Thursday, 31 May 2012

LULU AWATESA ASKARI!!!




IMEBAINIKA kuwa staa wa picha za Kibongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ anawapa wakati mgumu askari magereza na polisi kufuatia ulinzi mzito wanaolazimika kumpatia wakati wa kumpeleka mahakamani na kumrejesha mahabusu kwenye Gereza la Segerea, Dar es Salaam, Amani linafunguka.
Baada ya wiki kadhaa mambo kutulia na ulinzi kuwa wa kawaida tofauti na siku ya kwanza alipofikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Jumatatu wiki hii hali hiyo ilijirudia ambapo Lulu ambaye anakabiliwa na kesi ya kifo cha Steven Kanumba alifikishwa katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam akiwa na ulinzi wa kutisha.
Amani lilimshuhudia Lulu akishushwa mahakamani hapo akiwa mtuhumiwa pekee kwenye basi huku akisindikizwa na askari magereza wanawake zaidi ya kumi.
Mbali na askari magereza wanawake, kulikuwa na difenda la magereza lenye king’ora lililokuwa limejaa askari magereza wanaume na polisi wa kawaida.
ULINZI MAHAKAMANI
Mara baada ya ‘Kalulu Kadogo’ kufikishwa mahakamani hapo walipokezana na polisi wa mahakamani na katika kufumba na kufumbua, kila kona kulikuwa na askari waliokuwa wameimarisha ulinzi nje na ndani ya eneo hilo.
Maafande hao walishuhudiwa wakiwa wamevaa majaketi yasiyopenya risasi (bullet proof), kofia za chuma huku wakiwa na ‘mabunduki’ aina ya SMG zilizokuwa zimejaa risasi na mikanda ya risasi za ziada.
Wakati baadhi wakitanda ndani ya mahakama wakiwa wamemzunguka Lulu, wengine walizagaa nje huku wakizuia watu kukatizakatiza ovyo.

he Royal Navy Prepare For The Diamond Jubilee Thames Pageant At HMS President




Boats of the Royal Navy's Royal Barge Honour Guard pass under Tower Bridge on May 30, 2012 in London, England. The Royal Navy will be providing The Royal Barge Honour Guard during the Diamond Jubilee River Pageant on The River Thames on June 3, 2012

Father of 17 and his wife to appear in court today charged with murdering their six children in council house blaze !!!




The parents of six children who died when their house was gutted by fire were last night charged with their murder.
Mick and Mairead Philpott were due to appear before Southern Derbyshire Magistrates’ Court this morning.
They face six counts of murder after prosecutors decided that pressing charges was ‘in the public interest’.
This morning, more than 20 friends and members of the family turned up at court ahead of the hearing, including one man believed to be Mick Philpott's brother.

Read more: http://www.dailymail.co.uk/news/article-2152254/Derby-deaths-Mick-Mairead-Philpott-charged-murdering-6-children.html#ixzz1wRCOHvbI

WAPENDA "SURPRISE" ONE DAY MTAJIKUTA HAPA!!


NYOKA NI NYOKA, INAKUWAJE AWE RAFIKI WA BINADAMU?



Brendan Rodgers agrees deal to become new Liverpool manager!!

The 39-year-old will sign a three-year contract at Anfield and his appointment is likely to be officially confirmed within 24 hours.

Liverpool are negotiating a compensation package  - expected to amount to between £4m and £5m - with Swansea to secure Rodgers' services.
Liverpool sacked former manager Kenny Dalglish on 16 May after finishing eighth in the Premier League.
The Reds were 17 points away from a Champions League qualification spot, but won the League Cup and reached the FA Cup final.
In contrast, Northern Irishman Rodgers guided his Swansea side to an impressive first season in the top flight, including a 1-0 win over Liverpool on the final day of the season.

EMBU CHEZA KIDOGO MDAU NA SONGI LA- Xai Xai_A Dancer.VOB

ASKOFU MOKIWA ACHARUKA ZANZIBAR!!!

