Thursday 15 November 2012

Wema Sepetu anusurika kutekwa!!!!


MISS Tanzania 2006 ambaye pia ni mcheza filamu mkali Bongo, Wema Isaac Sepetu, hivi karibuni alikumbwa na kizaazaa cha kutaka kutekwa na watu wasiojulikana wakimtuhumu kuwatukana kupitia Facebook.
Akizungumza na Amani jijini Dar juzi, Wema alisema tukio hilo lilimtokea Kijitonyama, Dar wakati akitoka kwenye mishemishe zake kuelekea nyumbani kwake.
Alisema alipofika maeneo hayo, gari asilolijua lilimpita na kwenda kusimama mbele yake kisha wakashuka watu asiowajua na kuanza kumuuliza ni kwa nini anawatukana katika mtandao wa kijamii wa Facebook.
“Nilivyosikia wanasema Facebook, roho yangu ikatulia maana najua kuna watu kama 37 wanaotumia jina langu na picha zangu kwenye Facebook, nilishuka kweye gari na kuanza kuwaelewesha kuhusu hilo, bahati nzuri walinielewa,” alisema Wema.
chanzo:globalpublishers

No comments:

Post a Comment