BIFU lisilojulikana mwisho wake lini baina ya wasanii wa muziki wa bongo fleva ambao wana asili ya visiwani Zanzibar, linazidi kuchukua sura mpya.
Katika bifu hilo, walianza AT na kundi lake la zamani la Off Side Trick, na sasa mwanadada Baby J naye ameingia.
AT na Off Side Trick wamekuwa wakitupiana vijembe kupitia nyimbo zao, bila kujulikana hasa chanzo cha ugomvi wao ni nini.
Lakini wakati mashabiki na wadau wa muziki wakishindwa kubaini chanzo baada ya Off Side Trick kutoka na wimbo wao ‘Kidudu Mtu’ na AT akawajibu na ‘Vifuu Tundu’, Baby J ametoka na ‘Domo Kaya’ akimshirikisha Gelly wa Rhymes.
Wimbo huo wa Baby J unadaiwa kuwa ni kijembe kwa AT.
No comments:
Post a Comment