Friday, 31 May 2013

Hoja ya USHOGA yaleta machafuko bungeni

Hotuba ya Kambi Rasmi ya Upinzani kuhusu bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushrikiano wa Kimataifa  jana ilisababisha mtafaruku mkubwa bungeni na siku nzima Bunge likakwama kufanya shughuli zake.

Awali  Naibu Spika, Job Ndugai, aliahirisha Bunge asubuhi hadi jioni, lakini hata liliporejea jioni, aliliahirisha tena ili kutuliza hali ya hewa.

Vile vile, Msemaji wa Kambi hiyo, Ezekiah Wenje alinusuruka kupigwa ka wabunge wa Chama cha Wananchi (CUF), baada ya kuokolewa na askari wa Bunge na kupelekwa kusikojulikana kutokana na hotuba aliyokuwa ameitoa bungeni..

Vurugu zilianza wakati Wenje alipokuwa akisoma maoni ya kambi ya upinzani kuhusu Wizara hiyo na kukihusisha Chama cha Wananchi (CUF), na vyama vinavyoshabikia vitendo vya ushoga na usagaji duniani.

Wenje alikuwa anawasilisha hotuba ya kambi ya upinzani baada ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, kusoma hotuba yake ya bajeti kwa mwaka 2013/14.

 Hali ya hewa bungeni ilibadilika alipofika ukurasa wa saba wa hotuba yake aliposema itikadi za CUF ni za mrengo wa kiliberali ambazo miongoni mwa misingi yake ni pamoja na kupigania haki za ndoa za jinsia moja, usagaji na ushoga na kwamba hilo ndilo tangazo la chama hicho kwenye mtandao wao wa umoja wa maliberali duniani.

Uraia wawatesa Watanzania ughaibuni

WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, amesema Watanzania wengi walio ughaibuni wanaathirika sana na suala la uraia wa nchi mbili.
Membe alitoa kauli hiyo mjini hapa jana wakati akiwasilisha hotuba ya bajeti ya wizara yake kwa mwaka wa fedha 2013/2014, ambapo alibainisha kutokuwepo kwa sheria inayoruhusu uraia wa nchi mbili kunawafanya wakose ajira za kueleweka, huduma za afya, elimu na mikopo.
Membe alisema kuwa wizara hiyo katika maoni yake kwa Tume ya Katiba ililipa suala la uraia pacha kipaumbele kwa kuwa wanaamini kwamba kufanya hivyo kutawawezesha Watanzania walioko nje kuchangia kwa kiwango kikubwa maendeleo ya nchi.
Kuhusu ziara za viongozi wakuu wa kimataifa kuitembelea Tanzania, Membe alisema kuwa zimefungua milango mipya ya mashirikiano kati yake na mataifa pamoja na kuchochea na kukuza biashara.
Mbali na Rais wa Marekani ambaye anatarajiwa kuitembelea Tanzania hivi karibuni, Membe alisema kuwa vilevile kati ya Juni na Julai mwaka huu, Rais wa Sri-Lanka, Mahinda Rajapaksa, na Waziri Mkuu wa Thailand, Yungluck Shinawatra, watafanya ziara rasmi hapa nchni.
Nayo Kamati ya Mambo ya Nje katika maoni yake, ilisema kuwa licha ya wizara kukubali manufaa ya kutekeleza ushauri uliotolewa bungeni mwaka jana, mambo mengi hayakufanyiwa kazi kabisa.

Sunday, 26 May 2013

DAKTARI wa meno Alnord Limo aaga dunia kwa kujinyonga

DAKTARI wa meno wa Hospitali ya Wilaya ya Morogoro, Alnord Limo anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 40, amekutwa amefariki dunia kwenye chumba cha gesti huku habari zikidai alijinyonga kwa shuka.
Mkasa huo ulimfika daktari huyo Jumatano iliyopita kwenye nyumba ya kulala wageni ya Camel iliyopo Kihonda, kandokando ya barabara kuu ya Morogoro kwenda Dodoma. 
Mhudumu wa gesti hiyo ambaye aliomba hifadhi ya jina, kwa kuwa si msemaji mkuu wa kazini kwake, alidai siku ya tukio marehemu alifika kwenye gesti hiyo na kukodi chumba namba 2 ambapo walimchukulia kama mteja wa kawaida.
”Alikuja na kuomba chumba, tukampa namba mbili. Aliingia akiwa peke yake, lakini baada ya muda alitoka na kuja mapokezi, sijui alikuwa na shida gani, halafu akarudi tena ndani,” alisema mhudumu huyo.
Aliongeza kuwa asubuhi walipoona hatoki na muda wa kuondoka ulifika, ndipo walipoingiwa na wasiwasi na kwenda kufungua ambapo walimkuta amekufa.
Habari za ndani zaidi zilidai kwamba, daktari huyo alifunga ndoa miezi mitatu iliyopita na kwamba siku ya tukio mkewe alikuwa safarini.
Inadaiwa siku moja kabla ya tukio hilo alikusanya nguo zake na simu ya mkononi na kupeleka kwenye kambi ya kulea watoto yatima ya Mgolole iliyopo mjini hapa.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Faustine Shilogile alipohojiwa na mwandishi wetu alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa marehemu hakuacha ujumbe wowote.
chanzo:.globalpublishers

Lipumba aibua jambo zito kuhusishwa na video ya UDINI

MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, ameibua suala zito akikihusisha chama chake na “kumnusuru” Rais Jakaya Kikwete katika uchaguzi mkuu uliopita.
Tanzania Daima limefahamishwa kuwa Profesa Lipumba alitoboa siri hiyo katika Msikiti wa Idrissa, Kariakoo, jijini Dar es Salaam, alikokwenda kuswali swala ya Ijumaa, miezi kadhaa iliyopita.
Kwa mujibu wa video ya tukio hilo, ambayo gazeti hili lina nakala yake, Profesa Lipumba alikaribishwa kuzungumza na waumini hao mara baada ya utangulizi uliotolewa na Imamu wa msikiti huo, Sheikh Ali Basaleh, aliyemtaka awaeleze Waislamu hali ya kisiasa nchini kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2015.
Huku akisisitiza juu ya umuhimu wa mshikamano wa kiimani, Profesa Lipumba alianza kwa kuzungumzia matokeo ya uchaguzi mkuu wa 2010, na ushindani mkali wa kisiasa uliokuwapo.
Alisema hawaoni matunda ya jitihada walizofanya kumnusuru Rais Kikwete asishindwe, kwani hata chini ya uongozi wake, Waislamu wameendelea kutothaminiwa.
“Ninyi masheikh mnajua vizuri zaidi hali ya kisiasa ilivyokuwa, kwamba ilibidi zifanyike juhudi za makusudi ili kuokoa jahazi. Lakini pamoja na kuliokoa jahazi, hali halisi inaonyesha mpaka sasa hakuna matunda yoyote yaliyopatikana, na tupo katika mtihani mgumu zaidi,” alisema.
Katika hali ambayo inasemekana ushindi wa Rais Kikwete ulipatikana kwa mbinu, huku wengine wakiituhumu Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuwa ilimnusuru mgombea wa CCM, kauli hii ya Profesa Lipumba inadokeza kwamba anajua mkakati zaidi wa kazi ya Tume ya Uchaguzi.
Katika hali isiyo ya kawaida, Profesa Lipumba anaonekana kuhamasisha Waislamu kujipanga akisema “wenzetu wameanza kujipanga” kuelekea 2015.

