Monday 17 December 2012

Wataka wanawake waruhusiwe kuchumbia


MKAZI wa Wilaya ya Arumeru, mkoani Arusha, Phillipo Tango (25), amependekeza Katiba Mpya itoe haki na usawa katika suala la ndoa kwa wanawake kuruhusiwa kuchumbia, kutoa mahari na kuoa wanaume wanaowapenda na kukubaliana.
Akitoa maoni yake mbele ya Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Mpya juzi, Tango ambaye ni mkazi wa Kata ya Olmotonyi, wilayani Arumeru alisema lazima Katiba hiyo mpya ikomeshe mfumo dume unaotawala suala la ndoa.
“Katiba itoe haki sawa kwa jinsi zote mbili katika suala la kuoana na haki zote za ndoa tofauti na sasa ambapo wanaume ndiyo wenye maamuzi makubwa kulinganisha na wanawake,” alisema Tango.
chanzo:mwananchi

No comments:

Post a Comment