na baadaye akaonyesha uwezo mkubwa katika fani ya muziki.
Maisha ya Sharo Milionea
Kila kona za miji na vitongoji vyake nchini, huwezi kukosa kusikia watoto wakisema ‘umebugi meen...nataka kula meen’ na yote hiyo ni staili na ubunifu wa msanii huyo.

Sharo Milionea aliyejizolea umaarufu kwa staili yake ya utembeaji na uongeaji, na aliwateka mashabiki wa vichekesho hususani vijana na watoto kutokana na kubuni staili yake ya kuiga madoido ya watu wa Marekani, na kujiweka katika maisha ya juu ambayo kwa hakika hawezi kuyafikia.

Ingawa aliigiza maisha hayo yeye binafsi hakupenda kabisa staili hiyo ya maisha na lengo la kuigiza ni kuwafundisha wenye tabia kama hizo kuacha, kwani binadamu wote ni sawa na hakuna aliyebora kuliko mwingine.

Alizaliwa Septemba 12, 1987 Muheza, Tanga. Alijiunga na Shule ya Msingi Lusanga na baadaye akasoma Sekondari ya Kwabutu, Tanga.
Alipomaliza shule mwaka 2005, alihamia jijini Dar es Salaam kumfuata mama yake aliyekuwa akiishi jijini kwa muda mrefu.
Sharo Milionea alianza kujiingiza katika sanaa tangu akiwa shule ya msingi mkoani Tanga, alipoingia jijini Dar es Salaam hapo ndipo kipaji chake kilipozidi kukua baada ya kukutana na muigizaji mkongwe, Mzee Majuto na kujiingiza moja kwa moja katika kundi la Vituko Show.

Baada ya kukaa kwa miaka kadhaa ndani ya kundi hilo hatimaye Januari 2012 Sharo Milionea alijitoa na kujiunga na kampuni ya Al-Riyami, iliyowafadhili kama kikundi cha vichekesho, chenye maskani yake mjini Tanga.

Mtaa Wa tatu King Majuto

Tuesday, 27 November 2012

Best Steven Kanumba comedy with sharobaro Love & power

HILI NDIO GARI ALIYOPATA NAYO AJALI MAREHEMU SHARO USIKU WA JANA..



Gari alilopata nalo ajali marehemu HUSSEIN MKIETI a.k.a sharo milionea.

Mwili wa hayati Yasser Arafat wafukuliwa


Bwana Arafat alifariki dunia mwaka 2004 nchini Ufaransa baada ya kuugua kwa kipindi kifupi.
Maradhi yaliyopelekea kifo chake hayakubainika. Uamuzi wa kuufukua mwili wa Yasser Arafat katika kaburi lake lililoko ukingo wa Magharibi unafuatia makala ya televisheni iliyodai kupata mabaki ya madini ya kitonoradi aina ya Polonium kwenye nguo zake.
Wapalestina wengi wanashuku kwamba huenda Israel ilihusika katika kifo cha kiongozi huyo. Israel imekuwa ikikanusha shutuma hizo.
Uchunguzi wa mauaji dhidi ya Bwana Arafat umeanzishwa nchini ufaransa kufuatia ombi lililowasilishwa na mjane wake.
chanzo:bbc

Happy birthday Lilian Mtoka

I have three wishes for you on your birthday. First, I wish that this Birthday teaches you something new and beautiful. Second, I wish that you have a day that you'll remember forever with a smile. And third, I wish that such days keep coming in every single day.

Mashoga watano mbaroni Dar


POLISI jijijini Dar es Salaam inawashikilia wanaume watano wanaotuhumiwa kuwa mashoga kwa tuhuma za kuuza miili yao.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Marietha Komba, alisema jana kuwa watu hao walikamatwa juzi, majira ya saa 5:00 asubuhi maeneo ya Buguruni Chama wakati askari walipokuwa wakifanya msako.
Aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Sadan Hussein (17), Ranadhan Haji (35), Mathias Machumu (22), Joseph Salum (36), na Jawe Mgaya (35).
Alisema watuhumiwa hao watapelekwa mahakamani wakati wowote kuanzia sasa, kwani ni kosa la jinai kufanya vitendo hivyo.
Katika tukio jingine, Kamanda Komba alisema mwanaume mmoja ambaye hajafahamika jina lake amefariki akiwa chini ya mti baada ya kutapikana damu nyingi.
Mwanaume huyo anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 45-50 alikutwa juzi majira ya saa 7:00 mchana maeneo ya Vingunguti Majani ya Chai.
Kwa mujibu wa kamanda huyo, marehemu aliishiwa nguvu ghafla na kupumzika chini ya mti hatimaye kuanza kutapika damu na kufariki muda mfupi baadaye.
Kamanda Komba alisema chanzo cha kifo hicho bado hakijafahamika na mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa uchunguzi.
chanzo:daima