Siri ya vurugu za Mtwara hii hapa

SIRI za mzozo wa gesi mkoani Mtwara, imeelezwa kuchangiwa na udhaifu wa serikali pamoja na vyombo vya dola, Tanzania Daima Jumapili limedokezwa.
Mzozo huo ambao tayari umeshasababisha vifo, maafa na madhara makubwa ya uharibifu wa mali na baadhi ya watu kuachwa majeruhi, unadaiwa kutokana na uzembe wa serikali kupuuza hoja za msingi za wananchi wa Mtwara, pamoja na vyombo vya dola, hasa Idara ya Usalama wa Taifa kutokuwa makini katika kubaini mipango ya vinara wa mzozo huo.
Ingawa Bunge limeunda kamati teule kwenda kuchunguza chanzo cha vurugu hizo, taarifa za kiintelijinsia zinataja makundi makubwa matatu kwamba yako nyuma ya vurugu hizo.
Makundi hayo ni pamoja na wanasiasa, serikali, polisi, vyama visivyo vya kiserikali na wadau wengine wa ndani na nje.
Tayari Jeshi la Polisi linamshikilia kinara aliyekuwa akisambaza karatasi za kuchochea vurugu hizo

Saturday, 25 May 2013

Tapeli aponea CHUPU CHUPU kuchomwa moto




                         picha alizokutwa nazo tapeli huyo.                     
                         Baadhi ya vitambulisho alivyokutwa navyo tapeli huyo          
KWA muda mrefu Ijumaa limekuwa likipokea malalamiko kuhusu uwepo wa jamaa anayedaiwa ni tapeli maarufu Dar kisha kuingia mzigoni na kumnasa ‘laivu’ ambapo alihenyeshwa kwa kibano cha karne na raia waliokuwa na hasira.
Mtego huo ulifyatuka Jumanne ya Mei 21, mwaka huu ambapo kijana mmoja (jina halikupatikana) alinaswa na kupewa ‘henyahenya’ ya aina yake huku akinusurika kuchomwa moto.
Bila kujua kuna mtego, kijana huyo aliingia kwa mbwembwe katika Ukumbi wa Mango Garden, Kinondoni jijini Dar na kukaa katika moja ya viti kisha kuita mhudumu na kuchomoa noti ya shilingi ‘buku’ kumi, akaagiza misosi.
Akiwa amemeza tonge moja tu, aligeuka akatazama mlangoni, akamuona jamaa mmoja akimfuata kwa mwendo wa kasi na katika hali ya taharuki, ndipo akakurupuka akitaka kutoka nduki.
ILIKUWAJE?
Majira ya saa 9:00 alasiri, ghafla kijana huyo aliibua tafrani alipokurupuka mbio kutoka nje ya ukumbi huo. 
Nyuma ya kijana huyo, jamaa aliyekuwa amedaiwa kutapeliwa na mtu huyo alianza kumkimbiza akipiga kelele za mwizi ndipo baadhi ya raia nao wakaanza kumfukuzia.
ATIWA MIKONONI
Raia hao walitimua mbio wakimfukuza kijana huyo na  walipofika maeneo ya Vijana, Kinondoni, kwa bahati mbaya alijikwaa na kuanguka ndipo akatiwa mikononi.
Yule jamaa ambaye alikuwa anamwitia mwizi, alikuja mbio na kuwaambia watu kuwa huyo ni tapeli ambaye alimtapeli shilingi laki tatu na nusu baada ya kumsomesha kuwa yeye ni mwajiri wa kampuni moja.
Aliyetapeliwa alidai kuwa katika utapeli huo, kijana huyo huwa anashirikiana na mzee mmoja ambaye huwa anavaa nguo nadhifu huku akiwa anatembea na  ‘briefcase’ mkononi.
‘ASACHIWA’
Jamaa huyo ‘aliposachiwa’ alikutwa na vitu kibao vya kitapeli yakiwemo makaratasi yaliyokatwa na kufungwa kwa noti bandia za shilingi elfu kumi zinazoonekana kama burungutu la fedha kumbe hakuna chochote ni ‘bosheni’.
Pia alikutwa na vitambulisho kibao vya watu vikiwemo vya kupigia kura, leseni na picha za ‘passport size’ za watu mbalimbali.
Katika makabrasha yake kulikutwa barua mbalimbali za serikali za mitaa za jijini Dar.
Alipoulizwa kuwa vitu hivyo vya watu na nyaraka za serikali ni vya nini au alivipataje, jamaa huyo alijitetea kuwa ana mtu anayeshirikiana naye katika michongo hiyo.
APEWA KIBANO CHA KARNE
Baadaye wananchi wenye hasira kali walichukua sheria mkononi na kumpa kibano huku akitakiwa kumpigia simu bosi wake aje eneo hilo.
Zoezi la kuja kwa bosi wake lilishindikana baada ya kupigiwa simu na kumkana hivyo baadhi ya watu walimvisha tairi la gari wakamwagia mafuta ya petrol, tayari kwa kumchoma moto.
Huku akiwa amehenyeshwa kwa kipigo na kulowa damu chapachapa, wakitaka kumchoma moto, madereva teksi wa eneo la Vijana, Kinondoni waliwakataza wasimchomee maeneo hayo kwani hawakutaka ushahidi hivyo wakamwachia akiwa nyang’anyang’a.
chanzo:globalpublishers

Friday, 24 May 2013

Majambazi yatikisa Dar

WATU wanaoaminika kuwa ni majambazi ambao idadi yao haijafahamika, wamepora sh milioni 46, huku polisi wakishuhudia bila kutoa upinzani kukabiliana nao.
Fedha zilizoporwa ni mali ya mfanyabiashara wa bia za jumla jijini Dar es Salaam, Ivon Urio, wa wilayani Temeke.
Wakati majambazi wa Temeke wakipora kiasi hicho bila upinzani, tukio lingine la ujambazi limetokea jana asubuhi katika mtaa wa Sayansi na Kijitonyama wilayani Kinondoni ambapo walipora sh milioni 40, majira ya saa nne asubuhi.
Katika tukio la ujambazi la Temeke ambalo linadaiwa kuwa la nane kwa mwezi huu, lilitokea juzi kati ya saa nne na tano asubuhi katika eneo la Mbagala Rangi Tatu, wakati mfanyabiashara huyo akijiandaa kupeleka fedha hizo benki.
Kwa mujibu wa watu walioshuhudia tukio hilo kabla ya majambazi hao kupora fedha hizo, polisi wanaokadiriwa kufikia 10, walifika eneo hilo wakiwa wanalifuatilia gari lililokuwa linashusha mafuta ya kula katika moja ya maduka yaliyo jirani na eneo palipotokea wizi huo.

