Thursday 27 February 2014

Waumini watwangana makonde Msikitini.

WAUMINI wa Kiislamu wanaoswali katika Msikiti wa Mji wa  Zamani uliopo Mtaa wa Mji Mwema, wilayani Mpanda, wamepigana  makonde ndani ya msikiti  katika suala la kuamua nani  awe imamu wa msikiti huo.
Tukio hilo lilitokea Februari 21, mwaka huu, saa 8 mchana baada ya kumalizika kwa Ibada ya Ijumaa iliyofanyika katika msikiti huo iliyokuwa ikiongozwa  na Sheikh Hussein Mkumba.
Hali ndani ya msikiti huo ilianza kubadilika baada ya swala hiyo ambapo Kaimu Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Ally Hussein, ambaye pia ni Sheikh Mkuu wa Wilaya ya Mpanda, aliposimama na kuwaeleza waumini hao  kuwa hatua inayofuata ni ya kumkabidhi hati ya uimamu  mpya wa msikiti huo, Yassin Kasote.
chanzo:tz daima

No comments:

Post a Comment