Monday, 28 May 2012

MTOTO AFA HARUSINI!!

MTOTO mwenye umri wa miaka minne, Hassan Ibrahim, mkazi wa Mburahati amekufa papo hapo baada ya kunaswa na umeme akiwa kwenye sherehe ya harusi. 

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Charles Kenyela alisema mtoto huyo alinaswa juzi saa 4.30 usiku katika eneo la Manzese ambapo ilifanyika harusi hiyo. 

Alisema kuwa mtoto huyo alinaswa na umeme baada ya kukanyaga waya uliounganishwa na spika ya muziki katika sherehe hiyo ambapo alikufa papo hapo. 

Kenyela alisema kuwa maiti amehifadhiwa katika Hospitali ya Mwananyamala na polisi wanaendelea na upelelezi zaidi wa tukio hilo. 
chanazo habari leo.

No comments:

Post a Comment