Slaa: Simchukii JK kwa dini yake,bali utendaji kazi wake

Babati. Katibu Mkuu wa Chadema,Dk Willbroad Slaa amedai kuwa anachukia udhaifu wa utendaji kazi wa Rais Jakaya Kikwete,kama kiongozi mkuu wa nchi na katu hamchuki kutokana na dini yake kama watu wengine wavyopotosha.
Dk Slaa aliyasema hayo jana kwenye maeneo ya Riroda, Galapo,Mwada,Magara,Magugu,Mutuka,Sendo na Mamire,wilayani Babati,mkoani Manyara na kudai kuwa hatanyamaza kamwe kwa kuwa wananchi hawatendewi haki na matumaini yao yanaminywa na watawala.
Alisema hatamung’unya maneno wala kusita kuendelea kusema udhaifu wa Rais Kikwete hasa katika kushindwa kuchukua au kufanya uamuzi sahihi na kwa wakati sahihi kwa sababu matokeo yake yanaathiri Watanzania wote ambao yeye pamoja na chama chake wamejitolea kuwa wasemaji wao.
“Nchi hii inavunjwa,napambana na Kikwete kwa sababu ni dhaifu,” alisema na kuongeza:
“Kuna watu wanapotosha jambo hili,mimi sina chuki na Rais Kikwete kwa sababu ya dini yake”. alisema.
chanzo:mwananchi

Kipanya naeeee


Laana ya gesi MTWARA

UGUNDUZI wa gesi asilia mkoani Mtwara umegeuka laana kwa wakazi wake wanaoishi maisha ya wasiwasi hivi sasa.
Sauti za milio ya mabomu, risasi, na vipigo ndivyo vinavyonekana kushamiri zaidi kwenye mji huo uliosifika kwa amani na utulivu kwa muda mrefu.
Tanzania Daima lilishuhudia idadi kubwa ya askari polisi na wanajeshi wakiwa kwenye pikipiki na magari wakizunguka maeneo mbalimbali kwa lengo la kudhibiti vurugu.
Wakati hali ikizidi kuwa tete mkoani humo, jana polisi wanadaiwa kumuua kwa kumpiga risasi mjamzito aliyekuwa nyumbani kwake eneo la Magomeni.
Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Ligula, Mohamedi Kodi amethibitisha kupokea mwili wa mjamzito huyo ukiwa na tundu tumboni, na hivyo kufanya idadi ya maiti zilizopokelewa hospitalini hapo kufikia mbili na majeruhi 18.
“Ni kweli kwa leo tumepokea maiti moja ya mwanamke ambaye ni mjamzito wa miezi saba, amepigwa risasi tumboni.
“Pia tumepokea mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Chuno, amevunjwa miguu yote kwa risasi,” alisema Dk. Ligula.

VIDEO:Idadi ya watu waliokufa kwenye vurugu Mtwara

Waliomwagia tindikali sheha wa shehia ya Tomondo wachukuliwe hatua..

SIKILIZA WIMBO:Juma Nature - Haipotei.(Official Video)

Yule mtoto aliyecharangwa mapanga na baba yake afariki



                                          Devotha Gerald enzi ya uhai wake 
                                                Mama yake marehemu devotha
YULE mtoto wa miaka minne, Devotha Gerald aliyecharangwa mapanga kikatili na baba yake mzazi na kukimbizwa Hospitali ya Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga kwa matibabu, ameaga dunia.
Samson Bwire mkazi wa Kitongoji cha Sango, Kata ya Nyasubi, Wilayani Kahama mkoani hapa ndiye baba mzazi anayedaiwa kutenda unyama huo uliopitiliza.
Uhai wa Devotha ulikatika Mei 16, mwaka huu saa nne usiku akiwa amezungukwa na jopo la madaktari waliokuwa wakiupigania uhai wake.
Habari za kitabibu kutoka hospitalini hapo zinasema binti huyo aliaga dunia kutokana na kutokwa damu nyingi ambapo pia mapanga aliyokatwa yalizama kichwani.
Baadhi ya madaktari waliokuwa wakimtibu walitokwa machozi wakati mtoto huyo akikata roho. 
Mei 16, mwaka huu, majira ya jioni, Bwire ambaye ni polisi mstaafu alidaiwa kumcharanga mapanga mtoto wake huyo kisa kikidaiwa ni ugomvi uliotokana na wivu wa kimapenzi kati yake na mkewe, Happiness Elias (28).
Kwa mujibu wa mashuhuda, Bwire anadaiwa kufanya tukio hilo akiwa amelewa chakari. 
Habari zinadai kuwa, katika ugomvi huo, mwanaume huyo alikuwa akimtuhumu mkewe kumsaliti. Hata hivyo, mkewe alifanikiwa kukimbia kusikojulikana.
Baada ya mkewe kukimbia ndipo baba mzazi huyo akamgeuzia kibao mwanaye na kumkata mapanga kumaliza hasira zake.
Majirani walivunja mlango, wengine walipiga simu polisi ambao walifika na kumkamata mtuhumiwa.
Hata hivyo, Bwire hakuachwa salama kwani majirani hao wakiwa na hasira walimpiga sana.
Wakati mtuhumiwa akipelekwa polisi aliruka kutoka garini na kuangukia uso kitendo kilichomsababishia majeraha makubwa usoni.
Marehemu Devotha alizikwa Mei 17, mwaka huu mjini Shinyanga. Mama wa marehemu akizungumza kwa uchungu alisema: Maskini mwanangu amekufa kifo kibaya sana, wala hakuwa na hatia yoyote, naumia sana moyoni mwangu.
“Madaktari walipambana kuokoa uhai wake lakini Mungu akasema mwancheni aje kupumzika.”
chanzo:globalpublishers.

