Thursday, 11 October 2012

JOHN POMBE MAGUFULI AWATIA ADABU WACHINA NA KUWAPA FUNDISHO!!!!!


KAMPUNI ya Kichina ya Chico imeanza kubomoa na kujenga upya kipande cha barabara ya  lami kati ya Shelui na Mlima Sekenke, mkoani Singida chenye urefu wa zaidi ya kilomita 33.
Akizungumza na viongozi wa Mkoa wa Singida baada ya kukagua eneo hilo jana, Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli alisema  kampuni hiyo inatakiwa kubomoa na  kujenga upya  kipande  hicho kwa gharama zake  yenyewe, baada ya uchunguzi  uliofanywa kuonyesha ujenzi ulifanyika chini ya kiwango.
Dk Magufuli alisema  barabara hiyo iliyojengwa kwa zaidi ya Sh35 bilioni mwaka 2008 zikiwa mkopo, ilitarajiwa kudumu kwa zaidi ya miaka 15 lakini imebomoka  kipindi kifupi.
Dk Magufuli alisema serikali imechukua hatua hiyo ili kutoa fundisho kwa kampuni nyingine zinazoteleleza miradi chini ya kiwango na kusababisha hasara kwa Watanzania.
Alitoa  onyo kwa makandarasi washauri na wahandisi wanaopewa jukumu  la kusimamia miradi hiyo, kuwa makini.
Kwa mujibu wa  mkataba ujenzi huo unatarajiwa kukamilika kabla ya Januari 30, mwakani.
chanzo:mwananchi

No comments:

Post a Comment