Wednesday 30 May 2012

CCM YATAKA WAZIRI ZANZIBAR AJIUZULU!!

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar kimemtaka Waziri wa Sheria na Katiba wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), Abubakar Khamis Bakari ajiuzulu, kwa maelezo kuwa ameshindwa kuishauri vizuri Serikali kuhusu sheria na mwenendo wa vyama vya hiari nchini. 

Akizungumza na waandishi wa habari katika makao makuu ya CCM Kisiwandui, Unguja jana, Vuai Ali Vuai alisema kikundi cha kutoa mihadhara ya dini ya Kiislamu cha Jumuiya ya Uamsho, kimesajiliwa kutoa mihadhara ya dini na si kujishughulisha na siasa majukwaani. 

Alisema kitendo cha Abubakar kushindwa kuishauri vizuri Serikali kuhusu mwenendo wa kikundi hicho, kimesababisha maafa na kuiingiza nchi katika wasiwasi mkubwa kiasi cha kuvurugika kwa biashara na utalii. 

“CCM inamtaka Waziri wa Sheria na Katiba ajiuzulu mara moja, kwa sababu ameshindwa kumshauri vizuri Rais na Serikali kuhusu mwenendo wa kikundi cha Uamsho ambacho kinafahamika kazi yake ni kutoa mihadhara ya dini na si siasa,” alisema Vuai. 

No comments:

Post a Comment