RAIS wa Umoja wa Maaskofu Afrika Mashariki na Kiongozi wa Kanisa la Anglikana Tanzania, Askofu Dk Valentino Mokiwa amesema waumini Wakristo hawaridhishwi na utendaji kazi wa Polisi ukiwemo ufuatiliaji wa matukio ya kuchomwa moto kwa makanisa visiwani Zanzibar. 

Akizungumza katika kikao kilichokutanisha viongozi wa Dini na Serikali katika Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais jana, Dk Mokiwa alisema Polisi imeshindwa kufuatilia matukio ya uhalifu ikiwa ni pamoja na kuchomwa kwa makanisa hayo. 

Alisema tangu mwaka jana zaidi ya makanisa 25 yamechomwa moto na hakuna kesi iliyofikishwa mahakamani. 

“Matukio mengi ya kuchomwa moto kwa makanisa yamejitokeza Zanzibar tangu mwaka jana lakini hakuna kesi iliyofikishwa mahakamani au mtu aliyekamatwa,” alisema Dk Mokiwa. 

Aidha, alisema hadi sasa wafuasi Wakristo wanafanya kazi zao kwa hofu na wasiwasi kwani baadhi ya watu bado wanashambulia nyumba za ibada ikiwa ni pamoja na kurusha mawe. 

“Hadi sasa wafuasi wetu wanafanya kazi zao kwa wasiwasi mkubwa hata katika nyumba za ibada kwani wafuasi wenye siasa kali wanarusha mawe katika nyumba za ibada,” alisema. 
ENDELEA KUSOMA HAPA:http://www.habarileo.co.tz/kitaifa/?n=30756

WANAFUNZI CHUO KIKUU WABAKWA,WALAWITIWA!!!

WANACHUO wa Chuo Kikuu cha St John mjini Dodoma, leo wamegoma kuingia madarasani hadi wawasilishe malalamiko yao kwa Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Zelothe Stephen kutokana na kukithiri kwa vitendo vya kupigwa nondo, kuibiwa kadi za benki, kompyuta za mkononi, kulawitiwa na kubakwa. 

Hali hiyo ilisababisha wanafunzi kukusanyika huku wakiwa wamebeba mabango mbalimbali ambayo yalikuwa yakisomeka, ‘Tunaomba ulinzi ili kubaka na kulawitiwa kukomeshwe’, ‘Ulinzi ni haki yetu ya msingi polisi Mko wapi? Tumechoka kuwa wajinga katika jamii yetu na Ulinzi Shirikishi stop crime.’ 

Baadhi ya wanafunzi hao walilaani vitendo vya wenzao kubakwa na kulawitiwa na kudai kuwa katika siku za hivi karibuni, mwanafunzi wa kiume ambaye anasoma mwaka mwaka wa pili aliibiwa na kisha kulawitiwa hali iliyolazimu alazwe hospitali. 

“Kesi kadhaa zimepelekwa polisi lakini hakuna chochote kinachofanyika,” alisikika mwanachuo moja akizungumza kwa jazba. 

Walisema kwa muda mrefu wamekuwa wakikabiliwa na wakati mgumu kutokana na kuibiwa vifaa muhimu zikiwemo kompyuta za mkononi hali ambayo hulazimika kuishi kwa hofu. 

Wednesday, 30 May 2012

MAKAVU LIVE KWA WANAWAKE KUTOKA KWA SHOSTI KIBOGA-Orijino Jimbeeeeeeee

" NI UTAMU ULIOJE"WEMA SEPETU AVISHWA PETE NA MWINYI KUTOKA MACHOZI BAND!!

                                     mpaka chini kwa heshima kwa kumvika pete wema
                                   
                                       baada ya pete malavidavi yaliendelea
                                                   Wema na Bodyguard
                                                    Na mashosti wake
                      kwa picha zaidi:http://djchoka.blogspot.co.uk/

WEMA NA JOKATE NUSURA WAZICHAPE!!


