Thursday, 21 July 2011

NGWAIR ANAKUPA KITU B.B.M!!!!!!!!!


MKALI wa mitindo huru (free style) nchini, Albert Mangwea ‘Ngwair’ muda si mrefu ataachia ngoma mpya inayokwendwa kwa jina la B.B.M.
Black Beauty Model ndiyo kirefu cha BBM na kibao hicho kimerekodiwa katika studio za Bongo Records chini ya mtayarisha P-Funk Majani.
Ngwair amesema kama kawaida wimbo huo utakuwa mkali kama ilivyo nyimbo zake zilizowahi kutoka nyuma.
Mkali huyo toka Chamber Squad amewahi kutamba na singo kama ‘Gheto Langu’, ‘Hostel’ na nyinginezo.

No comments:

Post a Comment