Monday 2 December 2013

Mkaguzi wa hesabu akutwa amekufa maji ndani ya mto

Mkaguzi wa hesabu katika Shirika la COASCO, Sabas Mlengela (54), amekutwa amekufa maji ndani ya mto, mjini hapa.
 
Walioshuhudia wamesema tukio hilo lilitokea jana asubuhi ambapo mwili wa mkaguzi huyo ulikutwa ukielea kwenye maji.
 
"Tulipofika katika eneo hili tuliona sikio la mtu ndani ya maji na baadaye tukabaini kuwa  mtu amekufa akiwa na baiskeli yake na simu yake ilikutwa nje," alisema shuhuda mmoja.
 
Alisema simu hiyo ndiyo iliyotumika kuwapigia ndugu zake kuwajulisha tukio hilo.
Aliongeza kuwa kifo hicho kina utata huenda kilisababishwa na utelezi uliomfanya atumbukie kwenye daraja au watu wabaya walimsukuma.
 
"Kwa kweli tunashindwa kuelewa nini hasa chanzo cha kifo hiki, nadhani marehemu atakuwa ameuawa na kutupiwa kwenye maji na watu wabaya kwani haiwezekani mwili uwe majini halafu simu yake isiwe majini, na hawa waliomuua nadhani siyo vibaka kutakuwa na fitina fulani tu," alieleza shuhuda mwingine alijitambulisha kwa jina moja la John.
 
Kaimu Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga, ACP Kihenya Kihenya, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema mwili wa marehemu ulikutwa umezama kwenye mto huo pamoja na baiskeli yake, ingawa simu yake na kalamu vilikuwa vimeanguka pembeni mwa mto huo huku mwili wake ukiwa hauna majeraha yoyote.
 
Kamanda Kihenya alisema kwa mujibu wa maelezo ya ndugu wa marehemu, siku moja kabla ya tukio walikuwa pamoja na Sabas kwenye kikao cha kuvunja kamati, aliondoka saa 3 usiku na hakuonekana mpaka walipopata taarifa za kukutwa akiwa amekufa.
chanzo:nipashe

No comments:

Post a Comment