MASTAA wa kike wanaotambiana Bongo, Wema Sepetu na Jokate Mwegelo, ilibaki kidogo wazichape kavukavu kisa kikiwa kilekile, msanii anayetingisha katika Bongo Fleva, Naseeb Abdul ‘Diamond’.
Chanzo chetu makini kimenyetisha kwamba mtiti huo ulitokea Ijumaa Mei 25, mwaka huu katika Ukumbi wa Blue Pearl, Ubungo, Dar ambapo kulikuwa na Shindano la Miss IFM, 2012.
CHANZO KINADADAVUA
Katika ‘event’ hiyo, Wema alikuwa mmoja wa majaji waliochagua washindi wakati Jokate alifika kama mdau wa urembo huku uwepo wa Diamond ukiwa kwa ajili ya kupiga shoo.
“Wema alikuwa mmoja wa majaji, Jokate alikwenda kama shabiki tu, lakini mambo yalianza kuharibika baada ya mshindi kutangazwa ambapo Jokate hakuridhishwa na matokeo.
“Hata hivyo, watu walisema ni chuki zilizosababishwa na wivu wa kimapenzi kwa Diamond,” chanzo kilieleza.
JOKATE ALIANZA HIVI
Habari zinasema kwamba, Jokate aliamua kupita mbele ya meza ya majaji na kumuuliza Wema kama yeye aliridhika na matokeo yale.
“Ilikuwa balaa, Jokate alikwenda kwenye meza ya akina Wema (majaji), akaanza kumuuliza, yaani huyu ndiyo mshindi mliyetuchagulia? Miss gani anakuwa hivyo?” kilisema chanzo na kuongeza:
“Kifupi alikuwa akitoa kejeli kwa majaji hasa Wema kwa vile aliwahi kuiwakilisha Tanzania katika mashindano ya dunia.”
WEMA AKAMALIZA
Baada ya chokochoko za Jokate ambaye inasemekana alikuwa ‘amechangamka’ kidogo, Wema alijibu mashambulizi kwa staili ya aina yake, alikaa kimya akiendelea na shughuli nyingine.
“Ukimya wa Wema ukasababisha Jokate azomewe kwa sauti kubwa na mashabiki huku wakimsonya. Kiukweli bila ushabiki, Wema alionesha ukomavu siku ile.
“Kama naye angepandisha hasira, ilibaki kidogo sana wakung’utane, maana Jokate alionekana dhahiri kutaka ugomvi lakini mashabiki wakaununua kwa kumzomea. Aliabika sana,” kiliendelea kupasha chanzo hicho.
DIAMOND AAMSHA SOO UPYA
Wakati Diamond akiwa jukwaani ‘akipafomu’ wimbo wa Nimpende Nani? ikawa kama ameamsha ‘muziki’ upya kabisa kwa upande wa Jokate.

Euro 2012: Balotelli threatens to walk off if abused


Manchester City and Italy striker Mario Balotelli has threatened to walk off the pitch if he is racially abused at Euro 2012, which kicks off next week.
Balotelli added he would "kill" anyone who dared throw a banana at him in the street.
A recent BBC Panorama programme revealed cases of racism and anti-Semitism in football grounds in host nations Poland and Ukraine.
"If [racism] does happen I would leave the pitch and go home," said Balotelli.
"Racism is unacceptable to me, I cannot bear it. We are in 2012, it can't happen.
"If someone throws a banana at me in the street, I will go to prison because I will kill him."
The Panorama programme showed fans making Nazi salutes on the terraces, black players being taunted with monkey chants and a vicious assault on a group of Asian students.
Former England captain Sol Campbell advised fans not to travel, suggesting they would be risking their lives if they did so.

MWANAUME USIFIWA KULA!!!!


