Friday 21 December 2012

Wolper: Biashara ya sabuni ilinipa umaarufu


NYOTA wa filamu aliyeteka soko la filamu kwa sasa, Jackline Wolper ‘Ilham,’amesema umaarufu wake haukuanzia kwenye uigizaji, bali tangu akifanya biashara ya kuuza sabuni ya unga katika maeneo mbalimbali, jijini Dar es Salaam.
Kupitia kipindi cha mikasi, Wolper alisema anashukuru nyota yake kung’aa tangu akiwa mtaani ambapo wateja walimwita dada wa sabuni kila alipopita.
Akizungumzia namna alivyoingia kwenye tasnia ya la filamu, msanii huyo alisema alishawishiwa na msanii Lucy Komba ambapo alimsadia kumkutanisha na wasanii wakubwa akiwemo Ray na Marehemu Steven Kanumba.
Anasema hao ndio alifanyanao kazi yake ya kwanza ya filamu ya ‘Oprah’ baada ya kutafuta msichana aliyelandana na Jackline Uwoya.
Kwamba, kuanzia hapo ndio akawa anaitwa na watu mbalimbali.
chanzo:daima

No comments:

Post a Comment