Wanachama wa CCM kupigwa marufuku kuitwa waheshimiwa.

Monday, 26 November 2012

JOKATE ATUMIKA KUTAPELI LAPTOP


SASA imeshakuwa ni kawaida kwa watu mbalimbali kutapeliwa kupitia mtandao wa Kijamii wa Facebook na watu wanaotumia majina ya mastaa.
Safari hii limetumika jina la  Miss Temeke 2006, aliyejikita kwenye tasnia ya filamu na kutamba kwenye mitindo kwa kutumia lebo ya kidoti, Jokate Mwegelo kumtapeli mwanafunzi wa kike wa chuo Kikuu cha Mzumbe kilichopo nje kidogo ya mji wa  Morogoro, Ijumaa Wikienda  linakujuza.
Tukio hilo lililotokea hivi karibuni baada ya mwanafunzi  huyo, (jina tunaliminya) kutapeliwa na Jokate ‘fake’ Kompyuta mpakato ‘laptop’ kupitia mtandao huo.
Kwa mujibu wa mwanafunzi huyo, awali alimuomba urafiki Jokate akiamini ni Jokate halisi, kumbe alikuwa akiwasiliana na Jokate feki.
“Siku moja Jokate aliniambia kuwa anatafuta ma-modo, kuna patna wake aitwaye Mario alikuwa akitokea Kenya na kuniuliza kama ningeiweza kazi hiyo, sikujivunga kwa kuwa hiyo ilikuwa ni mojawapo kati ya ndoto zangu,” alisema.
Baada ya kumkubalia, mwanafunzi huyo alitakiwa kutuma picha ili zionwe na Mario ambaye angefika Dar na baadaye kuelekea Arusha.
Mwanafunzi huyo akafanya kama alivyoagizwa kwa kuziingiza picha hizo kwenye mtandao wa Jokate, baada ya muda akaambiwa kuwa Mario ameziona na amezipenda. 
“Baada ya siku chache Jokate akaniambia kuwa Mario ametokea  kunipenda, hivyo anataka niwe mpenzi wake, nilikataa pamoja na vishawishi vingi hatimaye tukakubaliana kuendelea kufanya kazi tu.”
Mwanafunzi huyo anazidi kusema kuwa, siku nyingine Jokate alimpigia simu na kumwambia kuwa laptop yake imeharibika na Mario hana kompyuta ya kutumia.
“Akaniomba nimuazime laptop yangu ili Mario aitumie mpaka pale yake itakapopona, nilijua Jokate hawezi kuniibia nikamkubalia,” alisema Mwanafunzi huyo.
Siku ya tukio, Jokate alimpigia tena simu mwanafunzi huyo na kumwambia kuwa yeye atachelewa kufika Morogoro na anamtuma Mario chuoni kwao ili ampe laptop kisha watakutana kikaoni.
“Sijui ni kitu gani, baada ya kuitoa laptop yangu, nikahisi kuwa nimetapeliwa, akili zikanijia, nikampigia simu Mario lakini hakupokea, ukweli nilichanganyikiwa hata nyumbani sijawaambia wazazi wangu kilichonipata,” alisema kwa masikitiko.
Mwanafunzi huyo alisema kuwa, Mario akawa hapokei tena simu yake na alipopokea alisema neno moja tu, ‘Usinisumbue’ kisha kuikata.
Alizitaja  namba za Mario kuwa ni 0659 227 229 na mpaka gazeti hili lilipokuwa likienda mitamboni bado simu hiyo ilikuwa ikiita.
Jitihada za mwanafunzi huyo kwenda kwenye kampuni inayohusika na mtandao wa simu hiyo zilidhihirisha kuwa ametapeliwa baada ya  kuambiwa kuwa  mtu anayetumia simu hiyo haitwi Mario bali ana jina lingine.
“Nilijaribu kwenda polisi lakini nao walitaka niwape pesa ili waweze kumsaka mhalifu, kwa kweli sikuwa na pesa nikaona niachane nao,” alisema mwanafunzi huyo.
Hatimaye mwanafunzi huyo  aliamua kutafuta namba ya kweli ya Jokate, alipoipata ndipo alipogundua kuwa mlimbwende huyo hakuhusika  katika kutapeliwa kwake.
Jokate alipoongea na mwandishi wetu alisikitishwa na tukio hilo na kuwataka watu kuwa makini maana wizi huo umeota mizizi.
“Nimeumia sana kwa jina langu kutumika katika utapeli, ninaomba watu wawe makini na wengine waache tabia hiyo ya kutumia majina ya watu maarufu katika michongo yao,” alisema Jokate.
Hivi Karibuni, baadhi ya mastaa wa kike wakiwemo Wema Sepetu, Jacqueline Wolper na Agness Gerald ‘Masogange’ wamekumbwa na matukio ya kuhusishwa na matukio mbalimbali kutokana na majina yao kutumiwa na watu wengine katika mtandao huo.
chanzo:globalpublishers