Thursday, 23 May 2013

Kikwete atoa msimamo mkali kuhusu vurugu za MTWARA

Dar es Salaam. Rais Jakaya Kikwete amekemea vikali vurugu zilizotokea jana mkoani Mtwara baada ya kusomwa bungeni kwa Bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini.
Akizungumza katika eneo la Kizota, Dodoma wakati wa kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Barabara ya Dodoma kwenda Iringa, Rais Kikwete alisema wote waliohusika na vurugu hizo watasakwa na kuchukuliwa hatua kali.
Rais Kikwete alisema rasilimali inayopatikana mahali popote pale nchini inatakiwa kutumiwa na Watanzania wote... “Hivi watu wa Nyarugusu wadai dhahabu ya pale au kinachopatikana Chalinze basi kisitumiwe na watu wa Morogoro! Hivi tutakuwa na taifa kweli?,” alihoji kwa ukali Rais Kikwete.
Rais Kikwete alisisitiza kuwa Serikali itawasaka wale wote wanaoongoza vurugu hizo na watawajibishwa kwa makosa hayo... “Tutawasaka hawa watu na viongozi wao hata kama wana mapembe kiasi gani, tutayakata.”
Alichosema Waziri Muhongo
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo amesema mradi wa kusafirisha gesi kutoka mkoani Mtwara kwenda Dar es Salaam, umeanza kwa kasi na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda atakwenda huko wiki ijayo kuweka jiwe la msingi.
Akiwasilisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini jana, Waziri Muhongo alisema:
“Mradi wa kujenga bomba la gesi uko palepale na unaendelea kwa kasi na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ataenda kuweka jiwe la msingi wiki lijalo.”
“Tumezungumza mengi kuhusu suala hilo na hata viongozi wa watu wa Mtwara walipelekwa nje kujifunza faida zake, lakini hata kama hawajaelewa, nimetoa kijitabu kinachozungumzia faida mbalimbali watakazopata wana Mtwara katika mradi huo.”

Polisi lamshikilia askari wake kwa kutorosha mtuhumiwa

Jeshi la Polisi Mkoani Arusha linamshikilia Ofisa wa jeshi hilo, Inspekta Isaack Manoni kwa tuhuma za kumtorosha mtuhumiwa wa usafirishaji magunia ya bangi,Koplo Edward, ambaye alikuwa dereva wa gari la Polisi lenye magunia hayo, namba za usajili T. 2025 Toyota Land Cruser.

Akizungumzia tukio hilo jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas, alisema katika sakata la usafishaji bangi kwenda mpaka wa Holili, watuhumiwa walikuwa wawili na askari mwenye namba G.2434 PC George, ambao wote wamefukuzwa kazi mara moja.

Alisema watuhumiwa hao walipelekwa kwenye nyumba zao, kwa upekuzi ndipo walipokuwa nyumbani kwa mtuhumiwa huyo alikimbia na kutokomea kusikojulikana.

“Wakati wakiwa katika nyumba ya mtuhumiwa huyu, kulikuwa na askari saba, akiwamo Inspekta Isaack ambaye alikuwa kiongozi, hivyo baada ya tukio lazima tumshikilie huyu kwa uzembe kazini,” alisema.

Alisema baada ya jeshi hilo kumaliza mahojiano na ofisa huyo, hatua za kinidhamu zitachukuliwa dhidi yake.

Aidha, mtuhumiwa mmoja PC. George, mwenye namba za usajili G.2434 amefikishwa Mahakamani, Mkoani Kilimanjaro.

Awali watuhumiwa hao walikamatwa Mei 18 mwaka huu, majira ya saa 5 usiku, huko Himo na askari Polisi wa Kilimanjaro, wakiwa na gari la Polisi lenye namba za usajili T.2025 Toyota landa Cruser lililokuwa likiendeshwa na Koplo Edward, huku likiwa na magunia 18 ya bangi,yakipelekwa Holili mpakani Kenya.
chanzo:nipashe

Tz All Female Stars- Kidole Kimoja (FISTULA) (Official Video)

Vurugu zaibuka mkoani Mtwara baada ya bajeti ya wizara ya nishati na mad...

Wednesday, 22 May 2013

MWAKIFWAMBA: WANAOVAA VIMINI KWENYE FILAMU WANAJIUZA

RAIS wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF) Simon Mwakifwamba amesema wasanii wanaovaa mavazi yasiyo na staha ikiwemo vimini kwenye sinema wanajiuza.

Mwakifwamba aliyasema hayo katika mahojiano na kituo kimoja cha runinga, jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita, akiwa ameongozana na msanii Riyama Ally.
Kauli hiyo ya Mwakifwamba imekuja siku chache baada ya sakata la uvaaji vimini na udhalilishaji wanawake na wototo kwenye filamu kuzungumziwa bungeni, Dodoma.
APIGIA MSUMARI
“Hili suala nimeshalikemea kwa muda mrefu sana... naamini kama ni watu wa kuelewa watakuwa wameelewa na wale ambao wanaendelea na hayo mambo maana yake ujue wana mambo yao.
“Siyo wote wanaoingia kwenye filamu ni wasanii wa kweli, wengine wanatumia tasnia hii kutafuta mabwana ndiyo maana wanavaa mavazi ya ajabu ili waonekane, jambo ambalo tunalikemea kila wakati.
“Sikatai wakati mwingine kuna ‘scene’ zitahitaji uhusika fulani kama uchangudoa lakini utakuta msanii anatakiwa kuvaa uhusika wa ofisini, yeye anavaa vinguo vya hovyo, maana yake ni nini kama si kutafuta soko?” alisema Mwakifwamba na kuongeza:
“Imefika wakati wasanii wanatakiwa wabadilike kwani hali ilipofikia siyo pazuri. Bado msanii anaweza kuonekana ana kiwango kizuri bila kuvaa nguo zinazomdhalilisha na kumtafsiri vibaya mbele ya jamii.”
Akasema: “Sasa nasema hivi, yeyote atakayekiuka utaratibu tuliokubaliana tutamchukulia hatua. Hatutamfumbia macho. Tunahitaji kuwa na tasnia yenye heshima.”

