Wednesday 5 June 2013

MBAKAJI aponea chupu chupu kuuawa, kwa kupigwa na kuchomwa moto!!!!




Mkazi mmoja wa Mwangata katika Manispaa ya Iringa amenusurika kuuwawa na wananchi baada ya kukutwa akimbaka binti wa miaka kumi.
Tukio hilo linaelezwa kutokea jana saa nane mchana, pale ambapo mzazi wa binti huyo alipomsikia mwanaye akilia kwa uchungu, na aliposogea kujua kulikoni, alimshuudia kijana huyo akiendelea na ubakaji jambo lililosababisha apige kelele kuomba msaada wa wananchi.
Kutokana na kushamiri kwa vitendo vya ubakaji katika eneo hilo, mtuhumiwa huyo alijikuta akipokea hasira za wananchi kwa kupigwa na kunusurika kuchomwa moto baada ya baadhi ya wananchi wengine kushauri afikishwe polisi.
Mtuhumiwa huyo amefikishwa katika kituo kikuu cha polisi mjini Iringa akivuja damu kichwani.

No comments:

Post a Comment