Married Premier League star on £90,000 a week 'tricked model into two year affair by telling her he was a car salesman'




Premier League family man Kolo Toure had a two year tryst with a model after he fooled her into believing he was a car salesman, it is alleged
The Manchester City defender, who earns a lucrative £90,000 a week wage for the Premiership champions, hid behind sunglasses and caps when the pair were out to hide his real identity.
He even told 22-year-old Kessel Kasuisyo his name was 'Francois' as he bought her lavish gifts he claimed were paid for thanks to selling cars in his native Africa.
And all the while he was living a double life with the mother of his two children - marrying her in a ceremony in Africa during the alleged affair.
The 31-year-old is said to have kept up the charade for two years, routinely refusing to pose for photographs, and not allowing her to meet his family because of his strict Muslim heritage.
In fact it wasn't until two week ago that she discovered it was all a rouse - when a friend of hers recognised him and urged her to Google the former Arsenal star.
Speaking to the Sunday Mirror, Miss Kasuisyo said: 'I am devastated. On some of the wedding pictures he is crying but a few weeks before he was in my bed.
'Two or three weeks after the wedding he was at mine. Around the time he got married he called and said he was back in Africa and had just sold two cars.
'I believed everything he said, I am hurt and confused by it all. Maybe he wanted me to be a second wife. I just don’t know. Everything about his strange ­behaviour now all makes sense.'
He told her he was originally from Ghana, sold cars back in Africa and was a student in the UK, before the pair began an on and off relationship until December.

And despite lavishing her with lingerie, and even a £1,000 ring, he was heading back to his fiance of nine years, in the Manchester house they shared with their daughter and son.
By December she says he had stopped calling before he rekindled the affair nine months later - arriving at her house with a gold watch and 18 carat diamond earrings.
She said she still had no idea he was a top footballer and that he continued to hand her cash for food and to send back home to her mother in Zimbabwe .
Eventually she got fed up with his behaviour and the pair broke off all ties two and half months ago - only for her to discover that he wasn't who he said he was.
Touré who plays alongside his brother Yaya at Manchester City is a practicing Muslim and still lives with wife Awo, daughter Sania and son Yiassin.
He came to the UK in February 2002, when he joined Premier League outfit Arsenal from Ivory Coast side ASEC Mimosas.
He joined Manchester City in 2009 but was out of the game for six months from March 2011, when he failed a drugs test, having taken his wife's diet pills.
A source close to Toure told the Sunday Mirror: 'I have spoken to Kolo and he is denying ever knowing or meeting the girl.'
 http://www.dailymail.co.uk/

