WE REALLY HAD THE TIME OF OUR LIVES.........
Monday, 31 December 2012
Friday, 28 December 2012
VIDEO YA DIAMOND PLATNUMZ X-MAS 2012 DAR LIVE
Mtwara watishia gesi kugeuka maji
MUUNGANO wa vyama vya upinzani mkoani Mtwara, umepinga gesi asilia kwenda Dar es Salaam na kuwahimiza wananchi wa kusini hususani mikoa ya Lindi na Mtwara kuungana kupinga suala hilo.
Vyama vilivyoungana kupinga gesi asilia isiondolewe Mtwara, ni NCCR-Mageuzi, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), UDP, TLP, ADC, APPT, SAU na DP.
Vyama hivyo vinafanya mikutano katika maeneo mbalimbali ili kuwaomba wananchi waungane nao kupinga gesi hiyo kuondoka kabla ya Wanamtwara hawajafaidika.
Makamu Mwenyekiti wa muungano huo, Uledi Abdallah, aliyasema hayo juzi kwenye mkutano wa hadhara uliofanywa katika Kata ya Madimba na Msimbati mkoani hapa.
“WanaMtwara lazima tuungane kwa pamoja gesi yetu isiondoke Mtwara, tusiogope na wala tusirudi nyuma tutetee haki yetu, kwani gesi ni mali yetu WanaMtwara…tuache mambo ya woga tusimame imara kutetea rasilimali yetu,” alisema Uledi ambaye pia ni Mwenyekiti wa NCCR -Mageuzi Jimbo la Mtwara Mjini.
Kwa upande wake, Mkuu wa Kaya ya Msimbati, Somoe Issa, alipinga gesi hiyo kupelekwa Dar es Salaam na kuongeza kuwa endapo wataendelea kung’ang’ania itageuka maji kwenye mabomba watakayotumia kusafirishia.
Alisema mara ya kwanza walipochimba gesi walishindwa kuendelea kutokana na mitambo kunasa kwenye shimo na kila walipojaribu kuitoa ilishindikana ndipo walipoenda kuwachukua mafundi kutoka Canada ambao nao walishindwa.
“Sasa kama mimi ndio niliowasaidia kunasua mitambo yao na wakaendelea na kazi zao ya uchimbaji wa gesi, basi nawaomba mimi kama mkuu wa kaya waachane mara moja na wazo la kuondoa gesi asilia Mtwara,” alisema.
Naye mkazi wa Msimbati, Juma Hassani, alisema kitendo cha serikali kutaka kuiondoa gesi hiyo si kitendo kizuri, kwani ni rasilimali pekee wanayoitegemea.
chanzo:daima
Vyama vilivyoungana kupinga gesi asilia isiondolewe Mtwara, ni NCCR-Mageuzi, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), UDP, TLP, ADC, APPT, SAU na DP.
Vyama hivyo vinafanya mikutano katika maeneo mbalimbali ili kuwaomba wananchi waungane nao kupinga gesi hiyo kuondoka kabla ya Wanamtwara hawajafaidika.
Makamu Mwenyekiti wa muungano huo, Uledi Abdallah, aliyasema hayo juzi kwenye mkutano wa hadhara uliofanywa katika Kata ya Madimba na Msimbati mkoani hapa.
“WanaMtwara lazima tuungane kwa pamoja gesi yetu isiondoke Mtwara, tusiogope na wala tusirudi nyuma tutetee haki yetu, kwani gesi ni mali yetu WanaMtwara…tuache mambo ya woga tusimame imara kutetea rasilimali yetu,” alisema Uledi ambaye pia ni Mwenyekiti wa NCCR -Mageuzi Jimbo la Mtwara Mjini.
Kwa upande wake, Mkuu wa Kaya ya Msimbati, Somoe Issa, alipinga gesi hiyo kupelekwa Dar es Salaam na kuongeza kuwa endapo wataendelea kung’ang’ania itageuka maji kwenye mabomba watakayotumia kusafirishia.
Alisema mara ya kwanza walipochimba gesi walishindwa kuendelea kutokana na mitambo kunasa kwenye shimo na kila walipojaribu kuitoa ilishindikana ndipo walipoenda kuwachukua mafundi kutoka Canada ambao nao walishindwa.
