Thursday 6 September 2012

MAHARAMIA WAITEKA MELI YA MAFUTA NIGERIA!!!!

Shirika la kimataifa la mabaharia, liliambia shirika la habari la AFP kwamba mabaharia 23 walikuwa kwenye meli hiyo wakati ilipotekwa na walikuwa wamejifungia ndani ya chumba kimoja salama wakati wa tukio hilo.

Wadadisi wanasema kuwa visa vya uharamia vimekithiri katika maeneo mengi ya Afrika Magharibi.
Shirika la kimataifa la mabaharia, linasema liliweza kurekodi visa kumi na saba vya utekaji nyara wa meli nchini Nigeria, katika miezi ya kwanza sita ya mwaka huu. Linasema kumekuwa na ongezeko kubwa la visa hivyo ikilinganishwa na mwaka 2011.
Mkuu wa kituo cha shirika hilo cha kuripoti visa vya uharamia nchini Malaysia, Noel Choong, amesema kuwa wale waliofanya kitendo hicho, huenda ni kundi moja la maharamia walioteka nyara meli za mafuta nchini Togo mwezi jana, kuiba mafuta na baadaye kuwaachilia mabaharia waliokuwa kwenye meli hiyo.
Luteni Omodara anasema kuwa helikopta moja inatumiwa kuisaka meli hiyo katika juhudi za kuikoa.
Mwaka jana Nigeria na nchi jirani ya Benin zilianza mpango wa pamoja wa kuweka usalama baharani ili kupambana na uharamia.
chanzo:bbc

No comments:

Post a Comment