Amtoboa macho mkewe kwa wivu


WIVU wa mapenzi umemsababishia madhara Christina Nakamwela (38) mkazi wa Kijiji cha Sinyanga, Kata ya Ipande wilayani Kyela mkoani Mbeya, baada ya kupigwa na kujeruhiwa vibaya kwa kutobolewa macho yake na mumewe, Benard Mbembele.
Akisimulia mkasa huo, baba mzazi wa mwanamke huyo, Andason Nakamwela, alisema kuwa mtoto wake alipatwa na mkasa huo juzi saa 2:00 usiku baada ya mumewe kutoka kunywa pombe na kuanza kumuadhibu akimtuhumu kuwa alichelewa kupika kwa sababu alikuwa kwa mwanaume mwingine.
Alieleza kuwa baada ya kubishana kwa takribani nusu saa, ndipo mwanaume huyo alianza kumpiga mkewe kwa vitu vyenye ncha kali maeneo ya kichwani na hivyo kumjeruhi kisha kumtoboa macho yote mawili.
Nakamwela alifafanua kuwa, ugonvi huo uliamuliwa na mwenyekiti wa kijiji hicho, baada ya kusikia mayowe.
Alisema kuwa alipewa taarifa na mwenyekiti huyo baada ya tukio hilo na hivyo kulazimika kukodi usafiri na kumkimbiza mwanae katika hospitali ya Wilaya ya Kyela kwa ajili ya matibabu.
Mwenyekiti wa kijiji hicho, Frank Mbembele alithibitisha kuwepo kwa tukio hilo na kudai kuwa, kijana huyo alidhamiria kumuua mkewe kwa kuwa alikuwa akimpiga kwa kutumia kitu chenye ncha kali maeneo ya usoni.
Alibainisha kuwa, alitumia taratibu za kisheria kwa kuwaagiza mgambo wamkamate mtuhumiwa na kumfikisha katika kituo cha polisi cha wilaya ambako anashikiliwa hadi sasa.
Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya, Apasaria Lumisha, alikiri kumpokea mgonjwa huyo na kwamba juhudi zinafanywa ili kujaribu kuokoa uhai wake kwa vile alifikishwa hospitalini hapo akiwa hajitambui.

SHARO MILIONEA FT. DULLY SYKES - CHUKI BURE

Wanaomaliza vifungo hawataki kuishi uraiani


Idadi kubwa ya wafungwa wanaomaliza muda wa kutumikia vifungo vyao katika magereza mbalimbali nchini wanashindwa kukaa uraiani badala yake wanafanya mbinu za kurejea kwenye magereza.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Mambo ya ndani ya Nchi, Dk. Immanuel Nchimbi wakati akizindua karakara ya kutengezea magari pamoja na namba mpya za magari katika Gereza la Ukonga jijini Dar es Salaam jana.
Alisema katika utafiti imebainika kati wa wafungwa 100 wanaomaliza muda wao wa kifungo, 35 wanarudi tena gerezani baada ya kufanya vitendo vya kihalifu kwa makusudi .
Dk. Nchimbi alisema sababu kubwa inayosababisha kukithiri kwa hali hiyo ni tatizo la Jeshi la Magereza kutoweka kipaumbele kuwarekebisha kwa kuwapa mafunzo mbalimbali ya ufundi ili wanaporejea uraiani wawe kazi ya kufanya.
"Wimbi la watu wanaomaliza kifungo chao na kurejea tena gerezani linazidi kukua, kibaya zaidi watu hawa wanafanya makosa kwa makusudi wakijua watafungwa gerezani baada ya kushindwa kuishi kutokana na kutokuwa na kitu cha kufanya," alisema Dk. Nchimbi.
Hata hivyo, alisema uanzishwaji wa karakara ya magari ndani ya Gereza hilo utatoa nafasi kwa wafungwa kujifunza ufundi na watakapomaliza kifungo wataendeleza kazi hiyo.
Hata hivyo, Dk. Nchimbi alisema mradi huo wa utengenezaji wa magari uonyeshe mwanga wa utumishi bora wa Jeshi kwa magari yanayopelekwa hapo na taasisi mbalimbali za Serikali yatengenezwe kwa muda unaokubalika na gharama nafuu.
Alisema imekuwa kawaida kwa miradi mingi ya Serikali kuwa na nguvu ya soda kwa kufunguliwa kwa mbwembwe kubwa, lakini inapoanza kazi haidumu kwa siku nyingi na kuzusha malalamiko kwa wateja.
"Nimeona hapa mradi huu tunauzindua kwa mbwembwe lakini sitegemei ndani ya mezi sita mambo yanakuwa mabaya, imani yangu mtazidi kutuonyesha kuwa miradi yote inayoanziushwa na Jeshi inakuwa bora," aliongeza kusema.
Waziri Dkt. Nchimbi alisema kuna haja kwa sheria ya manunuzi ya Serikali kuangalia upya kwani nyingi haziendi na wakati na kusababisha ukwamaji wa vitu mbalimbali.
Akizungumzia namba mpya za magari za Magereza zinazoanzia na maneno ya MT, Waziri huyo alisema uamuzi huo unalenga kulitambulisha rasmi na kuweka uwazi kwa wananchi wote.
Awali kamishna Mkuu wa Magereza, John Minja alisema kuanzishwa kwa karakana hiyo kutaongeza kasi ya utendaji kazi kwa askari kurekebisha wafungwa kwa vitendo pamoja na kurahisisha jeshi hilo pamoja na Taasisi za Serikali kutumia pesa nyingi kutengeneza magari kwa taasisi zingine.
Aidha alisema namba za magari zimeanza kutumika baada ya waziri husika kuridhia kifungu namba 114 sura 168 ya usalama barabarani kama alivyopewa jukumu hilo kisheria.
Chanzo:nipashe