“Sasa kama mimi ndio niliowasaidia kunasua mitambo yao na wakaendelea na kazi zao ya uchimbaji wa gesi, basi nawaomba mimi kama mkuu wa kaya waachane mara moja na wazo la kuondoa gesi asilia Mtwara,” alisema.
Naye mkazi wa Msimbati, Juma Hassani, alisema kitendo cha serikali kutaka kuiondoa gesi hiyo si kitendo kizuri, kwani ni rasilimali pekee wanayoitegemea.
chanzo:daima
Mzungu anyongwa hoteli ya kitalii Dar
Raia wa Bulgaria, Rola Cheterolia (42), mfanyakazi wa casino ya Kilimanjaro inayomilikiwa na Hoteli ya kitalii ya Sea Cliff jijini Dar es Salaam, amenyongwa na watu wasiojulikana.
Mwili wa mwanamke huyo ulikutwa katika nyumba za kupanga zilizoko eneo la hoteli hiyo ya kitalii iliyoko Masaki.
Habari zilizothibitishwa na Jeshi la Polisi zinaeleza kuwa mwanamke huyo alinyongwa huku akiwa amefungwa mikono na miguu kwa kutumia kamba.
Marehemu alikuwa mfanyakazi wa casino hiyo na alikutwa na mkasa huo saa 3:00 usiku wa kuamkia jana.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Charles Kenyela, aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa tukio hilo lilitokea juzi usiku.
“Tunasikitika sana kwa kitendo hiki kilichofanywa na watu hawa wasiojulikana cha huyu mwanamke wa kigeni kuuawa huko Sea Cliff, lakini bado tunafuatilia kwa kina kwani upelelezi unaendelea kubaini waliohusika katika tukio hilo,” alisema Kamanda Kenyela.
Kamanda Kenyela alisema kuwa uchunguzi wa awali umebaini kwamba hakukuwa na dalili zozote za uvamizi ama ujambazi.
Hata hivyo, alisema kuna uwezekano wa tukio hilo kuwa la ulipizaji kisasi, lakini alisisitiza kuwa upepelezi bado unaendelea.
Alisema mlinzi wa eneo hilo alikimbia baada ya tukio hilo na Jeshi la Polisi linaendendelea kumsaka.
Uongozi wa Hoteli ya Sea Cliff ulipoulizwa jana kuhusiana na tukio hilo, ulithibitisha kutokea na kusema kwamba marehemu aliuawa juzi usiku.
Mwili wa mwanamke huyo ulikutwa katika nyumba za kupanga zilizoko eneo la hoteli hiyo ya kitalii iliyoko Masaki.
Habari zilizothibitishwa na Jeshi la Polisi zinaeleza kuwa mwanamke huyo alinyongwa huku akiwa amefungwa mikono na miguu kwa kutumia kamba.
Marehemu alikuwa mfanyakazi wa casino hiyo na alikutwa na mkasa huo saa 3:00 usiku wa kuamkia jana.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Charles Kenyela, aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa tukio hilo lilitokea juzi usiku.
“Tunasikitika sana kwa kitendo hiki kilichofanywa na watu hawa wasiojulikana cha huyu mwanamke wa kigeni kuuawa huko Sea Cliff, lakini bado tunafuatilia kwa kina kwani upelelezi unaendelea kubaini waliohusika katika tukio hilo,” alisema Kamanda Kenyela.
Kamanda Kenyela alisema kuwa uchunguzi wa awali umebaini kwamba hakukuwa na dalili zozote za uvamizi ama ujambazi.
Hata hivyo, alisema kuna uwezekano wa tukio hilo kuwa la ulipizaji kisasi, lakini alisisitiza kuwa upepelezi bado unaendelea.
Alisema mlinzi wa eneo hilo alikimbia baada ya tukio hilo na Jeshi la Polisi linaendendelea kumsaka.
Uongozi wa Hoteli ya Sea Cliff ulipoulizwa jana kuhusiana na tukio hilo, ulithibitisha kutokea na kusema kwamba marehemu aliuawa juzi usiku.
Thursday, 27 December 2012
Msikilize Jackline Wolper ndani Mkasi -SO5E05
Hivi Ndivyo Ilivyokua X-Mas Bata
Subscribe to:
Posts (Atom)