RIYAMA SASA
Mkali wa kucheza na hisia, Riyama naye alitoa maoni yake kuhusu mavazi na mwenendo mzima wa filamu za Kibongo ambapo kwa upande wake alisema anaamini wanaofanya hivyo wanatafuta kuwa mastaa kwa njia ya mkato.
“Tatizo ni ulimbukeni wa kuiga wasanii wa nje. Wasanii tunakiwa kujitambua na kufahamu na kulinda utamaduni wetu. Wasanii wengi hawajui thamani zao, jamani ustaa siyo kukaa uchi.
“Tujue kuwa kwenye filamu siyo sehemu ya kutafutia mabwana. Kuonesha urembo wetu wa nje na wa ndani kwenye hadhara siyo kitu kizuri kwa utamaduni wetu... hao wanaofanya hivyo wanasababisha wasanii wote tuonekane machangudoa,” alisema Riyama.
chanzo:.globalpublishers

Gesi Mtwara: Vipeperushi vyapingana

Hali ya wasiwasi imeendelea kuwakumba wakazi wa mkoa wa Mtwara kufuatia watu wasiojulikana kuendelea kusambaza vipeperushi vya uchochezi wakishinikiza gesi isisafirishwe kwa bomba kwenda jijini Dar es Salaam, lakini wengine wakipinga ilani ya kusitisha biashara zao leo.

Moja ya kundi hilo limetuma ujumbe mfupi wa maneno kwa wananchi wa mikoa hiyo ukiwataka wasitishe shughuli zao wapate fursa ya kusikiliza hotuba ya bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini inayowasilishwa leo bungeni mjini Dodoma itakayowasilishwa leo.

Hii ni mara ya pili kusambazwa kwa vipeperushi hivyo. Mara ya kwanza ilikuwa Alhamisi wiki  iliyopita.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, Linus Sinzumwa, amethibitisha kusambazwa kwa vipeperushi na ujumbe mfupi wa maneo katika simu za mikononi vilivyoonekana katika maeneo kadhaa ya Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara Mikindani vikiwa na ujumbe mbalimbali.

Ujumbe mfupi uliotumwa katika simu za mikononi unaeleza kuwa “Hii ni kwa wakazi wote wanaoishi mikoa ya kusini… kuanzia vijiji na wilaya zote… tunakumbushana kuwa siku ya Jumatano tarehe 22,05,2013 kuanzi saa 3:00 asubuhi tusikilize bunge la bajeti juu ya uwasilishaji wa bajeti ya Nishati na Madini ili tujue hatima yetu wana-kusini juu ya gesi yetu.” 

Umezidi kueleza kuwa: “Kama kawaida yetu siku hiyo hakutakuwa na kazi yoyote, huduma zote za kijamii zisitishwe kuanzia bodaboda, daladala hata gari za mikoani na….(onyo ukikutwa umekiuka agizo la wana-kusini kazi kwako)…tuma ujumbe huu kwa wana-kusini wote…gesi haitoki hata kwa bomba la peni.” 

Hata hivyo, kundi la watu wengine wasiofahamika lilisambaza vipeperushi vya kupinga uchochezi huo ambavyo vilikuwa na ujumbe mbalimbali.

“Wana-kusini tusiwe wajinga tuamke, kweli gesi yetu ni mali yetu wote wana-kusini. Kama ni kunyanyasika serikali ya nchi yetu ilitutupa kabisa. Tarehe 17.05.2013 tuliungana kufunga maduka na biashara zote wala Shilingi hatukupata hata chakula. Je? sasa Jumatano tena tusifanye biashara. Tuacheni ujinga, wana-kusini wenzetu wengine hata kazi hawana, gesi itazidi kutufanya tuwe maskini.

Kipanya naeeeeeeeee


Spika wa bunge amekataa kutengua baadhi ya kanuni za bunge.

SIMANZIII:Aliyemuua baba yake kwa risasi siku ya HARUSI




SAKATA la kijana Bonny Fabian Kavishe kudaiwa kumuua kwa kumpiga risasi baba yake, mzee Livingstone Kavishe akiamini ni mwizi sasa ni simulizi ya machozi kufuatia kusomwa kwa waraka mzito ulioandikwa na mtuhumiwa huyo ambaye bado yupo mahabusu ya Polisi Mlandizi, Bagamoyo, Pwani

Waraka huo ulizidi kuwatoa machozi baadhi ya waombolezaji siku ya mazishi yaliyofanyika Marangu, Wilaya ya Moshi Vijijini, Mkoa wa Kilimanjaro kutokana na maneno yenye huruma ya Bonny kuomba msamaha.
WARAKA ULIANDIKIWA NDANI YA MAHABUSU
Habari zisizo na chenga wala kumulika tochi zinasema, mtuhumiwa akiwa mahabusu aliamua kuandika waraka huo na kumpa ndugu yake mmoja (jina halikupatikana) akimpa maelekezo kwamba usomwe siku ya mazishi ya mzee huyo kabla hajafukiwa kaburini kwa vile yeye hatakuwepo.
“Kwa kweli inauma sana! Jamaa alipoona hatapata ruhusa ya askari ili akashiriki mazishi ya baba yake aliomba karatasi na kalamu na kuandika waraka, akampa ndugu yake mmoja, akamwambia usomwe siku ya mazishi ya marehemu kabla hajafukiwa kaburini,” kilisema chanzo.
MWILI WAAGWA NYUMBANI KWA MTUHUMIWA, WASAFIRISHWA NA WARAKA
Jumatano ya Mei 15, mwaka huu, mwili wa marehemu mzee Kavishe uliagwa nyumbani kwa mtuhumiwa licha ya yeye kutokuwepo na ukasafirishwa kwenda Marangu kwa mazishi.
Miongoni mwa mambo yaliyozingatiwa kwenye kusafirisha mwili huo ni uwepo wa waraka huo ambao mtuhumiwa aliomba usomwe mbele ya waombolezaji siku ya mazishi.
MANENO NDANI WARAKA NI HAYA
Siku ya mazishi, mwanaume aliyepewa jukumu la kuongea kwa niaba ya familia aliusoma waraka huo huku waombolezaji wakiwa makini kumsikiliza.
Alisema waraka huo umeandikwa kwa mikono ya Bonny Kavishe, licha ya kuzungumzia mambo mengine, aliwaomba msamaha ndugu, jamaa na marafiki kwamba wamsamehe kwa kitendo cha kumuua baba yake.
Alisema alifanya kitendo hicho bila kukusudia na wala hajui nini kiliendelea. Haikuwa nia yake kumtoa uhai baba yake aliyefikia nyumbani kwake Mlandizi kwa ajili ya kusherehekea harusi ya mdogo wa mtuhumiwa huyo iliyofanyika Mei 11, mwaka huu.