EMBU CHEKA KIDOGO: kitale na sharo jingle

BAHATI BUKUKU KORTINI

MWIMBAJI mahiri wa Injili Bongo, Bahati John Bukuku (pichani chini) yuko kwenye mchakato wa kutinga kortini kwa ajili ya kumburuza mumewe, Daniel Basila ili atoe talaka.
Kwa mujibu wa chanzo, Bahati ambaye wimbo wake wa Dunia Haina Huruma ameuchezea filamu, ataenda mahakamani Jumatatu ya keshokutwa lengo likiwa kuitaka sheria imsaidie aweze kupata hati ya talaka ya kutengana na mwanaume huyo ambaye haishi naye kwa miaka sita sasa.
“Bahati anasema lengo la Daniel ni kumuweka njia panda ndiyo maana aliahidi kwenda mahakamani wiki mbili zilizopita ili ashughulikie talaka lakini hakufanya hivyo, sasa Jumatatu atakwenda mwenyewe,” kilisema chanzo.
Wakati huohuo, habari zinadai kwamba Daniel amekuwa akisema wimbo wa mkewe, Dunia Haina Huruma ametungiwa yeye kama kijembe.
Risasi Jumamosi liliwasaka wote wawili kwa nyakati tofauti ili kujua ukweli wa madai hayo.
Bahati: “Mimi ninachotaka ni talaka, aliahidi mbele ya kaka yangu kwamba angeshughulikia wiki mbili zilizopita, lakini hajafanya hivyo. Kwa hiyo mimi kwenda mbele ya sheria ni sawa tu. Huo wimbo namshangaaa, kama aliwahi kufumaniwa basi kweli ni wake.”
Basila: “Nilibanwa na mambo, lakini nakumbuka ahadi, nitaitekeleza lakini naomba isiwe kwa presha sana. Kuhusu wimbo lini nimesema alinitungia mimi?”
chanzo:globalpublishers

Saturday, 24 November 2012

MGAMBO DAR WABOMOA BAR USIKU WANYWAJI WAKIWA NDANI

                                 
Dada mmoja ambaye ni mhudumu wa baa hiyo akichomolewa na Wasamaria wema  kutoka katika kifusi.

                                       Baadhi vitu vya baa hiyo vikiwa nje
           Mwandishi wa Global Publishers, Issa Mnally, akiangalia baadhi ya vitu vilivyoharibika.
                               Bi Matola akiwa haamini  kilichotokea akiwa ndio mmiliki wa baa hiyo. 

WANYWAJI katika baa moja iliyoko Tazara Magorofani, Manispaa ya Temeke, walinusurika kifo, baada ya mgambo wa manispaa hiyo kuivamia na kuanza kuibomoa mnamo saa 8.30 usiku wa kuamkia leo.

Wavunjaji hao walifika eneo hilo bila hata kuongozana na  mjumbe wala mwenyekiti wa serikali ya mtaa husika na hawakuwa na barua yoyote  ya kuelekeza  uvunjaji wa baa hiyo ambamo kulikuwa na watu waliokuwa wakipata vinywaji.
chanzo: globalpublishers