MAANDALIZI YA "DIAMOND JUBILEE YA QUEEN ELIZABETH 11




TETEMEKO LA ARDHI LASAMBARATISHA ITALY!!!







Tetemeko la ardhi lasambalatisha mji wa Mirandola nchini Italy,watu 16 inasemekana wamepoteza maisha yao na wengine majeruhiwa.

SONGI LA NESA NESA- FidoDido ft Tunda Man

IDDY SIMBA NA WENZAKE KORTINI!!



ALIYEKUWA Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Usafiri Dar es Salaam (UDA), Iddi Simba, Meneja Mkuu Victor Milanzi na mjumbe Salim Mwaking'inda, wamefikishwa mahakamani wakikabiliwa na mashitaka saba, yakiwamo ya kujipatia Sh milioni 320 za shirika hilo kinyume cha sheria. 

Vigogo hao wa Uda walisomewa mashitaka yao jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, na wakili wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, Ben Lincon mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Ilvin Mugeta, na baada ya kukana mashitaka waliachiwa kwa dhamana. 

Washitakiwa hao waliachiwa baada ya kutimiza masharti yaliyowataka kusaini hati ya dhamana ya Sh milioni 500 kila mshitakiwa na kutoa mali isiyohamishika ambapo Simba alitoa hati ya kampuni ya Keys. 

Mashitaka ya kwanza kusomwa yalihusu kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu ambapo ilidaiwa kwamba Septemba 2, 2009 Simba na Milanzi walitenda kosa hilo. 
ENDELEA KUSOMA HAPA:http://www.habarileo.co.tz/kitaifa/?n=30688

CCM YATAKA WAZIRI ZANZIBAR AJIUZULU!!

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar kimemtaka Waziri wa Sheria na Katiba wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), Abubakar Khamis Bakari ajiuzulu, kwa maelezo kuwa ameshindwa kuishauri vizuri Serikali kuhusu sheria na mwenendo wa vyama vya hiari nchini. 

Akizungumza na waandishi wa habari katika makao makuu ya CCM Kisiwandui, Unguja jana, Vuai Ali Vuai alisema kikundi cha kutoa mihadhara ya dini ya Kiislamu cha Jumuiya ya Uamsho, kimesajiliwa kutoa mihadhara ya dini na si kujishughulisha na siasa majukwaani. 

Alisema kitendo cha Abubakar kushindwa kuishauri vizuri Serikali kuhusu mwenendo wa kikundi hicho, kimesababisha maafa na kuiingiza nchi katika wasiwasi mkubwa kiasi cha kuvurugika kwa biashara na utalii. 

“CCM inamtaka Waziri wa Sheria na Katiba ajiuzulu mara moja, kwa sababu ameshindwa kumshauri vizuri Rais na Serikali kuhusu mwenendo wa kikundi cha Uamsho ambacho kinafahamika kazi yake ni kutoa mihadhara ya dini na si siasa,” alisema Vuai. 

AJINYONGA KWA MADAI YA UGUMU WA MAISHA!!

                                 mwili wa marehemu ukiwa unaning'inia baada kujinyonga

                                           Mke wa marehemu

MWANAMME mmoja ambaye hakutambulika jina lake, aliyekuwa mkazi wa Kigogo-Mbuyuni jijini Dar es Salaam asubuhi ya kuamkia leo (Mei 29), amejinyonga kwa madai ya ugumu wa maisha uliosababishwa na kukosa ajira.
Wakizungumza na mtandao wa huu, baadhi ya majirani ambao walihojiwa walisema kuwa jamaa huyo kwa muda mrefu alikuwa hana kazi hivyo kumsababishia ugumu wa maisha ambao ulikuja kumfanya ajinyonge.
“Siku zote mwanaume ameumbwa kutafuta riziki na si kukaa kusubiri kuletewa riziki. Jamaa huyu alikuwa akikaa tu nyumbani akimuachia mkewe aende akatafute riziki, matokeo yake ndio haya,” alisema jirani mmoja aliyekuwepo eneo la tukio.


habari zaidi:http://www.globalpublishers.info

Tuesday, 29 May 2012

MZUNGU ADAKWA AKIIBA FEDHA ATM!



