Saturday, 11 August 2012

MAELFU WAMZIKA ATTAS MILLS

Baadhi ya wakuu wa nchi za Afrika wapatao kumi na wanane na Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Marekani Hillary Clinton walihudhuria mazishi hayo katika uwanja wa historia ya uhuru mjini Accra.

Mills aliyeugua saratani ya koo kwa muda mrefu amefariki ikiwa imebaki miezi mitano tu kabla ya kufanyika uchaguzi wa urais ambao angegombea tena nafasi hiyo.
Mwandishi wa BBC mjini Accra anasema kifo chake kimewaunganisha Waghana katika majonzi.
Anasema kifo hicho kilionekana kama jaribio kwa demokrasia changa ya nchi hiyo.
Mills aliyeanza kipindi cha miaka minne ya urais mwezi Januari mwaka 2009, amerithiwa na makamu wake rais John Dramani Mahama.
Ghana imepongezwa na jumuiya ya kimataifa kwa namna ambavyo imeshughulikia kipindi cha mpito katika taifa hilo linalofahamika kwa siasa zake za mgawanyiko.
chanzo:bbc

No comments:

Post a Comment