Thursday 2 June 2011

FLAVIANA MATATA KATIKA KUSAIDIA JAMII.




Flavia (Miss Universe Tanzania 2007 na mwanamitindo wa kimataifa) ameanzisha mfuko wa FLAVIANA MATATA (FLAVIANA MATATA FOUNDATION) ukiwa na madhumuni ya kusaidia watoto ikiwa ni kumbukumbu kwa mama yake mpendwa ambaye alifariki kwenye ajali ambayo kamwe Watanzania hawataweza kuisahau, ajali ya MV Bukoba iliyotokea kwenye ziwa Victoria mwaka 1996, ambayo iliua watu zaidi ya 1000.
. Halfa ya uzinduzi huo ilifanyilka jana (31.5.2011) katika hoteii ya Kempisk jijini Dar es Salaam, ikiwa imehudhuliwa na waheshimiwa na marafiki zake. 
Pia aliwashukuru wote ambao wamemwezesha kufika hapo alipo.
POLE SANA DADA FLAVIANA, KWANI MUNGU NDIYE ALIYETOA NA AKATWAA.
NA
HONGERA SANA DADA FLAVIANA KWA HATUA ULOCHUKUA YA KUSAIDIA JAMII , MUNGU AWE KIONGOZI WAKO KWA KILA UFANYALO. 

AMINA

No comments:

Post a Comment