RAIA mmoja wa Bulgaria, Petez Ninkov, 32, (pichani) amenusurika kuuawa baada ya kudaiwa kuiba fedha katika mashine ya kuchukulia fedha (ATM) jijini Dar es Salaam.
Tukio hilo lilitokea hivi karibuni katika Benki ya Standard Chartered, Tawi la Ilala ambapo mzungu huyo aliponea chupuchupu kupigwa baada ya kuokolewa na polisi ambao walikuwa doria na haraka wakamkimbiza polisi.
Habari ambazo tumezipata zinaeleza kuwa, tayari amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala kujibu mashitaka ya kuiibia benki hiyo fedha taslimu shilingi milioni 35.
Ninkov amefikishwa katika mahakama hiyo kujibu shitaka hilo la wizi katika benki hiyo tawi la Ilala jijini Dar es Salaam.
Mwendesha mashitaka wa serikali, Aidah Kisumo alidai mahakamani hapo kuwa mshitakiwa alitenda kosa hilo kati ya Februari 6 na Aprili 4 mwaka huu.
Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa, kati ya siku hizo mtuhumiwa aliiba Dola za Kimarekani 23,000 kutoka katika mashine ya kuchukulia fedha (ATM), mali ya Benki ya Standard Chatered huku akijua kuwa ni kosa.
Katika shitaka la pili Mwendesha mashitaka alidai kuwa, mtuhumiwa aliiba tena Mei 17, mwaka huu katika benki hiyo baada ya kupanga njama ya kutenda kosa hilo.
Hakimu anayesikiliza kesi hiyo, Tarsila Kisoka aliiahirisha kesi hiyo hadi Juni 6, mwaka huu na mshitakiwa ametupwa rumande baada ya kushindwa masharti ya dhamana ambayo ni kuwa na wadhamini wawili wanaotambuliwa na serikali ambao watasaini nusu ya mali iliyoibiwa.
Akizungumzia tukio hilo jana kwa njia ya simu, Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum Dar es Salaam, Suleiman Kova alisema ni lazima benki kuwa waangalifu kwa kuwa mbinu zinazotumika kwa wizi huo ni za kisasa. Ametoa wito kwa wananchi kutoa taarifa polisi wakimtilia shaka mtu yeyote aliye katika mashine za ATM


habari na http://www.globalpublishers.info/

KITIMU-TIMU CHA BOM MOI AVENUE KENYA!!

UJUMBE KWA WAJUMBE!!


MATEMBEZI YA AMANI YA WAZANZIBAR KUTUMA UJUMBE WAO KWA DUNIA

EDEN HAZARD SET TO JOIN CHELSEA FROM LILLE!!


Sought-after Lille midfielder Eden Hazard looks set to sign for Chelsea this summer after announcing he is joining the "Champions League winner".
The 21-year-old had reportedly attracted interest from several of Europe's top clubs, including Manchester City and Manchester United.

ALIYEKUPA WEWE NDIO KANYIMA YULE!!!


Woman student, 22, 'savagely raped' after she was thrown off night bus because she was 20p short on cost of fare!!! !!!



A law student was dragged into a park and savagely raped after being ‘turfed off’ the last bus home because she was 20p short of the £5 fare, a court has heard.
The 22-year-old victim was left stranded in a city centre at 3am after the bus driver refused to wait a few moments so she could withdraw extra money from a nearby cash dispenser.
But after walking for less than a mile, the prosecution claim she was targeted by drink-fuelled Joseph Moran, who then allegedly launched a ‘savage’ attack which was ‘almost devoid of any mercy’, a court heard.