Sakata la Jaydee, Clouds latua bungeni


MSEMAJI wa kambi rasmi ya upinzani, Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ (CHADEMA), amefikisha rasmi bungeni mgogoro kati ya mwanamuziki maarufu Judith Wambura ‘Lady Jaydee’ na wamiliki wa Clouds Media.
Akiwasilisha maoni ya kambi hiyo bungeni jana, Sugu alisema kuwa mgogoro huo umesababisha kutopigwa nyimbo za Bongo fleva kwa siku nzima.
Sugu alisema kuwa kwa sasa watu wachache wenye fedha wamewageuza wasanii kuwa ni sehemu ya mtaji wao, kwa kutumia sanaa zao kujitajirisha.
“Sanaa inaendelea kufanywa mtaji wa biashara wa watu wachache ambao wanatumia nguvu waliyonayo katika jamii na uwezo wao wa kifedha, katika kukandamiza maslahi ya wasanii hapa nchini,” alisema Sugu.

Tuesday, 21 May 2013

Joseph Mbilinyi: Serikali inanyonya wasanii


Kambi ya Upinzani bungeni imeilaumu serikali kwa kushindwa kusimamia sheria inayoviagiza vyombo vya utangazaji nchini kuwalipa wanamuziki kutokana na matumizi ya nyimbo zao.
Akisoma hotuba kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Habari,Utamaduni na Michezo bungeni mjini Dodoma jana, Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani, Joseph Mbilinyi (Sugu) alisema, ni aibu serikali kushindwa kuvidhibiti vyombo vya utangazaji ambavyo vimeendelea kuwanyonya wanamuziki kwa kutumia nyimbo zao pasipo kuwalipa hata senti moja.
“Leo hii wasanii wanalazimishwa kuandika barua kuwa wametoa nyimbo zao kwa vyombo hivyo zipigwe bila kulipia na kutokana na mazingira yaliyotengenezwa, wanamuziki wanajikuta ni lazima wahonge! ili nyimbo zao zipigwe ili waweze kupata soko la kazi zao,”.alisema Mbilinyi.

KIPANYA NAEEEEE


VIDEO:Spika wa Bunge aliahilisha bunge kwa dharura kujadili hotuba ya kambi ya upinzani.

VIDEO:Mchungaji Peter Msigwa na watuhumiwa wengine 75 wafikishwa mahakamani.

POLISI AMCHARANGA MAPANGA MWANAYE KISA MAPENZI



KATI ya stori za mwaka zinazosikitisha, hii ni mojawapo! Polisi mstaafu, mkazi wa Kitongoji cha Sango, Kata ya Nyasubi wilayani Kahama mkoani hapa, Samson Bwire (54), anashikiliwa na jeshi la polisi kwa kumcharanga mapanga binti yake, Devotha Gerald (4), kisa kikidaiwa ni wivu wa kimapenzi.
Tukio hilo lilitokea Mei 16, mwaka huu, majira ya jioni nyumbani kwa Bwire alipokuwa akigombana na mke wake, Happiness Elias (28).
Kwa mujibu wa mashuhuda, baba Devotha anadaiwa kufanya tukio hilo huku akiwa amelewa tilalila.
Habari zilidai kuwa, mwanaume huyo alikuwa kwenye ugomvi wa kimapenzi na mkewe ambapo katika purukushani akimtuhumu mama Devotha kumsaliti, mkewe huyo alifanikiwa kuchoropoka.
Ilidaiwa kuwa baada ya mama Devotha kuchoropoka ndipo baba huyo akamgeuzia kibao Devotha na kumalizia hasira zake kwa kuanza kumkatakata kwa panga bila huruma.
Kwa mujibu wa majirani, kelele zilisikika kutoka kwenye familia hiyo na kwamba walipokwenda walimkuta baba Devotha akichoma nguo za mkewe na alipowaona, aliingia ndani na kuanza kumkata mapanga mtoto huyo huku akiwa amefunga mlango.
Ilifafanuliwa kwamba baada ya kusikia kelele za mtoto, majirani walianza kuvunja mlango huku wakiomba msaada kutoka kwa polisi na baada ya polisi kufika walifanikiwa kumnusuru mtoto akiwa amejeruhiwa vibaya.
Kufuatia hali mbaya ya mtoto aliyekuwa amelowa damu kichwani, majirani walishindwa kuzuia hasira zao na ndipo walipoanza kumpiga Bwire ambaye ni askari polisi mstaafu wa cheo cha koplo.
Katika hali kama hiyo, ilibidi polisi wafanye kazi ya ziada kumnusuru baba Devotha na kumpakia kwenye gari kwenda kituoni.
Hata hivyo, wakati gari la polisi likiwa katika mwendo wa kasi eneo la Soko la Mkulima, baba Devotha aliruka kutoka kwenye gari na kuangukia lami, kitendo kilichomsababishia majeraha makubwa sehemu za usoni.
Mtoto Devotha na baba yake, wote walikimbizwa na kulazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Kahama kwa matibabu huku Bwire akiwa chini ya ulinzi mkali wa polisi ikiwa ni pamoja na kufungwa pingu.
chanzo:globalpublishers

Monday, 20 May 2013

Nine in ten parents want online porn automatically blocked by the Government



Parents overwhelmingly support calls for the Government to impose an automatic block on online pornography, headteachers have revealed.
The National Association of Headteachers (NAHT) found nine out of ten parents want a default setting on computers and smartphones which prevents the viewing of adult material.
The dramatic survey figures reveal 90 per cent of parents wanted the default block on porn sites. 
Two-fifths are so worried about the ease with which it can be found – often by mistake – that they want children as young as five to have guidance in classes
Half thought advice should be given to children once they reach the age of 13.
Only 7 per cent thought it was never appropriate to discuss the issue in class.
And just one in eight parents felt they were able to sufficiently educate their children about the dangers of what they can find online without the help of teachers and support from schools.

