Thursday 6 March 2014

Mama wa marehemu ashinda kesi ya kugombea MAITI ya mwanae.


 Hoyce Temu akipongezana na Dkt. Helen Kijo Bisimba baada ya upande wao kushinda kesi.
Marehemu Emmanuel Lewi Nambuo Temu (33) enzi za uhai wake.
HUKUMU ya kesi ya familia ya Miss Tanzania 1999, Hoyce Nambuo Temu, kuhusu mzozo mkubwa wa wapi pa kumzikia mwanafamilia mwenzao, Emmanuel Lewi Nambuo Temu (33) aliyefariki dunia Februari 16 mwaka huu katika Hospitali ya Temeke, Dar imetolewa leo katika Mahakama ya Wilaya ya Temeke ambapo Mama wa marehemu Emmanuel, Hilda Lewi ameshinda!
Mama wa marehemu Emmanuel, Hilda Lewi Nambuo alikuwa anashikilia msimamo kwamba, mwanaye akazikwe kwenye makaburi waliyozikwa mababu zao yaliyopo kwenye eneo la Kitahire, Old Moshi, Kilimanjaro lakini mjomba mtu aitwaye Jacob Nambuo Temu alikuwa akipinga.
Hukumu hiyo imetolewa na Hakimu Mkazi Mfawidhi, Kassim Mkwawa na mwili wa marehemu uliokuwa bado umehifadhiwa Hospitali ya Temeke utazikwa eneo la Kitahire, Old Moshi mkoaniKilimanjaro.
CHANZO:.globalpublishers

No comments:

Post a Comment