Wednesday 30 May 2012

IDDY SIMBA NA WENZAKE KORTINI!!



ALIYEKUWA Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Usafiri Dar es Salaam (UDA), Iddi Simba, Meneja Mkuu Victor Milanzi na mjumbe Salim Mwaking'inda, wamefikishwa mahakamani wakikabiliwa na mashitaka saba, yakiwamo ya kujipatia Sh milioni 320 za shirika hilo kinyume cha sheria. 

Vigogo hao wa Uda walisomewa mashitaka yao jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, na wakili wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, Ben Lincon mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Ilvin Mugeta, na baada ya kukana mashitaka waliachiwa kwa dhamana. 

Washitakiwa hao waliachiwa baada ya kutimiza masharti yaliyowataka kusaini hati ya dhamana ya Sh milioni 500 kila mshitakiwa na kutoa mali isiyohamishika ambapo Simba alitoa hati ya kampuni ya Keys. 

Mashitaka ya kwanza kusomwa yalihusu kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu ambapo ilidaiwa kwamba Septemba 2, 2009 Simba na Milanzi walitenda kosa hilo. 
ENDELEA KUSOMA HAPA:http://www.habarileo.co.tz/kitaifa/?n=30688

No comments:

Post a Comment