Wednesday 4 July 2012

FIGO ZA DK ULIMBOKA ZAANZA KUFANYA KAZI!!!


AFYA ya Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari, Dk Steven Ulimboka imeendelea kuimarika baada ya kupata matibabu nchini Afrika  Kusini na sasa figo zake zimeanza kufanya kazi.Dk Ulimboka alipelekwa nchini huko mwishoni mwa wiki baada ya kushambuliwa na watu wasiojulikana kiasi cha kusababisha figo zake kushindwa kufanya kazi.Katibu wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), Dk Rodrick Kabangila alisema Dar es Salaam jana kwamba, hali ya Dk Ulimboka imeimarika na kuwaomba Watanzania wamuombee apone haraka.“Taarifa tulizozipata kutoka Afrika Kusini zinasema kwamba,  hali ya Dk Ulimboka imezidi kuimarika tofauti na alivyokwenda, figo zimeanza kufanya kazi ingawa kwa polepole na amefanyiwa vipimo vingine,” alisema Dk Kabangila na kuongeza:
“Pia ameanza kuzungumza, anawatambua watu vizuri na zaidi amewaomba Watanzania wamuombee apone haraka.”
Awali, chanzo kimoja cha habari kilidokeza kwamba  hali ya Dk Ulimboka imeimarika kutokana na kupatiwa huduma za matibabu kwa haraka kwa kufanyiwa pamoja na vipimo vingine, kile cha usafishaji damu na figo (Dalysis), mara kwa mara. Kabla ya kuondoka nchini, Dk Ulimboka alifanyiwa usafishaji huo mara mbili.

Madaktari walisema kuwa, kipimo hicho kililenga  kupunguza kiwango cha sumu iliyoonekana  kwenye damu, ambayo haikutambulika mara moja kama ilitengenezwa ndani ya mwili au vinginevyo kwa kuwa hakuna kipimo cha kubaini tatizo hilo nchini.

Migomo hospitalini
Licha ya huduma kurejea taratibu katika baadhi ya hospitali nchini, mgomo wa madaktari bingwa umeendelea chini kwa chini.Pia jana, Serikali imewataka madaktari wote walio katika mafunzo ya vitendo kuripoti Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, ifikapo Ijumaa.

Jana, wizara hiyo ilitoa taarifa ikitaka madaktari wote nchini wanaofanya mafunzo kwa vitendo (interns) ambao 

No comments:

Post a Comment