Read more: http://www.dailymail.co.uk/news/article-2151270/Woman-student-22-savagely-raped-thrown-night-bus-20p-short-cost-fare.html#ixzz1wFUvrn00

NIDANGANYE ,NIDANGANYE TU! UKINIAMBAIA UKWELI NITAUMIA: Shetta ft Diamond - Nidanganye!!!!


VIDEO MIXCARTERTZ

KANISA LINGINE LACHOMWA ZANZIBAR!!!

BAADA ya Kanisa la Assemblies of God kuchomwa moto katika vurugu zilizoanza mwishoni mwa wiki iliyopita, jana Kanisa Katoliki Parokia ya Mpendae nalo limechomwa moto. 

Akizungumzia hali hiyo jana, kiongozi wa Kanisa hilo, Ambaros Mkenda, alidai kwamba Kanisa hilo lilichomwa moto na watu wasiojulikana na kusababisha uharibifu mkubwa. 

Alidai Kanisa hilo lilichomwa moto jana saa 8.30 mchana na watu wanaohisiwa kuwa wafuasi wa Jumuiya ya Kiislamu ya Uamsho, waliokuwa wakitoka katika Mahakama ya Mwanakwerekwe kusikiliza kesi ya wenzao waliokamatwa juzi. 

Mkenda alidai kuwa watu hao waliwazidi nguvu walinzi wawili wa Kanisa hilo na kuvunja lango kuu la kuingilia ndani ya Kanisa na kuchoma moto na waliharibu madirisha na vifaa kadhaa vyenye thamani ya Sh milioni 20. 

“Tunasikitika sana na uharibifu mkubwa uliofanywa katika Kanisa letu ambalo lilikuwa tegemeo kubwa kwa wafuasi wapatao 2,000 wa eneo la Parokia ya Mpendae na jirani,” alisema Mkenda. 
ENDELEA KUSOMA HAPA:http://www.habarileo.co.tz/kitaifa/?n=30651

Monday, 28 May 2012

"HEBU MWACHENI MUNGU AITWE MUNGU"-SAJUKI.

SAJUKI
                          
                                                Sajuki pembeni yake mkewe Wastara
HEBU mwacheni Mungu aitwe Mungu! Hatimaye habari njema kutoka katika Hospitali ya Saifee iliyopo jijini Mumbai, India anakotibiwa staa wa filamu za Kibongo, Sadick Juma Kilowoko ‘Sajuki’ zinatia faraja kwa Watanzania, Ijumaa Wikienda linakupa stori ‘exclusive’ kutoka nchini humo.
ANYANYUKA KITANDANI, AONGEA
Habari hizo njema zinaeleza kuwa Sajuki aliyeambatana na mkewe, Wastara Juma na kaka yake, hatimaye ameweza kunyanyuka kitandani na kuongea tofauti na siku aliyoondoka Bongo na mwanzoni alipofikishwa hospitalini hapo.
Akizungumza na Ijumaa Wikienda, mwishoni mwa wiki iliyopita kwa njia ya simu, Wastara alisema Sajuki alikuwa amepata nafuu na hali siyo mbaya kwani alikuwa na uwezo wa kuzungumza hivyo akampa simu ili azungumzie afya yake yeye mwenyewe jinsi anavyojisikia

UMAJO WA MATAIFA WAISHUTUMU SYRIA KWA MAUAJI MAKALI NCHINI UMO








Taarifa ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa imesema mji huo ulishambuliwa kwa makombora na vifaru, mashambulio ambayo taarifa hiyo imeyataja kuwa ni matumizi mabaya ya nguvu dhidi ya raia ambayo yanakiuka sheria za kimataifa.
Balozi wa Syria katika Umoja wa Mataifa, Bashar Ja'afari, amekanusha taarifa hiyo ambayo ameiita kuwa ni tsunami ya uongo unaoenezwa na wajumbe wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ambao wanaishutumu serikali yake kutokana na vifo hivyo.
Zaidi ya watu 100 waliuwa katika tukio ili.