Mawaziri watatu kung’olewa


UPEPO mbaya ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) unazidi kuvuma, safari hii wabunge wake wakimtaka Rais Jakaya Kikwete kuwafukuza kazi mawaziri watatu.
Mawaziri wanaotakiwa kung’olewa ni Dk. Shukuru Kawambwa (Elimu na Mafunzo ya Ufundi), Dk. Mathayo David Mathayo (Mifugo na Maendeleo ya Uvuvi) na Dk. Fenella Mukangara (Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo).
Kama Rais Kikwete atakubali kuwaondoa madarakani mawaziri hao, hii itakuwa mara ya pili kwake kufanya hivyo. Mara ya kwanza ilikuwa Mei mwaka jana.
Mwaka jana Rais Kikwete aliamua kuwaengua madarakani baadhi ya mawaziri waliokuwa wakiandamwa kwa tuhuma mbalimbali, ikiwemo uwajibikaji mbovu.
Miongoni mwa walioenguliwa mwaka jana ni Dk. Haji Mponda aliyekuwa Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Mustafa Mkulo (Waziri wa Fedha), William Ngeleja (Nishati na Madini na Ezekiel Maige (Maliasili na Utalii).
Msimamo huo wa wabunge wameutoa jana katika kikao baina yao na Rais Kikwete kilichokuwa kikitathimini mwenendo wa chama na utendaji wa wabunge.
Chanzo chetu ndani ya kikao hicho kilieleza kuwa baada ya Rais Kikwete kutoa hotuba ya ufunguzi, baadhi ya wabunge walianza kuchangia, huku wengine wakishutumiana kwa kuvujisha siri za vikao nje kwa waandishi wa habari.
Wabunge hao walidai kuwa mawaziri hao watatu wamekuwa mzigo kwa Serikali ya CCM kutokana na utendaji wao kutokuwa wa kuridhisha.
Walisema matunda ya uwepo wa mawaziri hao kwenye wizara husika hayaonekeni, hivyo kumtaka Rais Kikwete awang’oe.
Waziri Kawambwa analaumiwa kwa kuzembea kwenye sekta ya elimu ambayo inazidi kushuka kiasi cha kuifanya serikali ifute matokeo ya kidato cha nne ya mwaka jana.

SIKILIZA SONGI JIPYA LA: shilole - paka la bar

Polisi wakamatwa na bangi gunia 18


SIKU chache baada ya Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam kuwakamata askari 16 wakituhumiwa kujihusisha na biashara ya magendo, askari wengine wawili wa jeshi hilo wamekamatwa mkoani Kilimanjaro wakiwa na shehena kubwa ya bangi wakiisafrisha kwenda nchini Kenya.
Askari hao walikamatwa Mei 19 mwaka huu saa nne usiku eneo la Kilemapofu, Wilaya ya Moshi Vijijini wakiwa na magunia 18 ya bangi ambayo walikuwa wameyapakia kwenye gari la Mkuu wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) mkoani Arusha aina ya Toyota Land Cruiser lenye namba PT 2025.
Akithibitisha kukamatwa kwa askari hao, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Robert Boaz alisema askari hao walikuwa wakipeleka bangi hiyo Wilaya ya Rombo kwa mfanyabiashra mmoja ambaye hakutaka kumtaja jina lake.
Kamanda Boaz aliwataja askari waliokamatwa na wanashikiliwa kwenye kituo kikuu cha polisi katika mji mdogo wa Himo kuwa ni F.1734 Koplo Edward (dereva) wa kikosi cha kutuliza ghasia (FFU) mkoani Arusha na G.2434 Konstebo George wa kituo cha polisi Ngarenanyuki Wilaya ya Arumeru.
Alibainisha kuwa kukamatwa kwa askari hao kunatokana na operesheni ya kukabiliana na dawa za kulevya inayofanywa na polisi katika mikoa ya Arusha na Kilimanjaro.
Alisema operesheni hiyo imefanyika kikamilifu katika Mkoa wa Arusha uliokuwa ukitumika kupitishia bidhaa hiyo, na sasa wahusika wameamua kuutumia Mkoa wa Kilimanjaro.
“Baada ya kuwahoji askari wale, walidai kuwa walikodishwa na mfanyabiashara huyo kuipeleka bangi hiyo wilayani Rombo tayari kwa kusafirishwa kwenda nchini Kenya ambako inaaminika kuna soko kubwa,” alisema.

Kibanda kuliteka Bunge leo


TUKIO la kutekwa na kuumizwa vibaya kwa Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri nchini (TEF), Absalom Kibanda linatarajia kuteka mjadala wa Bunge leo.
Jambo hilo linatarajiwa wakati wa kujadili hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kwa mwaka 2013/2014 itakayowasilishwa bungeni leo.
Kibanda ambaye pia ni Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya New Habari (2006), alivamiwa na watu wasiojulikana usiku wa Machi 6 mwaka huu, nyumbani kwake Mbezi Juu jijini Dar es Salaam.
Mhariri huyo akiwa getini kwake akisubiri kufunguliwa, akapigwa kwa nondo kichwani, kutobolewa jicho la kushoto, kukatwa kidole, kung’olewa kucha na meno mawili.

Mulongo: Arusha ipo nyuma matumizi ya vyoo

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo, amekerwa na tabia ya baadhi ya wananchi mkoani hapa kutokutumia vyoo na badala yake wanajisaidia holela na kuchafua mazingira.

Amesema mkoa huu ni miongoni mwa mikoa ambayo bado iko nyuma katika matumizi ya vyoo.

Amesema uchafuzi unaofanywa wa kujisaidia hovyo unaharatisha afya za watu kwa kuambukizwa maradhi ya milipuko.

Alisema hayo mwishoni mwa wiki katika hotuba yake iliyosomwa na Mkuu wa Wilaya ya Monduli, Jowika Kasunga, wakati wa ufunguzi wa semina elekezi ya viongozi wa mkoa kuhusu utekelezaji wa kampeni ya kitaifa ya usafi wa mazingira ya miaka minne ambayo inafanywa mashuleni na kwenye kaya.

Alisema lengo la kitaifa linaitaka mikoa iwe na matumizi ya vyoo katika mashule na kaya na kwamba mkoa huo unafanya uhamasishaji wa kutekeleza malengo hayo kutoka asilimia 12 hadi kufikia asilimia 53 ifikapo mwaka 2015.

Saturday, 18 May 2013

Huu ndio WARAKA wa Vinega “AntiVirus” kuhusu Ruge na Kusaga dhidi ya JayDee

Ni wazi na dhahiri kabisa kesi iliofunguliwa mahakamani dhidi ya Lady JayDee haina maana yoyote isipokuwa ni hofu ya mafisadi wa muziki nchini (Kusaga na Ruge) kwa kuwa waraka wa piliulikuwa utoke tar 15 may na mwingine tar 17 may mwaka huu wa 2013.
Hapa la kujiuliza ni juu ya interview ya Rugen a kinachoendelea sasa,eti suala limefika mahakamani,kweli Kusaga na Ruge mmeweza kuthibitisha nyie ni mafisadi na mnamuaibisha Rais Kikwete ambaye nina uhakika anajua kuwa nyie ndio kikwazo kikubwa na hata Bungeni alishawahi kuzungumza kuwa alitoa studio na pango kumbe tatizo sio hilo,tujiulize wote kuna nini wanachoficha hadi kumtafutia kesi raia mwema asie na hatia?
Tena anaejitafutia rizki ambayo wao wanapigana nayo kwa kumkandamiza?
Huku wakitumia mabavu wakilindwa na baadhi ya viongozi wa serikali na waandishi ambao majina yao mtayapata kupitia nyaraka zinazokuja (zipo 88) na huu ndio wa kwanza.
Nimesikitika sana na njia pekee ya kuufahamisha umma juu ya ufisadi huu wa Ruge Mutahaba na Joseph Kusaga ni kuyaanika yote ambayo jamii na Viongozi wa Serikali kama mlikuwa hamjui sasa ndio wakati muafaka wa kuwajua watu hawa ambao kila kukicha ni kuimarisha ufisadi wao na kujipendekeza kwa Viongozi sambamba na watoto wao (mtajua mpaka majina yao)

Naanza kupatwa na wasiwasi nikijiuliza, endapo Lady JD angekuwa amegombana na msanii mwenzake mkubwa kama Prof Jay, Ray C au Juma Nature wanasiasa wangeingilia kati? Ni wazi wasingesogea kwa kuwa hakuna maslahi zaidi ya kuingilia mgogoro huu ambao hawataki jamii ijue maovu yao.

Napatwa mashaka jinsi wanasiasa wanavyolivalia njunga jambo binafsi
Kama hili na kulifanya ni la kiserikali basi tafuteni chanzo cha tatizo mjue ni sehemu gani sahihi ya kuanza kutatua kilichopo na sio kukimbilia kuunda vikao ambavyo naamini vimeshaitishwa vingi sana lakini hakuna kilichosaidia.
Wanasiasa badala ya kutafuta sababu zinazofanya wasanii wanalalamika mnakimbilia kutatua mgogoro wa Ruge na JD ili kusuluhisha mambo yasiendelee kuongelewa jamii ijue uovu wa mafisadi hawa.
Haitasaidia kwa sababu wanaojua maovu ya hawa mafisadi Rugen na Kusaga ni wasanii wengi wakubwa na watu wengine binafsi (kumbukeni waraka zipo 88)

Vijana mnaowategemea katika kampeni zenu na mnawaita Taifa la kesho, lakini mnakubali waendelee kukandamizwa na kunyanyasika huku wakizidi kuwaneemesha kina Ruge na Kusaga.
Tatizo mnalijua kaeni na wasanii wote wawaelezee matatizo yao, msikae na wasanii ambao wanaamrishwa na kina Ruge. Sikilizeni kilio cha wasanii wengine pia na itafutwe njia ya kupata maoni ya kila mmoja na kuachana na watu wengine ambao wanaendesha mtandao wa ufisadi chini ya kivuli cha Ruge (Said Fella na Babu Tale) ambao mtapata kujua kila kitu kuhusu ufisadi wao na kinachoendelea (kumbuka waraka zipo 88)

Ruge Mutahaba amekuwa ni tatizo na janga la Kitaifa katika tasnia ya muziki kwa ujumla, amekuwa akiwagawa wasanii kwa kutumia redio Clouds kwa vitisho vya kutopigiwa nyimbo, au kwa danganyio la kufanyiwa promotion mpaka kwenye magazeti endapo tu utakuwa chini ya bawa lake.
Wasanii wamekuwa hawalipwi vizuri ili waendelee kumtegemea fisadi huyu.
Kwani wasanii wote wangekuwa na kipato cha kuweza kusimama imara leo hii kauli kama ya Lady JD ingezungumzwa karibu na kila mwanabongoflava.

Fred Kavishe (fisadi mwingine) ambae anasimamia Kili music awards yuko bega kwa bega na Ruge kudanganya wananchi nani ni bora katika tuzo hizo ili kulinda maslahi yao binafsi.
Na wao huchagua wale wasanii ambao hawana sauti za kudai haki yao ili wawatumie kadri wanavyotaka.Tuzo za Kili ni uozo mtupu.Imefikia wakati basata itoe vibali kwa wadau wengine wa muziki (nako kuna ufisadi)wasio na interest binafsi na wasanii wao, kuendesha hizi shughuli ili kukuza muziki.Kutokuwepo na tuzo zingine kunasababisha ionekane kuwa basata nao wamo kwenye mgao wa mabepari hao wanaoua sanaa ya Tanzania

JINSI RUGE NA KUSAGA WANAVYOTAWALA
Njia anayoitumia Ruge na Kusaga iko wazi, wao wana redio na hapo hapo wana wasanii wao.Hivyo promotion inabidi wafanyie wasanii wao ambao ni waoga ili waweze kuwatumia bila wasanii hao kufanya fyoko fyoko.

Wasanii wengine ambao sio chini ya Clouds kwa kuwa hawana jinsi nyingine ya kupata hela inabidi wainyenyekee Clouds wakiamini ndio njia pekee ya kuwapatia vipato
Huku wakisubiri show moja ya fiesta ya kila mwaka.
Huko katika fiesta kuna wengine wanalipwa mpaka laki tatu na bado katika hiyo ili upangwe kwenye list ya kupanda jukwaani B12 nae lazima akate laki moja yake.
Hapo msanii anabakiwa na nini akirudi nyumbani?
Hivi laki tatu ni nini kwa maisha ya msanii?
Njia pekee ya kuwatawala ni kuwafanya waendelee kuwa maskini.
Leo hii mtangazaji wa redio ana sauti kuliko msanii.

Kwanini redio zingine hazilaumiwi? Ni kwa sababu hazijihusishi moja kwa moja na wasanii.Hilo ni kosa kubwa sana linalofanywa na Clouds au pengine ndio mtazamo wao walioamua kuufuata kwa sababu wanaamini Serikali ipo mikononi mwao.
Maisha na ajira za watoto wa watu ambao wengi hawajasoma wanategemea vipaji, mnayakatili bila huruma

Mwisho tumuombee Lady JD Mahakama imruhusu azungumze yote, kila mtu anataka kusikia sio siri Clouds, Ruge na Kusaga ni nyonya damu.
Mahakama itambue kuwa wanaojua maovu ya Rugen a Kusaga sio Lady JayDee pekee ni wengi mno na kama njia ya kukimbilia mahakamani ndio wameichagua basi ongezeni mahakama kwa kuwa tupo wengi tutakuja kuyaongea kuhusu mafisadi hawa wa Clouds (siku hizi wanaitwa wafu)
Hela ina nguvu hata palipo na haki, JD hajatukana matusi na amekuwa makini katika kutoa kauli zake sasa anashitakiwa kwa kosa gani? Anashitakiwa kwa kudai haki yake. Anaconda wewe songa na sisi tunakuja kizimbani na sasa ndio TANZANIA itawajua Rugen a Kusaga ni kina nani na walianzia wapi,walikuwa wapi,wako wapi na nani wanaoshirikiana nao

chanzo:https://www.facebook.com/antivirusvinega?hc_location=timeline